Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jl somo 10
  • Ibada ya Familia Ni Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ibada ya Familia Ni Nini?
  • Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mumuabudu Yehova Katika Familia
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo 10

SOMO LA 10

Ibada ya Familia Ni Nini?

Familia moja inafanya ibada ya familia

Korea Kusini

Bibi na bwana wanajifunza Biblia pamoja

Brazili

Shahidi mumoja wa Yehova anajifunza Biblia

Australia

Familia moja inazungumuzia habari fulani ya Biblia

Guinea

Kuanzia wakati wa zamani, Yehova anapenda watu wa kila familia wakuwe na wakati wa kujifunza pamoja ili wakuwe na urafiki wenye nguvu pamoja naye, na ili wakuwe na uhusiano wenye nguvu sana kati yao. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Njo maana, kila familia ya Mashahidi wa Yehova inapanga wakati fulani kila juma ili kumuabudu Yehova pamoja. Wakati huo, mu hali yenye kutulia, wanazungumuzia mambo ya kiroho yenye inapatana na mahitaji ya familia yao. Hata kama unaishi peke yako, unaweza kupanga wakati kama huo ili kumukaribia Mungu zaidi kwa kujifunza habari fulani ya Biblia yenye unapenda.

Ni wakati wa kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Biblia inasema hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Tunamujua Yehova muzuri wakati tunajifunza mambo mingi juu ya sifa zake na matendo yake kupitia Biblia, Neno lake. Namna ya mwepesi ya kuanza ibada ya familia ni kusoma Biblia pamoja kwa sauti kubwa, pengine kwa kufuata programu ya kila juma ya Mukutano Utumishi na Maisha. Kila mutu wa familia anaweza kupewa sehemu ya kusoma, na kisha ninyi wote munaweza kuzungumuzia mambo yenye mumejifunza mu Maandiko.

Ni wakati wa kutia nguvu uhusiano kati ya watu wa familia. Bibi na bwana, pia wazazi na watoto, wanatia nguvu uhusiano kati yao wakati wanajifunza Biblia mu familia. Wakati wa ibada ya familia unapaswa kuwa wakati wa furaha na amani, wakati wenye kila mutu mu familia anangojea kwa hamu katika juma. Kupatana na miaka ya watoto wao, wazazi wanaweza kuchagua habari za kuzungumuzia zenye zinapatana na mahitaji ya watoto wao. Pengine wanaweza kutumia habari za Munara wa Mulinzi na Amuka! ao habari zenye kuwa ku site yetu ya Enternete, jw.org. Munaweza kuzungumuzia magumu yenye watoto walipata ku masomo na kuwasaidia wajue namna ya kupambana na ile magumu. Munaweza kuangalia programu ya JW Télédiffusion (tv.jw.org) na kuizungumuzia pamoja. Munaweza kujifunza nyimbo zenye mutaimba ku mikutano, na munaweza kula ao kunywa kitu fulani kisha ibada ya familia.

Wakati huo wa maana wenye munapitisha pamoja kila juma ili kumuabudu Yehova, utasaidia kila mutu mu familia afurahie kujifunza Neno la Mungu, na Yehova atabariki sana bidii yenu.​—Zaburi 1:1-3.

  • Juu ya nini tunapanga wakati wa kufanya ibada ya familia?

  • Wazazi wanaweza kufanya nini ili kila mutu mu familia afurahie wakati huo?

ILI KUJUA MAMBO MINGI

Uliza ndugu na dada wengine mu kutaniko lenu namna wanafanyaka ibada yao ya familia. Tena, tafuta ku Jumba la Ufalme vichapo vyenye unaweza kutumia ili kufundisha watoto wako juu ya Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine