Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 10 uku. 22-23
  • Yesu Alikuwa Anatii Kila Wakati

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Alikuwa Anatii Kila Wakati
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alifikiri na Kuamua Katika Moyo Wake
    Tuige Imani Yao
  • Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Maria Iko na Mimba Lakini Hajaolewa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Alikuwa Baba Muzuri wa Familia, na Mwanaume Mwaminifu
    Tuige Imani Yao
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 10 uku. 22-23
Yosefu na Maria wanamupata kijana Yesu mu hekalu

SOMO LA 10

Yesu Alikuwa Anatii Kila Wakati

Ni nguvu kwako kuwatii wazazi kila wakati?— Ni kweli, wakati fulani ni nguvu kuwatii wazazi. Unajua kama Yesu alikuwa anatii Yehova na pia wazazi wake?— Mufano wake unaweza kukusaidia uwatii wazazi wako hata kama wakati fulani unaona ni nguvu kufanya mambo yenye wanakuomba ufanye. Ni muzuri tujifunze sasa namna Yesu alikuwa anatii.

Yesu aliishi mbinguni pamoja na Yehova, Baba yake, mbele ya kuya duniani. Lakini pia hapa duniani Yesu alikuwa na wazazi. Wanaitwa Yosefu na Maria. Unajua ni juu ya nini tunasema kama Yosefu na Maria walikuwa wazazi wa Yesu?—

Yehova alitosha uzima wa Yesu kule mbinguni na akautia katika tumbo la Maria ili Yesu azaliwe na kuishi duniani. Ilikuwa tendo la kushangaza ao muujiza! Kwa kawaida mutoto anafanya miezi kenda katika tumbo la mama yake mbele ya kuzaliwa. Yesu pia alifanya miezi kenda katika tumbo la Maria, kisha akazaliwa. Ndio maana tunaweza kusema kama Maria na Yosefu, bwana yake, walikuwa wazazi wa Yesu hapa duniani.

Wakati Yesu alikuwa mutoto wa miaka 12 tu, kulitokea jambo fulani lenye lilionyesha kama alimupenda sana Yehova, Baba yake. Jambo hilo lilitokea wakati Yesu pamoja na wazazi wake na wadogo yake walifanya safari murefu ya kuenda kule Yerusalemu. Walienda kule ili kufurahia sikukuu ya Pasaka. Wakati wazazi wake walikuwa wanarudia nyumbani, hawakumuona Yesu kati ya watoto wengine. Unajua Yesu alikuwa wapi?—

Ni juu ya nini Yesu iko mu hekalu?

Yosefu na Maria walirudia mbio kule Yerusalemu ili kumutafuta Yesu kila fasi. Lakini, hawakumupata. Kwa hiyo, walihangaika sana akili. Kisha siku tatu, walimukuta mu hekalu! Unajua ni juu ya nini Yesu alikuwa mu hekalu?— Alikuwa mu hekalu juu ni kule angeweza kujifunza habari za Yehova, Baba yake. Yesu alimupenda Yehova na alipenda kujifunza namna ya kumufurahisha Yehova. Hata wakati alikomaa na kuwa mutu muzima, Yesu alimutii Yehova kila wakati. Yesu alitii hata wakati ilikuwa nguvu kwake kufanya vile, na hata kama iliomba ateseke. Unawaza kama Yesu aliwatii pia wazazi wake, Yosefu na Maria?— Ni vile Biblia inasema.

Mufano wa Yesu unakufundisha nini?— Weye pia unapashwa kuwatii wazazi wako, hata kama wakati fulani unaona ni nguvu kufanya mambo yenye wanakuomba ufanye. Utafanya vile?—

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Luka 1:30-35; 2:45-52

  • Waefeso 6:1

  • Waebrania 5:8

MAULIZO:

  • Ni juu ya nini tunasema kama Yosefu na Maria ndio walikuwa wazazi wa Yesu hapa duniani?

  • Ni juu ya nini Yosefu na Maria walirudia kumutafuta Yesu kule Yerusalemu, na walimukuta wapi?

  • Mufano wa Yesu unakufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine