Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 7 uku. 16-17
  • Unajisikia Kuwa Peke Yako na Mwenye Kuogopa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unajisikia Kuwa Peke Yako na Mwenye Kuogopa?
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Kuna Wakati Unapojihisi Mpweke na Mwenye Woga?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mungu Wake Alimufariji
    Tuige Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yehova Alitia Eliya Moyo
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 7 uku. 16-17
Kijana mumoja mwanaume anajisikia kuwa peke yake na anaogopa

SOMO LA 7

Unajisikia Kuwa Peke Yako na Mwenye Kuogopa?

Angalia picha hii. Mutoto huyu anaonekana kuwa peke yake na mwenye kuogopa. Si vile? Weye pia umekwisha kujisikia vile wakati fulani?— Kuko wakati kila mutu anajisikia vile. Katika Biblia muko hadisi za marafiki wa Yehova wenye walijisikia pia kuwa peke yao na wakati fulani waliogopa. Mumoja wao ni Eliya. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya Eliya.

Malkia Yezebeli anafoka kwa kasirani

Yezebeli anataka kumuua Eliya

Eliya aliishi katika Israeli zamani sana mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Ahabu mufalme wa Israeli hakuwa anamuabudu Yehova, Mungu wa kweli. Ahabu na Yezebeli, bibi yake, walikuwa wanaabudu Baali, mungu wa uongo. Kwa hiyo, watu wengi katika Israeli walianza pia kumuabudu Baali. Malkia Yezebeli alikuwa mwanamuke mubaya sana. Alitaka kuua waabudu wote wa Yehova. Alitaka kumuua pia Eliya! Unajua Eliya alifanya nini?—

Eliya alikimbia! Alienda mbali mu jangwa na kujificha mu tundu kubwa lenye lilikuwa ndani ya jiwe. Unawaza Eliya alijificha juu ya nini?— Ni juu aliogopa. Lakini Eliya hakupashwa kuogopa. Juu ya nini? Ni juu Eliya alijua kama Yehova anaweza kumusaidia. Mbele ya pale, Eliya alikuwa amekwisha kuona nguvu za Yehova. Siku moja, Eliya alisali, na Yehova akashusha moto kutoka mbinguni ili kujibia sala yake. Kwa hiyo, Yehova angeweza pia kumusaidia wakati Yezebeli alimuogopesha!

Yehova anajibia sala ya Eliya kwa kutuma moto kutoka mbinguni; Eliya iko mu tundu kubwa ndani ya jiwe; Eliya anafurahi kisha kusikia maneno ya Yehova yenye kutia moyo

Yehova alimusaidia Eliya namna gani?

Wakati Eliya alikuwa mu tundu kubwa ndani ya jiwe, Yehova alimuuliza hivi: ‘Uko unafanya nini hapa?’ Eliya akamujibu hivi: ‘Ni miye peke yangu nimebaki kukuabudu. Niko peke yangu, na ninaogopa kama wataniua.’ Eliya aliwaza wamekwisha kuua waabudu wote wa Yehova. Lakini Yehova alimuambia Eliya hivi: ‘Hapana Eliya, unajidanganya. Kungali watu 7 000 wenye wanaendelea kuniabudu. Usiogope. Ningali na kazi yenye unapashwa kufanya!’ Unawaza Eliya alifurahi kusikia maneno ya Yehova?—

Mambo yenye ilimupata Eliya yanakufundisha nini?— Haupashwe hata kidogo kujisikia kuwa peke yako na kuogopa. Usisahau kama uko na marafiki wenye kukupenda na wenye kumupenda Yehova. Tena, Yehova ana nguvu mingi sana, na kila siku hatakosa kukusaidia! Unafurahi sasa kujua kama hauko peke yako hata kidogo?—

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 1 Wafalme 19:3-18

  • Zaburi 145:18

  • 1 Petro 5:9

MAULIZO:

  • Katika siku za Eliya, watu wengi katika Israeli walikuwa wanamuabudu Yehova? Walikuwa wanamuabudu nani?

  • Ni juu ya nini Eliya alikimbia na kujificha mu tundu kubwa ndani ya jiwe?

  • Yehova alimuambia Eliya nini?

  • Mambo yenye ilimupata Eliya yanakufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine