Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 13 uku. 28-29
  • Timoteo Alipenda Kuwasaidia Watu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Timoteo Alipenda Kuwasaidia Watu
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Paulo, Sila, na Timoteo
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • ‘Mutoto Wangu Mupendwa na Muaminifu Katika Bwana’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Utimize Mugao Wako kwa Moyo Wako Wote!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Wanaume Wenye Kuwa na Madaraka—Muige Mufano wa Timotheo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 13 uku. 28-29
Mama ya kijana Timoteo, Enise, na tate yake, Loisi, wako wanamufundisha kijana Timoteo

SOMO LA 13

Timoteo Alipenda Kuwasaidia Watu

Timoteo alikuwa kijana mwenye furaha juu alipenda kuwasaidia watu. Alitembelea miji mingi ili kuwasaidia watu wengine. Juu aliwasaidia watu wengine, alikuwa na maisha yenye furaha sana. Utapenda kusikia habari ya kijana Timoteo?—

Mama ya Timoteo na tate yake wanamufundisha habari za Yehova

Timoteo alikomalia katika muji wa Listra. Tate yake (ao kambo yake) Loisi na mama yake Enise walianza kumufundisha habari za Yehova wakati alikuwa angali mutoto mudogo sana. Wakati Timoteo alikuwa anakomaa, alipenda kuwasaidia wengine wajifunze habari za Yehova.

Wakati Timoteo alikuwa angali kijana tu, mutume Paulo alimuomba waende naye kuhubiria watu katika miji mingine. Timoteo aliitika. Alikuwa tayari kuenda kuwasaidia watu wengine.

Timoteo na mutume Paulo walienda mupaka muji wa Makedonia wenye kuitwa Tesalonika. Ili wafike kule, iliwaomba wafanye safari murefu kwa miguu na kisha wakamate mashua. Wakati walifika Makedonia walisaidia watu wengi kujifunza habari za Yehova. Lakini watu fulani walisirika na walitaka kuwafanya mubaya. Kwa hiyo, iliomba Paulo na Timoteo watoke katika muji ule na kuenda kuhubiri katika miji mingine.

Timoteo anasafiri pamoja na mutume Paulo kwenye mashua

Maisha yenye kufurahisha ya Timoteo

Kisha miezi fulani, Paulo alimuomba Timoteo arudie Tesalonika ili aone kama ndugu wako katika hali gani. Iliomba Timoteo asikuwe na woga ili kurudia kule; juu kurudia katika muji ule ilikuwa ni kutia maisha mu hatari! Lakini, Timoteo aliitika kuenda juu alikuwa anawahangaikia ndugu wenye walikuwa Tesalonika. Wakati alirudia, alimuletea mutume Paulo habari njema. Alimuambia mutume Paulo kama ndugu wa kule Tesalonika wako katika hali muzuri kabisa!

Timoteo na mutume Paulo walitumika pamoja miaka mingi. Wakati fulani mutume Paulo aliandika kama Timoteo ndiye alistahili sana kutumwa ili kusaidia makutaniko. Alisema vile juu Timoteo alimupenda Yehova na aliwapenda watu.

Weye pia unawapenda watu na unapenda kuwasaidia wajifunze habari za Yehova?— Kama ni vile, unaweza kuwa na maisha yenye kufurahisha sana kama vile Timoteo!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 2 Timotheo 1:5; 3:15

  • Matendo 16:1-5; 17:1-10

  • 1 Wathesalonike 3:2-7

  • Wafilipi 2:19-22

MAULIZO:

  • Timoteo alikomalia katika muji gani?

  • Timoteo aliitika kuenda pamoja na mutume Paulo? Juu ya nini?

  • Ni juu ya nini Timoteo alirudia Tesalonika?

  • Unaweza kufanya nini ili ukuwe na maisha yenye kufurahisha sana kama vile Timoteo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine