Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 6 uli. 1-5
  • Kuko Tumaini Gani Juu ya Watu Wenye Wamekufa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuko Tumaini Gani Juu ya Watu Wenye Wamekufa?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Wafu Wana Tumaini Lolote?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tumaini la Kweli juu ya Watu Tuliowapenda Waliokufa
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Wafu Wako mu Hali Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 6 uli. 1-5

SOMO LA 6

Kuko Tumaini Gani Juu ya Watu Wenye Wamekufa?

1. Kuko habari gani njema juu ya watu wenye wamekufa?

Martha na Maria wanamukaribisha kaka yao Lazaro ambaye amefufuliwa

Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alikuwa na rafiki yake mwenye aliitwa Lazaro, mwenye alikuwa anaishi Betania karibu na Yerusalemu. Siku moja Lazaro alikufa, na Yesu akafika Betania siku ine kisha Lazaro kufa. Yesu alienda ku kaburi pamoja na Marta na Maria, dada za Lazaro. Bila kukawia, watu wengi sana walikuja pale. Wazia namna Marta na Maria walifurahi sana wakati Yesu alimufufua Lazaro!​—Soma Yohana 11:21-24, 38-44.

Tayari Marta alikuwa anajua habari njema juu ya watu wenye wamekufa. Alijua kama Yehova atawafufua ili waishi tena ku dunia.​—Soma Yobu 14:14, 15.

2. Watu wenye wamekufa wako mu hali gani?

Adamu anaumbwa, na baadaye anakufa

Mungu alimuambia Adamu hivi: “Wewe ni mavumbi na utarudia katika mavumbi.”​—MWANZO 3:19.

Mungu alituumba kwa kutumia mavumbi. (Mwanzo 2:7; 3:19) Hakuna roho yenye haiwezi kufa yenye kuishi ndani ya mwili wetu. Sisi ni viumbe wa kimwili, wakati tunakufa hakuna sehemu yenye inatoka mu mwili wetu na kuendelea kuishi mahali fulani. Wakati tunakufa, ubongo wetu unakufa pia, na mawazo yetu inapotea. Njo maana wakati Lazaro alifufuka, hakusema kama aliona mambo fulani ao alikuwa mahali fulani, kwa sababu watu wenye wamekufa hawajue kitu chochote.​—Soma Zaburi 146:4; Muhubiri 9:5, 6, 10.

Kisha watu kufa, Mungu anawatesa mu moto? Biblia inafundisha kama watu wenye wamekufa hawajue kitu chochote. Kwa hiyo, watu wenye wanafundisha fundisho la uongo la moto wa mateso wanamusingizia Mungu mambo ya uongo. Kwanza wazo tu la kutesa watu mu moto linamuchukiza Mungu sana.​—Soma Yeremia 7:31.

Angalia video Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?

3. Watu wenye wamekufa, wanaweza kuzungumuza na sisi?

Watu wenye wamekufa hawawezi kuzungumuza na hawawezi kusikia. (Zaburi 115:17) Lakini kuko malaika fulani wabaya, na malaika hao wanaweza kuzungumuza na watu kwa kujifanya kuwa kama watu hao wenye wamekufa. (2 Petro 2:4) Yehova anatukataza kabisa tusipime kuzungumuza na watu wenye wamekufa.​—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10, 11.

4. Ni nani wenye watafufuliwa?

Mwanaume aliyefufuliwa ili kuishi katika Paradiso anafundishwa juu ya Mungu. Kisha mwanaume huyo anasaidia kuwafundisha wengine waliofufuliwa.

Mamilioni ya watu wenye kuwa mu makaburi watafufuliwa ili waishi ku dunia. Hata watu fulani wenye hawakumujua Mungu na wenye walifanya mambo ya mubaya watafufuliwa.​—Soma Luka 23:43; Matendo 24:15.

Wale wenye watafufuliwa watapewa nafasi ya kujifunza juu ya Mungu na kuonyesha imani yao katika Yesu kwa kumutii ao kumusikia. (Ufunuo 20:11-13) Wale wenye watafufuliwa na kufanya mambo ya muzuri watapata uzima wa milele ku dunia.​—Soma Yohana 5:28, 29.

5. Ufufuo unatufundisha nini juu ya Yehova?

Kwa sababu Mungu alimutuma Mwana wake ili akufe kwa ajili yetu, jambo hilo linatupatia tumaini kama watu wenye wamekufa watafufuliwa. Kwa hiyo, ufufuo unatufundisha kama Yehova anatupenda na anatuonyesha fazili zake zenye hazistahiliwe. Wakati watu wenye wamekufa watafufuliwa, utapenda sana kuona nani?​—Soma Yohana 3:16; Waroma 6:23.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 6, 7 na 10 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine