Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ll sehemu 8 uku. 18-19
  • Kifo cha Yesu Kitakuletea Faida Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kifo cha Yesu Kitakuletea Faida Gani?
  • Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sehemu ya 8
    Umusikilize Mungu
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Kutakuwa Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
ll sehemu 8 uku. 18-19

SEHEMU YA 8

Kifo cha Yesu Kitakuletea Faida Gani?

Yesu alikufa ili tupate uzima. Yohana 3:16

Wanamuke wanaangalia kaburi la Yesu lenye kuwa wazi

Siku tatu kisha Yesu kufa, wanamuke fulani walienda ku kaburi lake na wakakuta liko wazi. Yehova alikuwa amemufufua Yesu.

Yesu anatokea mitume wake, kisha wakati fulani anapanda mbinguni

Kisha, Yesu alitokea mitume wake.

Kwa kweli, Yehova alimufufua Yesu; alikuwa sasa malaika mwenye nguvu na mwenye hawezi kufa. Wanafunzi wa Yesu walimuona wakati alipanda mbinguni.

  • “Mushahara” wa zambi ni nini?​—Waroma 6:23.

  • Yesu alifungua njia yenye kuongoza kwenye uzima wa milele.​—Waroma 5:21.

Mungu alimufufua Yesu na akamufanya kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Danieli 7:13, 14

Yesu iko kwenye kiti chake cha Ufalme na Yesu anatawala watu mu dunia paradiso

Yesu alitoa uzima wake ili kulipia wanadamu bei ya ukombozi. (Matayo 20:28) Kupitia ile bei ya ukombozi, Mungu alifanya iwezekane tuishi milele.

Yehova alimufanya Yesu kuwa Mufalme ili atawale dunia. Atakuwa pamoja na watu waaminifu 144000 wenye wanafufuliwa ili waende kuishi mbinguni. Yesu na wale 144000 njo wenye watafanyiza serikali ao guvernema ya mbinguni yenye itatawala kwa haki, ni kusema, Ufalme wa Mungu.​—Ufunuo 14:1-3.

Ufalme wa Mungu utafanya dunia ikuwe paradiso. Hakutakuwa tena vita, kuvunja sheria, umaskini, na njaa. Watu watakuwa na furaha kabisa.​—Zaburi 145:16.

  • Ufalme wa Mungu utaleta baraka gani?​—Zaburi 72.

  • Tunapaswa kusali Ufalme wa Mungu ukuje.​—Matayo 6:10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine