Kampanye ya Pekee Itakayoanza Tarehe 20 Mwezi wa 10 Mpaka Tarehe 16 Mwezi wa 11 Ili Kuwatolea Watu Trakti!
1 Kuanzia Siku ya Kwanza tarehe 20 mwezi wa 10 na kuendelea kwa muda wa majuma 4, tutashiriki katika kampanye ya pekee ya kugawia watu trakti mpya yenye kichwa Je, Ungependa Kujua Kweli? Tunatumaini kwamba kampanye hiyo ya pekee ya ulimwenguni pote itasaidia watu wengi zaidi wapendezwe na chanzo kimoja cha kweli.—Yoh. 17:17.
2 Trakti hiyo inatoa kwa kifupi majibu ya Biblia kwa maulizo sita ya maana yafuatayo: “Je, kweli Mungu anatuhangaikia?” “Je, vita na mateso vitakwisha wakati wowote?” “Ni Jambo gani linalotupata tunapokufa?” “Je, kuna tumaini lolote kwa wafu?” “Namna gani ninaweza kusali ili Mungu anisikie?” na “Ninaweza kufanya nini ili nipate furaha maishani?” Dini zinazojiita kuwa za Kikristo hazijapata kutoa majibu yenye kutosheleza kwa maulizo hayo. Hata watu wengi ambao si Wakristo wamejiuliza maulizo hayo, lakini labda hawajui kwamba Biblia inatoa majibu yaliyo wazi kwa maulizo hayo. Kwa hiyo, tunatumaini kwamba habari iliyo katika trakti hiyo itapendeza watu wengi.
3 Malizeni Eneo Lenu: Katika eneo lenu, mujikaze kuhubiri nyumba kwa nyumba munapotolea watu trakti hiyo. Ikiwa eneo lenu ni kubwa, wazee wanaweza kuwatia moyo muache trakti katika nyumba ambako hamukukuta watu. Mukumbuke kutolea trakti hiyo majirani, watu wa jamaa, watu munaofahamiana nao kwenye kazi ao shuleni, na wengine munaoongea nao kwa ukawaida. Labda munaweza kufanya mipango ili kufanya upainia msaidizi katika mwezi wa 10 ao mwezi wa 11. Je, wewe una mtoto ao mwanafunzi wa Biblia ambaye anafanya maendeleo ya kiroho na ambaye anastahili kushiriki pamoja nasi katika kampanye hiyo akiwa mhubiri asiyebatizwa? Ikiwa ni hivyo, julisha wazee.
4 Tutasema Nini: Ili kutolea watu wengi zaidi ujumbe, ni vizuri kufanya utoaji wetu uwe mfupi. Tunaweza tu kuuliza msikilizaji wetu ulizo moja kati ya maulizo sita yaliyo kwenye ukurasa wa kwanza na kumwonyesha jibu katika trakti. Hilo litasaidia kila mhubiri apatanishe utoaji wake na mahitaji ya watu walio katika eneo. Ikiwa mutu fulani anaonyesha kupendezwa, andika mambo fulani kumhusu na umurudilie wakati mwingine. Siku ya Posho na Siku ya Yenga tunaweza kutolea watu magazeti mapya pamoja na trakti. Kampanye itakapokwisha tarehe 16 mwezi wa 11, tutatolea watu kitabu Biblia Inafundisha. Trakti zitakazobaki zitatumiwa kama tunavyotumia trakti zingine zinazopatikana.
5 Tuanzishe Mafunzo ya Biblia: Trakti hiyo imetayarishwa hasa ili kutusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tunaporudilia mutu ambaye alionyesha kupendezwa, tunaweza kumuuliza ni kweli gani ya Biblia iliyomfariji? Tumwonyeshe ukurasa wa mwisho ambako mpango wa funzo la Biblia unaonyeshwa, na kumtolea kitabu Biblia Inafundisha. Ikiwa inawezekana, tuchunguze kwa kifupi fungu moja ao mafungu mawili katika sura yenye kuzungumzia zaidi habari ambayo alichagua.
6 Yehova anatafuta wale ambao watamwabudu kwa “roho na kweli.” (Yoh. 4:23) Basi, sisi wote na tushiriki katika kampanye hii ili kusaidia wengine wajue kweli!