Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv uku. 207-uku. 208 fu. 3
  • Namna ya Kuishi na Mutu Aliyetengwa na Kutaniko

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kuishi na Mutu Aliyetengwa na Kutaniko
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Onyesha Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Wakati Mupendwa Wako Anamuacha Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Tunapaswa Kumupenda Sana Yehova Kuliko Watu wa Familia Yetu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
Ona Habari Zaidi
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv uku. 207-uku. 208 fu. 3

NYONGEZA

Namna ya Kuishi na Mutu Aliyetengwa na Kutaniko

Inahuzunisha sana mutu wa familia ao rafiki yetu wa sana anapotengwa na kutaniko kwa sababu amefanya zambi nzito na amekosa kutubu. Tukifuata yale Biblia inasema kuhusu mupango huo, hilo litaonyesha kwamba tunamupenda kabisa Mungu na kwamba sisi tunashikamana kabisa na mipango yake.a Acha tuzungumuzie maulizo fulani kuhusu jambo hilo.

Namna gani tunapaswa kuishi na mutu aliyetengwa na kutaniko? Biblia inasema hivi: ‘Muache kuchangamana katika ushirika pamoja na mutu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni muasherati ao mutu mwenye pupa ao muabudu-sanamu ao mutukanaji ao mulevi ao munyanganyi, hata musikule chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.’ (1 Wakorintho 5:11) Kuhusu mutu yeyote ambaye ‘hakae katika fundisho la Kristo,’ Biblia inasema hivi: ‘Musimupokee kamwe nyumbani mwenu wala kumusalimu. Kwa maana yeye anayemusalimu anashiriki katika matendo yake maovu.’ (2 Yohana 9-11) Hatupaswe kuwa marafiki wa watu waliotengwa ao kuwa na uhusiano wowote wa kiroho pamoja nao. Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 9, 1981, kwenye ukurasa 25, ulisema hivi: “Kusema neno ndogo tu kama ‘Jambo’ (ao Habari?) kunaweza kuwa ndio hatua ya kwanza inayopanuka na kuwa mazungumuzo na hata kuwa urafiki. Je, utapenda kufanya hatua hiyo ya kwanza kuelekea mutu aliyetengwa?”

Je, tunapaswa kumuepuka kabisa? Jibu ni ndiyo, na kuna sababu zinazotuchochea kufanya hivyo. Sababu ya kwanza: kwa kufanya hivyo tunaonyesha ushikamanifu wetu kwa Mungu na Neno lake. Tunamutii Yehova wakati wote, iwe ni vyepesi ao hapana. Upendo wetu kwa Mungu unatuchochea kutii amri zake zote; tunatambua kama yeye ni Mungu mwenye haki, mwenye upendo, na kwamba sheria zake ni kwa faida yetu kabisa. (Isaya 48:17; 1 Yohana 5:3) Sababu ya pili: kumuepuka mutengwa kunatulinda sisi na pia ndugu wengine katika kutaniko ili hali yetu ya kiroho na mwenendo wetu usiambukizwe, na ili kutaniko lisitukanwe. (1 Wakorintho 5:6, 7) Sababu ya tatu: tukishikamana kabisa na kanuni za Biblia, hilo linaweza kumusaidia mutengwa. Tukiunga mukono uamuzi wa halmashauri ya hukumu, labda hilo linaweza kugusa moyo wa mukosaji ambaye hakutubu wakati wazee walikuwa wanajaribu kumusaidia. Kupoteza urafiki na watu aliopenda kunaweza kumusaidia arudiwe na “fahamu zake” ao mawazo mazuri, aone uzito wa zambi yake, na achukue hatua za kumurudilia Yehova.—Luka 15:17.

Tutafanya nini na mutu wa familia aliyetengwa? Katika hali kama hiyo upendo wa kifamilia unaweza kuwa jaribu kali la uaminifu wetu. Tunapaswa kuishi namna gani na mutu wa familia aliyetengwa? Ni vigumu kuzungumuzia hapa kila hali inayoweza kutokea, hata hivyo, acha tuzungumuzie hali mbili.

Wakati fulani, labda mutengwa bado anaishi nyumba moja na wazazi wake na ndugu zake na pia dada zake. Kwa kuwa kutengwa hakuvunje familia, tunaweza kuendelea kufanya mambo ya kawaida ya familia na mutu huyo. Hata hivyo, kumbuka kwamba kupitia mwenendo wake, mutu huyo amechagua kuvunja uhusiano wa kiroho kati yake na watu wa familia ambao ni Mashahidi. Kwa hiyo, watu wa familia ambao ni waaminifu hawataendelea kujiunga naye katika mambo ya kiroho. Kwa mufano, akiwa hapo wakati familia inakutana ili kujifunza Biblia, atakaa tu kimya, hatasema wala kufanya jambo lolote. Lakini, ikiwa mutengwa ni mutoto wa chini ya miaka 18, wazazi wake wangali na daraka la kumufundisha na kumuadibisha. Kwa hiyo, wazazi wenye upendo wanaweza kufanya mipango ya kuendelea kujifunza naye.b—Methali 6:20-22; 29:17.

Wakati mwengine, labda mutengwa anaishi kwake mbali na wazazi wake na pia ndugu ao dada zake. Hata ikiwa labda wakati fulani-fulani kunaweza kuwa lazima ya kuchangamana naye ili kushugulikia mambo fulani ya familia, hilo halipaswe kuwa zoezi. Wakristo waaminifu walio katika familia hiyo hawatatafuta visababu vya kuchangamana na ndugu yao mutengwa ambaye haishi nao nyumba moja. Ushikamanifu wao kwa Yehova na kwa tengenezo lake utawachochea kuunga mukono mupango wa Kimaandiko wa kumutenga mutu huyo. Ushikamanifu wao ni alama ya kwamba wanatafuta faida zake na hilo linaweza kumusaidia afaidike na nizamu aliyopata.c—Waebrania 12:11.

a Kanuni za Biblia kuhusu mutu anayetengwa na kutaniko zinamuhusu pia mutu anayejitenga mwenyewe na kutaniko.

b Ili kupata habari zaidi kuhusu watoto wa chini ya miaka 18 waliotengwa na ambao wanaishi pamoja na wazazi wao, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 2001, ukurasa wa 16-17, na ule wa tarehe 15 Mwezi wa 11, 1988, ukurasa wa 20.

c Ili kupata habari zaidi kuhusu namna ya kuishi na mutu wa familia aliyetengwa, soma mashauri ya Biblia katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 1988, ukurasa wa 26-31, na ule wa tarehe 15 Mwezi wa 9, 1981, ukurasa wa 26-31.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine