Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 72 uku. 170-uku. 171 fu. 2
  • Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alikuwa Baba Muzuri wa Familia, na Mwanaume Mwaminifu
    Tuige Imani Yao
  • Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na Akavumilia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Anakomalia Katika Nazareti
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 72 uku. 170-uku. 171 fu. 2
Yesu iko na miaka 12, amekaa katikati ya walimu mu hekalu

72

Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Yosefu na Maria walikuwa wanaishi pamoja na Yesu, na watoto wao wengine wanamuke na wanaume. Ili familia yake ipate namna ya kuishi, Yosefu alikuwa anafanya kazi ya useremala (kazi ya mbao). Na alikuwa anafundisha watu wa familia yake juu ya Yehova na juu ya Sheria ya Yehova. Walizoea kuenda pamoja ku sinagogi juu ya kumuabudu Mungu. Na kila mwaka, walikuwa wanafanya safari ya murefu ya kuenda Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka.

Wakati Yesu alikuwa na miaka 12, familia yao ilienda Yerusalemu, kama vile walizoea kufanya. Yerusalemu ilikuwa imejaa watu wenye walikuja kwa ajili ya Pasaka. Kisha Pasaka, Yosefu na Maria walianza safari ya kurudia ku nyumba. Waliwaza kama Yesu iko na watu wengine wenye walikuwa wanasafiri pamoja nao. Lakini, wakati walimutafuta kati ya watu wa jamaa yao, hawakumupata.

Kwa hiyo, walirudia Yerusalemu na kutafuta Yesu kwa siku tatu. Ku mwisho, walienda ku hekalu. Na walimukuta kule. Alikuwa amekaa katikati ya walimu, alikuwa anawasikiliza sana, na kuwauliza maulizo. Wale walimu walifurahia sana namna Yesu alikuwa anazungumuza na walianza kumuuliza maulizo. Na majibu yake iliwashangaza. Ilionyesha kama alikuwa anaelewa muzuri Sheria ya Yehova.

Yosefu na Maria walikuwa na wasiwasi sana. Wakati Maria aliona Yesu, alisema hivi: ‘Mutoto wangu, tulikutafuta fasi yote! Ulikuwa wapi?’ Yesu akajibu: ‘Hamukujua kama ninapaswa kuwa mu nyumba ya Baba yangu?’

Kisha Yesu akarudia Nazareti pamoja na wazazi wake. Yosefu alifundisha Yesu kazi ya useremala. Unawaza Yesu alikuwa mutu wa namna gani wakati alikuwa kijana? Wakati aliendelea kukomaa, Yesu aliendelea kuwa na hekima. Mungu na watu waliendelea kumufurahia zaidi na zaidi.

Yosefu na Maria wako ku meza na Yesu na ndugu na dada zake

“Ee Mungu wangu, ninafurahia kufanya mapenzi yako, na sheria yako iko ndani yangu kabisa.”​—Zaburi 40:8

Maulizo: Yosefu na Maria walikuta Yesu wapi? Juu ya nini alikuwa mule mu hekalu?

Matayo 13:55, 56; Marko 6:3; Luka 2:40-52; 4:16; Kumbukumbu la Torati 16:15, 16

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine