Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 10 uku. 28-uku. 29 fu. 7
  • Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yesu Alikuwa Anatii Kila Wakati
    Uwafundishe Watoto Wako
  • Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na Akavumilia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Alikuwa Baba Muzuri wa Familia, na Mwanaume Mwaminifu
    Tuige Imani Yao
Ona Habari Zaidi
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 10 uku. 28-uku. 29 fu. 7
Yesu mwenye kuwa na miaka kumi na mbili anauliza walimu Wayahudi maulizo kwenye hekalu

SURA YA 10

Yesu Na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu

LUKA 2:40-52

  • YESU MWENYE KUWA NA MIAKA KUMI NA MBILI ANAULIZA WALIMU MAULIZO

  • YESU ANAMUITA YEHOVA “BABA YANGU”

Ni wakati wa kipindi cha kuchipuka kwa majani. Kwa hiyo, wakati umefika ili familia ya Yosefu, pamoja na marafiki na watu wa jamaa wafanye safari yao ya kila mwaka ya kuenda Yerusalemu. Wanaenda huko kwa ajili ya sherehe ya Pasaka, kama vile Sheria inaomba. (Kumbukumbu la Torati 16:16) Kutoka Nazareti mupaka Yerusalemu ni safari ya kilometre karibu 120. Ni wakati wenye mambo mengi na wenye kufurahisha kwa watu wote. Yesu, mwenye iko sasa na miaka 12, anangojea kwa hamu sana sherehe hiyo na nafasi ya kuwa tena kwenye hekalu.

Yesu na familia yake, hawaone Pasaka kuwa tu tukio la siku moja. Kisha siku ya Pasaka, ni mwanzo wa Sherehe ya Mikate Yenye Haina Chachu yenye inachukua siku saba. (Marko 14:1) Tukio hilo linaonwa kuwa sehemu ya kipindi cha Pasaka. Safari ya kutoka nyumbani kuenda Nazareti, kubakia katika Yerusalemu, na kurudia kwao, inachukua karibu majuma mbili. Lakini mwaka huu, kwa sababu ya jambo fulani lenye linamuhusu Yesu, safari hiyo inachukua zaidi ya majuma mbili. Inakuwa hivyo kwa sababu ya tatizo fulani lenye linatokea wakati wako wanarudia kutoka Yerusalemu.

SAFARI ZENYE KUFURAHISHA

Yesu na familia yake wanafanya safari ya kuenda Yerusalemu

Safari za kuenda Yerusalemu kwa ajili ya sherehe tatu za kila mwaka zilikuwa zenye kufurahisha kwa wote. (Kumbukumbu la Torati 16:15) Katika safari hizo, Yesu angeona sehemu mbalimbali za inchi, kujifunza jeografia ya inchi hiyo, na kukutana na waabudu wenzake kutoka maeneo mengine. Zilikuwa safari za muzuri sana!

Wakati wako katika safari, Yosefu na Maria wanawaza kuwa Yesu iko katika kikundi cha marafiki na watu wa familia wenye kusafiri kuenda upande wa kaskazini. Lakini, wakati wanasimamisha safari kwa sababu ya usiku, hawamuone. Kwa hiyo, wanaenda kumutafuta kati ya marafiki, lakini haonekane. Mutoto wao haonekane nafasi hata moja! Kwa hiyo, Yosefu na Maria wanarudia Yerusalemu ili kumutafuta.

Wanamutafuta siku nzima, lakini hawamupate. Wanamutafuta tena siku ya pili, hawamupate. Mwishowe, katika siku ya tatu, wanapata mutoto wao katika hekalu lenye vyumba vingi. Wanaona Yesu amekaa katikati ya walimu fulani Wayahudi. Iko anawasikiliza, anawauliza maulizo, na kuwashangaza na ujuzi wake.

Yosefu na Maria wanamupata Yesu

Maria anamuuliza hivi: “Mutoto wangu, sababu gani umetutendea hivi? Mimi na baba yako tumekutafuta tukiwa na wasiwasi sana.”—Luka 2:48.

Yesu anashangaa kusikia kama hawakujua nafasi kwenye angekuwa. Anauliza hivi: “Sababu gani mulikuwa munanitafuta? Je, hamukujua kama ninapaswa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”—Luka 2:49.

Sasa wako tena pamoja, Yesu anarudia nyumbani pamoja na Yosefu na Maria na anaendelea kujitiisha kwao. Anaendelea kuwa na hekima zaidi na kukomaa kimwili. Hata kama angali kijana, anakubaliwa na Mungu na wanadamu. Ndiyo, tangu utoto wake na kuendelea, Yesu anaonyesha mufano muzuri, haiko tu katika kupendezwa na mambo ya kiroho, lakini pia kuheshimia wazazi wake.

  • Ni safari gani Yesu na familia yake wanafanya kwa ukawaida katika kipindi cha kuchipuka kwa majani, na sababu gani?

  • Wakati Yesu iko na miaka 12, Yosefu na Maria wanatambua nini wakati wanarudia kutoka Yerusalemu, na hilo linasaidia kuvumbua jambo gani?

  • Ni mufano gani muzuri Yesu anaachia vijana leo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine