Kampanye ya Pekee–Tarehe 16 Mwezi wa 10 Mpaka Tarehe 12 Mwezi wa 11!
1 “Mwisho wa Dini ya Uongo Unakaribia!” Hicho ndicho kichwa cha trakti Habari ya Ufalme Na. 37, ambayo tutagawanyia watu ulimwenguni pote kuanzia mwezi unaokuja. Kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 15 ya mwezi wa 10, tutatolea watu magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kuanzia Siku ya Kwanza, tarehe 16 mwezi wa 10, mpaka Siku ya Yenga, tarehe 12 mwezi wa 11, tutajitoa sana katika kugawanyia watu trakti Habari ya Ufalme Na. 37. Kwenye miisho-juma wakati wa kampanye, tutatolea watu trakti hiyo pamoja na magazeti.
2 Nani Anayeweza Kushiriki?: Wote wale wanaotangaza habari njema kwa bidii watajitoa sana ili kushiriki katika kampanye hiyo. Wahubiri fulani wanaweza kuwa mapainia wasaidizi. Je, una watoto au watu unaojifunza nao Biblia na wanaofanya maendeleo ya kiroho? Uwasaidie wazungumze na wazee ili kuona ikiwa wanastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa. Wazee wanapaswa kuchukua hatua ya kwanza ya kuongea na wahubiri wasiotenda ili kuwatia moyo washiriki katika kampanye, labda wakitumika na wahubiri wanaozoea kazi ya kuhubiri.
3 Trakti Habari ya Ufalme Na. 37 ni yenye kutumwa kwenye makutaniko yote ili wahubiri na mapainia waweze kupokea trakti 50 hivi. Watu wanaopendezwa na ambao hawajakuwa wahubiri wanaweza kupokea trakti tano ili kuzigawanyia washiriki wa familia zao na marafiki zao. Wahubiri wote wanapaswa kuchunga na kuandika hesabu ya trakti ambazo waliachia watu na kuandika hesabu hiyo nyuma ya fomu ya ripoti ya utumishi wa shambani (S-4) watakapotoa ripoti ya mwezi wa 10 na wa 11. Mwandishi atafanya hesabu ya jumla ya trakti zote ambazo wahubiri wote wa kutaniko walitolea watu na kutuma hesabu hiyo kwenye Betheli mwisho wa mwezi wa 10 na wa 11. Trakti yoyote Habari ya Ufalme itakayobakia kisha kampanye inaweza kutumiwa katika aina yoyote ya mahubiri.
4 Tutasema Nini?: Uwe na maneno mafupi, ili uweze kuachia watu wengi trakti. Unaweza kusema: “Ninaachia watu wote trakti hii yenye habari ya maana sana ambayo tunagawanyia watu ulimwenguni pote. Chukua trakti yako. Usikose kuisoma.” Inaweza kuwa vizuri uende katika mahubiri bila sakoshi wakati wa kugawanya trakti hiyo. Usikose kuandika kwenye karatasi majina ya watu wote waliopendezwa na habari iliyo kwenye trakti hiyo.
5 Jinsi ya Kutolea Kila Mtu Trakti Katika Eneo Lako: Kuliko kugawanya trakti Habari ya Ufalme barabarani, lingekuwa jambo nzuri zaidi kugawanya trakti hiyo katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba na katika eneo la biashara ikiwa hilo linawezekana. Andika namba za nyumba ambako haukukuta watu na jaribu kurudia wakati mwingine au siku nyingine. Kuanzia Siku ya Kwanza, tarehe 6 mwezi wa 11, tunaweza kuwaachia trakti hiyo wale ambao hatukuwakuta nyumbani. Hata hivyo, ikiwa kutaniko lina maeneo mengi ambayo wahubiri hawawezi kumaliza katika muda wa kampanye, wazee wanaweza kupendekeza kwamba trakti Habari ya Ufalme iachiwe watu ambao hawakuwa nyumbani wakati wote wa kampanye.
6 Uharibifu wa “Babiloni Mkubwa” unakaribia sana. Watu wanahitaji kutoka kwake kabla hajaharibiwa kabisa. (Ufu. 14:8; 18:8) Fanya mipango sasa ili ushiriki kabisa katika kampanye ya ulimwenguni pote ili kusaidia watu wote wajue kwamba mwisho wa dini ya uongo unakaribia!