Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 100 uku. 232-uku. 233 fu. 2
  • Paulo, Sila, na Timoteo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Paulo, Sila, na Timoteo
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Timoteo Alipenda Kuwasaidia Watu
    Uwafundishe Watoto Wako
  • ‘Mutoto Wangu Mupendwa na Muaminifu Katika Bwana’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • ‘Kutia Makutaniko Nguvu
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Akafikiri Nao kwa Kutumia Maandiko”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 100 uku. 232-uku. 233 fu. 2
Paulo, Sila, na Timoteo

100

Paulo na Timoteo

Eunike, Loisi, na mutoto Timoteo

Timoteo alikuwa ndugu kijana wa kutaniko la Listra. Baba yake alikuwa Mugiriki, na mama yake alikuwa Muyahudi. Mama yake Eunike na tate (nkambo) yake Loisi walimufundisha Timoteo juu ya Yehova tangu wakati alikuwa mutoto.

Wakati Paulo alitembelea Listra mu safari yake ya pili ya umisionere, alitambua kama Timoteo alikuwa anapenda sana ndugu na dada na kama alikuwa tayari kuwasaidia. Paulo alimuomba Timoteo amusindikize katika safari yake. Paulo alimuzoeza Timoteo ili akuwe muhubiri muzuri na mwalimu muzuri wa habari njema.

Roho takatifu iliongoza Paulo na Timoteo kila fasi kwenye walienda. Usiku moja, katika maono, mwanaume fulani aliambia Paulo aende Makedonia awasaidie. Kwa hiyo, Paulo, Timoteo, Sila na Luka walienda kule ili wahubiri na waanzishe makutaniko.

Katika muji wa Tesalonike wenye ulikuwa Makedonia, wanaume na wanamuke wengi wakakuwa Wakristo. Lakini Wayahudi fulani wakasikilia Paulo na marafiki wake wivu. Wakakusanya watu wenye kufanya fujo na wakakokota ndugu fulani mupaka kwa watawala wa muji na kusema: ‘Hawa watu ni maadui wa serikali ya Roma!’ Uzima wa Paulo na Timoteo ulikuwa mu hatari, kwa hiyo wakakimbilia Beroya usiku.

Watu wa Beroya walikuwa na hamu ya kujifunza habari njema. Wayahudi na Wagiriki mingi wakakuwa waamini. Lakini wakati Wayahudi fulani walitoka Tesalonike na kuchochea watu wafanye fujo, Paulo alienda Atene. Timoteo na Sila walibakia Beroya ili kuwatia ndugu moyo. Kisha wakati fulani, Paulo aliambia Timoteo aende kusaidia ndugu wa Tesalonike kwa sababu walikuwa wanapambana na mateso makali. Kisha, Paulo alimutuma Timoteo aende kutembelea makutaniko ingine ya mingi ili kuwatia ndugu moyo.

Mtume Paulo iko katika kifungo mu nyumba, yeye na mulinzi wake wanafungwa munyororo mumoja na wakati uleule iko anamuambia Timoteo maneno ya kuandika katika barua

Paulo alimuambia Timoteo: ‘Wote wenye wanataka kumutumikia Yehova watateswa.’ Timoteo aliteswa na alitiwa mu gereza juu ya imani yake. Lakini alifurahi sababu alipata nafasi ya kuonyesha kama iko mushikamanifu kwa Yehova.

Paulo aliambia Wafilipi: ‘Ninamutuma Timoteo kwenu. Atawafundisha namna ya kutembea katika kweli. Na atawazoeza mu kazi ya kuhubiri.’ Paulo alijua kama Timoteo alikuwa mwenye kutegemeka. Walikuwa marafiki na walimutumikia Mungu pamoja kwa miaka mingi.

“Sina mutu mwingine mwenye kuwa na muelekeo kama wake mwenye atajali kabisa mahangaiko yenu. Kwa maana wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe, hapana faida za Yesu Kristo.”​—Wafilipi 2:20, 21

Maulizo: Timoteo alikuwa nani? Juu ya nini Paulo na Timoteo walikuwa marafiki wa sana?

Matendo 16:1-12; 17:1-15; Wafilipi 2:19-22; 2 Timoteo 1:1-5; 3:12, 14, 15; Waebrania 13:23

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine