Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/02 uku. 3-4
  • Onyesha Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Onyesha Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kuishi na Mutu Aliyetengwa na Kutaniko
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Wakati Mupendwa Wako Anamuacha Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Tunapaswa Kumupenda Sana Yehova Kuliko Watu wa Familia Yetu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 8/02 uku. 3-4

Onyesha Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo Mtu wa Jamaa Anapotengwa na Ushirika

1. Ni hali gani inayoweza kujaribu uaminifu-mshikamanifu wa Mkristo?

1 Kifungo kati ya washiriki wa familia kinaweza kuwa chenye nguvu sana. Hilo linaleta jaribu kwa Mkristo wakati mwenzi wa ndoa, mtoto, mzazi, au mtu mwingine wa jamaa ya karibu anapotengwa au anapojitenga mwenyewe na ushirika wa kutaniko. (Mt. 10:37) Wakristo waaminifu-washikamanifu wanapaswa kumtendeaje mtu wa jamaa kama huyo? Je, mtu huyo anapaswa kutendewa kwa njia tofauti ikiwa anaishi nyumbani mwako? Kwanza, acheni turudilie yale ambayo Biblia inasema kuhusu habari hiyo, tukikumbuka kwamba kanuni za Biblia zinatumika kwa namna ileile kwa wale wanaotengwa na wale wanaojitenga wenyewe na ushirika.

2. Kulingana na Biblia, Wakristo wanapaswa kuwatendeaje wale waliotengwa na ushirika wa kutaniko?

2 Jinsi ya Kutendea Wale Waliotengwa na Ushirika: Neno la Mungu linaamuru Wakristo wasiendelee kushirikiana na mtu aliyetengwa na ushirika wa kutaniko: “Mkome kuchangamana katika ushirika pamoja na yeyote aitwaye ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi, wala hata kula pamoja na mtu wa namna hiyo. . . . Ondoeni yule mtu mwovu miongoni mwenu wenyewe.” (1 Kor. 5:11, 13) Maneno ya Yesu yanayoandikwa kwenye Mathayo 18:17 ni yenye maana pia: “Mwache [yule aliyetengwa] awe kwako kama vile mtu wa mataifa na kama mkusanya-kodi.” Wasikilizaji wa Yesu walijua vizuri kwamba Wayahudi wa wakati huo hawakushirikiana hata kidogo na watu Wasio Wayahudi na kwamba waliepuka watoza-kodi kuwa watengwa. Hivyo, Yesu alikuwa akiwaagiza wafuasi wake wasishirikiane na watengwa.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1982, ukurasa wa 9-11.

3, 4. Ni aina gani ya ushirika pamoja na watu waliotengwa au waliojitenga wenyewe inayokatazwa?

3 Hilo linamaanisha kwamba Wakristo waaminifu-washikamanifu hawana ushirika wa kiroho na yeyote aliyetengwa na ushirika wa kutaniko. Lakini mengi zaidi yanahusika. Neno la Mungu linasema kwamba hatupaswi “hata kula pamoja na mtu wa namna hiyo.” (1 Kor. 5:11) Kwa sababu hiyo, tunaepuka pia ushirika wa kirafiki pamoja na mtu aliyetengwa. Hilo litatufanya tusijiunge naye kwenye karamu, mchezo wa mpira, kusafiri pamoja ili kununua vitu dukani, au kukaa kwenye mlo pamoja naye nyumbani au katika mkahawa.

4 Namna gani kuhusu kusema na mtu aliyetengwa na ushirika? Ingawa Biblia haizungumzii kila hali inayoweza kutokea, andiko la 2 Yohana 10 linatusaidia tuwe na maoni ya Yehova kuhusu mambo: “Ikiwa yeyote aja kwenu na haleti ufundishaji huu, msimpokee kamwe nyumbani mwenu wala kusema salamu kwake.” Ukitoa maelezo kuhusu jambo hilo, Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1982, ukurasa wa 17, unasema: “Kusema neno fupi tu la “Jambo” (Habari?) kunaweza kuwa ndiyo hatua ya kwanza inayopanuka na kuwa mazungumzo na hata kuwa urafiki. Je! tungetaka kuichukua hatua hiyo ya kwanza kumwelekea mtu aliyetengwa na ushirika?”

5. Anapotengwa na ushirika, mtu anapoteza nini?

5 Kwa kweli, ni kama ukurasa wa 23 wa toleo hilohilo la Mnara wa Mlinzi unavyosema: “Jambo la uhakika ni kwamba wakati Mkristo anapojiacha atende dhambi kisha inakuwa lazima atengwe na ushirika, yeye anapoteza mambo mengi: msimamo wake wenye kukubaliwa na Mungu; . . . ushirika mtamu pamoja na kina ndugu, kutia na mwingi wa ushirika aliokuwa nao pamoja na watu wa ukoo wake walio Wakristo.”

6. Je, Mkristo anaombwa kukata ushirikiano wote na mtu wa jamaa aliyetengwa na ushirika? Eleza.

6 Kuishi Katika Nyumba Moja: Je, hilo linamaanisha kwamba Wakristo wanaoishi katika nyumba moja na mshiriki wa familia aliyetengwa na ushirika wanapaswa kuepuka kuzungumza naye, kula naye, na kushirikiana na mtu huyo wanapotimiza shughuli zao za kila siku? Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1991, katika kielezi-chini kwenye ukurasa wa 22, unaeleza: “Ikiwa katika nyumba ya Kikristo kuna mtu wa ukoo ambaye ametengwa na ushirika, yeye bado angekuwa sehemu ya kawaida ya shughuli na utendaji wa kinyumbani wa kila siku.” Hivyo, washiriki wa familia wataachiwa uhuru wa kuamua ni kwa kiasi gani mshiriki wa familia aliyetengwa na ushirika anaweza kuhusishwa wakati wa kula au kuhusika katika shughuli nyingine za nyumbani. Na hata hivyo, hawangependa kufanya ndugu wanaoshirikiana nao wawe na maoni kwamba mambo ni kama yalivyokuwa kabla ya mtu huyo kutengwa na ushirika.

7. Ushirikiano wa kiroho nyumbani unabadilikaje mshiriki wa familia anapotengwa na ushirika?

7 Hata hivyo, Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1982, ukurasa wa 20, unasema hivi kuhusu mtu aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe na ushirika: “Uhusiano wa kiroho uliokuwapo umezuiwa kabisa. Ndivyo ilivyo hata kuhusiana na watu wa ukoo wake, kutia na wale walio ndani ya jamaa iyo hiyo ya karibu. . . . Hiyo itamaanisha wafanye mabadiliko katika ushirika wa kiroho ambao huenda ulikuwa katika jamaa hiyo. Kwa mfano, mume akitengwa na ushirika, mkewe na watoto hawatafurahia kumwacha awaongoze katika funzo la jamaa la Biblia wala katika usomaji wa Biblia na sala. Ikiwa yeye anataka kutoa sala, kama vile wakati wa kula, yeye ana haki ya kufanya hivyo katika nyumba yake mwenyewe. Lakini wao wanaweza kumtolea Mungu kwa kimya sala zao wenyewe. (Mit. 28:9; Zab. 119:145, 146) Namna gani ikiwa mtu aliyetengwa na ushirika katika nyumba hiyo anataka kuwapo wakati jamaa inaposoma Biblia pamoja au inapokuwa na funzo la Biblia? Wale wengine wanaweza kumwacha awepo asikilize ikiwa hatajaribu kuwafundisha au kuwatolea maoni yake ya kidini.”

8. Wazazi wana daraka gani kuelekea mtoto mdogo aliyetengwa na ushirika lakini ambaye anaishi nyumbani?

8 Ikiwa mtoto mdogo anayeishi nyumbani anatengwa na ushirika, wazazi Wakristo bado wana daraka la kumlea. Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1988, ukurasa wa 20, unaeleza: “Sawa na vile ambavyo wao wataendelea kumwandalia chakula, nguo, na makao, wao wanahitaji kumwagiza na kumtia nidhamu kupatana na Neno la Mungu. (Mithali 6:20-22; 29:17) Hivyo wazazi wenye upendo wangeweza kupanga kuwa na funzo la Biblia la kimaskani pamoja naye, hata ikiwa anatengwa na ushirika. Labda atapata manufaa iliyo na usahihisho mkubwa zaidi kutokana na kujifunza kwao pamoja naye akiwa peke yake. Au wangeweza kuamua kwamba yeye anaweza kuendelea kushiriki mpango wa funzo la jamaa.”—Ona pia Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 2001, ukurasa wa 16-17.

9. Ni kwa kiasi gani Mkristo anapaswa kupashana habari na mtu wa jamaa aliyetengwa na ushirika lakini anayeishi nje ya nyumba?

9 Watu wa Jamaa Wasioishi Nyumbani: Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1988, ukurasa wa 28, unasema: “Hali hii ni tofauti ikiwa yule ambaye ametengwa na ushirika au amejitenga na ushirika ni mtu wa ukoo anayeishi nje ya jamaa ile ya pale pale. Labda ingewezekana kuzuia karibu mawasiliano yote pamoja na mtu huyo wa ukoo. Hata kama kuna mambo fulani ya kijamaa yanayotaka mawasiliano, kwa uhakika yanapaswa kuwekwa katika kadiri ndogo kabisa.” Hilo linapatana na ile amri ya kimungu ya ‘kukoma kuchangamana katika ushirika pamoja na yeyote’ ambaye ana hatia ya kufanya dhambi bila kutubu. (1 Kor. 5:11) Wakristo waaminifu-washikamanifu wanapaswa kujitahidi kuepuka ushirikiano usio wa lazima na mtu wa jamaa kama huyo, hata kushughulika na mambo ya biashara pamoja naye kwa kadiri ndogo sana.—Ona pia Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1982, ukurasa wa 21-22.

10, 11. Mkristo atafikiria nini kabla ya kumruhusu mtu wa jamaa aliyetengwa na ushirika arudi nyumbani?

10 Mnara wa Mlinzi unazungumzia hali nyingine inayoweza kutokea: “Namna gani ikiwa mtu wa ukoo wa karibu, kama vile mwana au mzazi asiyeishi katika nyumba hiyo, ametengwa na ushirika na baada ya hapo anataka kurudi aishi pamoja nao? Jamaa hiyo inaweza kuamua jambo la kufanya kwa kutegemea ni hali gani iliyopo. Kwa mfano, huenda aliyetengwa na ushirika akawa ni mgonjwa au hawezi tena kujitunza mwenyewe kwa upande wa pesa au kimwili. Watoto Wakristo wana wajibu wa Maandiko na wa adili kumsaidia. (1 Tim. 5:8) . . . Jambo la kufanya huenda likategemea mambo kama mahitaji ya kweli ya mzazi huyo, nia yake na heshima ambayo kichwa cha jamaa kinayo kwa hali ya kiroho ya jamaa.”—Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1982, ukurasa wa 21.

11 Kwa habari ya mtoto, makala hiyohiyo inaendelea: “Nyakati nyingine wazazi Wakristo wamemkubali arudi nyumbani kwa muda fulani mtoto aliyetengwa na ushirika ambaye amekuwa mgonjwa sana kimwili au katika mawazo yake ya moyoni. Lakini katika kila kisa wazazi wanaweza kuzipima hali za mtu huyo waone ziko namna gani. Je! mwana aliyetengwa na ushirika amekuwa akiishi kwa kujitegemea mwenyewe, na je! sasa hawezi kufanya hivyo? Au yeye anataka kurudi nyumbani kwa sababu hasa akirudi maisha yatakuwa mepesi zaidi? Nazo tabia zake na nia yake iko namna gani? Je! ataingiza ‘chachu’ nyumbani?—Gal. 5:9.”

12. Ni nini faida fulani zinazotokana na mpango wa kutenga na ushirika?

12 Faida za Kuwa Mwaminifu-Mshikamanifu kwa Yehova: Kushirikiana na mpango wa Kimaandiko wa kutenga na ushirika na kuepuka wakosaji wasiotubu ni jambo lenye manufaa. Kunalinda usafi wa kutaniko na kunatutofautisha kwa kuonyesha kwamba tunategemeza viwango vya adili vya Biblia vilivyo vya juu. (1 Pet. 1:14-16) Kunatulinda dhidi ya uvutano wenye kuharibu. (Gal. 5:7-9) Kunatolea pia mkosaji nafasi ya kufaidika kikamili na nidhamu aliyopokea, ambayo inaweza kumsaidia kuzaa “tunda lenye kufanya amani, yaani, uadilifu.”—Ebr. 12:11.

13. Ni rekebisho gani ambalo familia moja ilifanya, na tokeo lilikuwa nini?

13 Baada ya kusikiliza hotuba kwenye kusanyiko la mzunguko, ndugu moja na dada yake pacha walitambua kwamba walihitaji kufanya marekebisho katika namna walivyomtendea mama yao, aliyeishi mahali pengine na ambaye ametengwa na ushirika kwa miaka sita. Baada tu ya kusanyiko, mwanamume huyo akamwita mama yake, na baada ya kumhakikishia upendo wao, akamweleza kwamba hawangemsemesha tena isipokuwa kuna mambo ya maana ya familia yanayoomba kupashana habari. Upesi baadaye, mama yake akaanza kuhudhuria mikutano na mwishowe akarudishwa. Mume wake asiyeamini alianza pia kujifunza na baadaye akabatizwa.

14. Sababu gani tunapaswa kutegemeza kwa uaminifu-mshikamanifu mpango wa kutenga na ushirika?

14 Kutegemeza mpango unaoonyeshwa katika Maandiko wa kutenga na ushirika kunaonyesha upendo wetu kwa Yehova na kunatoa jibu kwa yule anayemlaumu Yeye. (Mez. 27:11) Kama tokeo, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatubariki. Mfalme Daudi aliandika kuhusu Yehova: “Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu; sikuacha amri zake. Kwa [mwaminifu] utajionyesha kama [mwaminifu].”—2 Sam. 22:23, 26.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine