Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 2 uku. 6-8
  • Uwe Mwaminifu- mushikamanifu kwa Mwenzako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uwe Mwaminifu- mushikamanifu kwa Mwenzako
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 UHANGAIKIE NDOA YENU KWANZA
  • 2 ULINDE MOYO WAKO
  • Mumutegemee Mungu ili Ndoa Yenu Iwe na Furaha
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Mtendee Mwenzi Wako wa Ndoa kwa Heshima
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
Ona Habari Zaidi
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 2 uku. 6-8
Bwana anakamatisha bibi yake mwanvuli ili waingie katika motokari

SOMO LA 2

Uwe Mwaminifu- mushikamanifu kwa Mwenzako

‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’​—Marko 10:9

Yehova anataka ‘tupende ushikamanifu.’ (Mika 6:8) Hilo ni jambo la maana zaidi sana katika ndoa yako, kwa sababu ikiwa bibi ao bwana yako haiko mushikamanifu ni vigumu kumutumainia. Na ni lazima kumutumainia mwenzako ili uendelee kumupenda.

Leo, ushikamanifu unakosekana katika ndoa nyingi. Ili muendelee kuwa washikamanifu katika ndoa yenu, ni lazima muazimie kufanya mambo mawili.

1 UHANGAIKIE NDOA YENU KWANZA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Uhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Wafilipi 1:10) Ndoa yenu ni moja kati ya mambo yaliyo ya maana sana katika maisha yako. Ni lazima uihangaikie kwanza.

Yehova anataka umuhangaikie sana bibi ao bwana yako na “kufurahia maisha” pamoja naye. (Mhubiri 9:9) Anaonyesha wazi kwamba haupaswi kumuzarau bibi ao bwana yako, lakini, kila mutu anapaswa kutafuta namna ya kumufurahisha mwenzake. (1 Wakorintho 10:24) Umufanye mwenzako ajisikie kuwa wa maana na mwenye kupendwa.

Bwana anamuletea bibi yake kinywaji cha moto; bwana anaporudi nyumbani anamukuta bibi yake akipika chakula

MAMBO YA KUFANYA:

  • Mupitishe wakati pamoja kwa ukawaida, na umupatie mwenzako uangalifu wote

  • Uwe unafikiri kwa njia ya “sisi” kuliko “mimi”

Bibi na bwana wanafurahia maisha pamoja kwenye walitembelea

2 ULINDE MOYO WAKO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.’ (Mathayo 5:28) Ikiwa mutu anaendelea kuwaza juu ya mambo ya uasherati, kwa kadiri fulani, anakosa uaminifu kwa bibi ao bwana yake.

Yehova anasema kwamba ni lazima ‘ulinde moyo wako.’ (Methali 4:23; Yeremia 17:9) Ili kulinda moyo wako, ni lazima uzuie macho yako. (Mathayo 5:29, 30) Fuata mufano wa Ayubu, ambaye alifanya agano na macho yake ili asimutazame hata kidogo mwanamuke kwa kumutamani. (Ayubu 31:1) Epuka kabisa kutazama ponografia ao picha za ngono. Na uepuke kwa njia yoyote kufanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwingine asiyekuwa bibi ao bwana yako.

Bwana ana picha yake na bibi yake kwenye meza katika biro yake

MAMBO YA KUFANYA:

  • Acha wengine waone waziwazi kwamba unashikamana kabisa na bibi ao bwana yako

  • Fikiria mawazo ya moyoni ya mwenzako na ukate urafiki wowote ambao unaweza kumuchukiza bibi ao bwana yako

FANYA SEHEMU YAKO

Jua uzaifu wako. (Zaburi 15:2) Usisikie haya kuomba musaada. (Methali 1:5) Ikiwa unazoea kuwaza mambo ya uasherati, endelea kupigana ili kuyaondoa katika akili. Usivunjike moyo. (Methali 24:16) Yehova atakubariki unapojikaza kubaki mushikamanifu kwa bibi ao bwana yako.

JIULIZE . . .

  • Ninaweza kufanya nini ili nipitishe wakati mwingi zaidi na bibi ao bwana yangu?

  • Je, bibi ao bwana yangu ndiye rafiki yangu wa karibu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine