Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 47 uku. 114-uku. 115 fu. 3
  • Yehova Alitia Eliya Moyo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Alitia Eliya Moyo
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Wake Alimufariji
    Tuige Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Unajisikia Kuwa Peke Yako na Mwenye Kuogopa?
    Uwafundishe Watoto Wako
  • Je, Kuna Wakati Unapojihisi Mpweke na Mwenye Woga?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 47 uku. 114-uku. 115 fu. 3
Eliya anasimama inje ya pango ku Mulima Horebu na anasikiliza malaika wa Mungu

47

Yehova Alitia Eliya Moyo

Wakati Yezebeli alisikia jambo lenye lilipata manabii wa Baali, alikasirika sana. Akatuma mutu aambie Eliya hivi: ‘Kesho, na wewe utakufa sawa vile wale manabii wa Baali.’ Eliya akaogopa sana na akakimbilia mu jangwa. Akasali: ‘Yehova, siwezi kuvumilia tena. Acha tu nikufe.’ Eliya akalala usingizi chini ya muti juu alikuwa amechoka.

Malaika akamuamusha na kumuambia hivi kwa upole: ‘Amuka ukule.’ Eliya akaona mukate ya muviringo yenye ilikuwa juu ya majiwe ya moto na mutungi wa maji. Akakula na kunywa kisha akalala tena. Malaika akamuamusha tena na kusema: ‘Kula njo utapata nguvu ya kufanya safari ya murefu.’ Kwa hiyo, Eliya akakula tena. Kisha akatembea siku 40 muchana na usiku, mupaka wakati alifika ku Mulima Horebu. Kule, Eliya akaenda kulala ndani ya pango. Lakini Yehova akazungumuza naye. Akamuambia: ‘Eliya, uko unafanya nini hapa?’ Eliya akamujibia: ‘Waisraeli wamevunja ahadi yenye walifanya kwako. Wamebomoa mazabahu yako na kuua manabii wako. Sasa, na mimi wanatafuta kuniua.’

Yehova akamuambia: ‘Toka mu pango na uangalie.’ Kwanza, upepo mukubwa ukapita kwenye lile pango. Kisha, kukakuwa tetemeko na kisha kukakuwa moto. Ku mwisho, Eliya akasikia sauti ya chini na ya upole. Akakamata koti yake na akajifunika uso. Kisha akasimama inje ya lile pango. Kisha Yehova akamuuliza juu ya nini alikimbia. Eliya akasema: ‘Nimebakia mimi peke yangu.’ Lakini Yehova akamuambia: ‘Hauko wewe peke yako. Kuko watu wengine 7000 mu Israeli wenye wangali wananiabudu. Uende ufanye Elisha akuwe nabii pa nafasi yako.’ Mara moja, Eliya akaenda na kufanya vile Yehova alimuambia. Unawaza Yehova atakusaidia na wewe wakati unafanya jambo lenye anataka ufanye? Ndiyo, atakusaidia. Tuone jambo lingine lenye lillifanyika wakati mvua haikukuwa inanyesha.

“Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu.”—Wafilipi 4:6

Maulizo: Juu ya nini Eliya alikimbia? Yehova aliambia Eliya nini?

1 Wafalme 19:1-18; Waroma 11:2-4

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine