Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 29
  • Wafu Wako mu Hali Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wafu Wako mu Hali Gani?
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • Watu Waliokufa Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Kuko Tumaini Gani Juu ya Watu Wenye Wamekufa?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Tunaenda Wapi Wakati Tunakufa?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ni Nini Hutokea Wakati Wa Kifo?
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 29
Somo ya 29. Bibi na bwana wako nasali mbele ya kaburi.

SOMO YA 29

Wafu Wako mu Hali Gani?

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Ulishakafiwa? Mu ile wakati ya huzuni sana, unaweza kujiuliza: ‘Wakati mutu anakufa, anakuwaka mu hali gani? Kuko siku tutamuonaka tena?’ Mu hii somo na mu somo ya kufuata, tutaona namna Biblia inajibia ile maulizo. Majibu yenye Biblia inatoa, inaweza kututia moyo.

1. Wakati mutu anakufa, anakuwaka mu hali gani?

Yesu alisemaka kama kifo iko sawa vile usingizi. Mutu mwenye analala sana, hajuake mambo yenye iko napitikana pembeni yake. Kifo nayo ni vile. Mutu mwenye alishakufa, hasikiake maumivu. Hata kama alikuwa napenda sana watu wa familia yake na marafiki wake, hawezi kuwakumbuka. Biblia inasema hivi: “Wafu hawajue kitu chochote.”​—Soma Muhubiri 9:5.

2. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida gani?

Watu wengi wanaogopaka kifo, na wanaogopaka hata wafu. Lakini, mambo yenye Biblia inasema juu ya kifo inaweza kukutuliza. Yesu alisema hivi: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Dini za mingi zinafundishaka kama mutu anakuwaka na nafsi ao roho yenye inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa. Lakini Biblia haifundishe vile. Hakuna mutu mwenye anatesekaka kisha kufa. Tena, wafu hawajue kitu. Njo maana, hawawezi kututendea mubaya. Kwa hiyo, hatupaswe kuabudu wafu ao kuwafanyia mambo fulani juu ya kuwaza kama, ikiwa hatuwafanyie vile, watakasirika. Na hatupaswe kuwaombea.

Watu fulani wanasemaka kama wanaweza kuzungumuza na wafu. Lakini ile haiwezekane. Sawa vile tumejifunza, wafu “hawajue kitu chochote.” Mutu mwenye anawaza kama iko nazungumuza na mutu mwenye alishakufa, inawezekana iko njo nazungumuza na pepo wachafu, juu pepo wachafu wanajifanya kuwa sawa vile watu wenye walishakufa. Njo maana, kujua kweli juu ya hali ya wafu kunaweza kutulinda juu pepo wachafu wasitudanganye. Yehova anatushauria tusipime kuzungumuza na wafu juu anajua kama wakati tunafanya vile, tuko njo nazungumuza na pepo wachafu. Na wale pepo wachafu wanaweza kututendea mubaya.​—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-​12.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo ingine yenye Biblia inafundisha juu ya hali ya wafu na tuone mambo yenye inahakikisha kama Mungu mwenye upendo hawezi kutesa watu wenye walishakufa.

Mwanaume na watoto wake wawili wanamuke wanakaa ku kiti ku maziko ya bibi yake na mama ya watoto wake. Watu wa familia na marafiki wako pembeni yao juu ya kuwatia moyo na kuwatuliza.

3. Kweli juu ya hali ya wafu

Mu dunia yote watu wanaamini mambo mbalimbali juu ya hali ya wafu. Lakini haiko ile mambo yote njo ya kweli.

  • Fasi kwenye unaishi watu wanasemaka wafu wako mu hali gani?

Juu ya kuona mambo yenye Biblia inafundisha, muangalie VIDEO.

VIDEO: Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?​—Sehemu (1:19)

Picha: Picha za mu video ‘Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?​—Sehemu.’ 1. Maiti iko ku kitanda ya hopitali. 2. Mwanaume anasinzia katikati ya watu mbili wakati iko anasafiri mu treni.

Musome Muhubiri 3:20, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Vile ile andiko inaonyesha, mutu mwenye alishakufa iko mu hali gani?

  • Mutu anakuwaka na sehemu fulani yenye inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa?

Biblia inazungumuzia kifo ya Lazaro, rafiki ya Yesu wa sana. Musome Yohana 11:11-​14. Wakati munasoma ile andiko, angalia mambo yenye Yesu alisema juu ya hali yenye Lazaro alikuwa ndani. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yesu alionyesha kama kifo iko sawa nini?

  • Ile inatufundisha nini juu ya hali ya wafu?

  • Unaona namna gani mafasirio yenye Biblia inatoa juu ya hali ya wafu?

4. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida

Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatusaidia tusikuwe tunaogopa wafu. Musome Muhubiri 9:10, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wafu wanaweza kututendea mubaya?

Tena, kujua kweli ya Biblia kunatusaidia tusiamini mafundisho yenye kusema kama tunapaswa kuabudu wafu ao kuwafanyia mambo fulani juu wasikasirike. Musome Isaya 8:19 na Ufunuo 4:11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati mutu anaabudu ao anatafuta musaada wa mutu mwenye alishakufa?

PIcha: Desturi yenye kuhusiana na ibada ya wafu. 1. Mwanaume anapiga magoti na kusali mbele ya kaburi na iko na chakula ya kutolea wafu. 2. Wanaume wa kabila wako nacheza dansi na wamevala nguo za kwao. 3. Watu wanavaa maske na wanabeba vitu vyenye kuwa na umbo ya mifupa ya watu Siku ya Kukumbuka Wafu.

Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatusaidia tuachane na desturi zenye hazimufurahishe Yehova

5. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatutuliza

Watu wengi wamefundishwa kama, ikiwa wanakufa, watateseka juu ya mambo ya mubaya yenye walifanyaka zamani. Lakini, inatuliza sana kujua kama hakuna mutu mwenye anatesekaka kisha kufa, hata mutu mwenye alikuwa nafanya mambo ya mubaya sana. Musome Waroma 6:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia inasema kama mutu mwenye anakufa, analipia zambi zake zote. Kama ni vile, unawaza mutu mwenye alishakufa iko nateseka juu ya makosa yake ya zamani?

Wakati tunaendelea kumujua Yehova muzuri zaidi, tunafikia kuona kama hawezi hata kidogo kutesa wafu. Musome Kumbukumbu la Torati 32:4 na 1 Yohana 4:8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza Mungu mwenye iko na sifa zenye hii maandiko inazungumuzia anaweza kabisa kutesa watu wenye walishakufa?

  • Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuliza? Juu ya nini?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Ninaogopaka mambo yenye itanifikia siku nitakufa.”

  • Kama mutu anasema vile, unaweza kumupatia andiko gani ya kumutuliza?

KWA KIFUPI

Wakati mutu anakufa, maisha yake inaishia pale. Wafu hawatesekake na hawawezi kututendea mubaya.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wafu wako mu hali gani?

  • Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida gani?

  • Juu ya nini kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatutuliza?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Biblia inafasiria neno “nafsi.”

“Nafsi Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona ikiwa Mungu anatesaka watu wabaya mu moto wa mateso.

Kuko Moto wa Mateso? (3:07)

Tunapaswa kuogopa wafu?

Roho za Wafu​—Zinaweza Kukusaidia ao Kukutendea Mubaya? Zinakuwaka Kabisa? (broshua)

Ona namna kujifunza kweli juu ya hali ya wafu kulituliza mwanaume fulani.

“Nilifurahia Majibu ya Biblia Yenye Kuwa Wazi, na Yenye Kueleweka” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 2, 2015)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine