Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 5 uku. 15-17
  • Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 UWE NA MAONI MAZURI JUU YA WATU WA JAMAA
  • 2 USIKUBALI KILA JAMBO BILA SABABU
  • Uwe Mwaminifu- mushikamanifu kwa Mwenzako
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Mumutegemee Mungu ili Ndoa Yenu Iwe na Furaha
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Mtendee Mwenzi Wako wa Ndoa kwa Heshima
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 5 uku. 15-17
Ma-mukwe hafurahie namna ya kupika ya bibi ya mutoto yake

SOMO LA 5

Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa

‘Mujivike fazili . . . unyenyekevu, upole, na ustahimilivu.’​—Wakolosai 3:12

Ndoa inaanzisha familia mupya. Hata ikiwa utaendelea kuwapenda na kuwaheshimia wazazi wako, sasa mutu wa maana sana kwako katika dunia hii ni bibi ao bwana yako. Inaweza kuwa vigumu kwa watu fulani katika jamaa yako kuelewa jambo hilo. Lakini kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kuwa na usawaziko ili kuishi kwa amani na watu wa jamaa yako unapojikaza kufanya familia yako mupya iwe muzuri.

1 UWE NA MAONI MAZURI JUU YA WATU WA JAMAA

Bibi na bwana wanapitisha wakati muzuri pamoja na wazazi wao

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Muheshimie baba yako na mama yako.’ (Waefeso 6:2) Hata uwe na miaka ngapi, ni lazima uendelee kuheshimia wazazi wako. Usisahau kama bibi ao bwana yako pia anapaswa kuhangaikia wazazi wake kwa kadiri fulani. “Upendo hauna wivu,” kwa hiyo, usione vibaya wakati bibi ao bwana yako anatendea wazazi wake mambo fulani.​—1 Wakorintho 13:4; Wagalatia 5:26.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Epuka masemi kama vile “Watu wa jamaa yako hawaniheshimie” ao “Mama yako hanipendi”

  • Jikaze kuona mambo kama vile bibi ao bwana yako anayaona

2 USIKUBALI KILA JAMBO BILA SABABU

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mwanaume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na muke wake nao watakuwa mwili mumoja.’ (Mwanzo 2:24) Wakati munaoana, wazazi wenu wanaweza kufikiri kama wangali na daraka kuwaelekea, na wanaweza kutafuta kujiingiza katika mambo ya ndoa yenu hata kama si lazima.

Ni lazima ninyi wawili muamue kuhusu mipaka ambayo hawapaswe kuvuka na kisha muwajulishe mipaka hiyo kwa busara. Munaweza kuwaambia waziwazi na moja kwa moja, lakini kwa upole. (Met 15:1) Sifa kama vile unyenyekevu, upole, na uvumilivu zitawasaidia kuwa na uhusiano muzuri pamoja na watu wa jamaa zenu na kuendelea ‘kuvumiliana katika upendo.’​—Waefeso 4:2.

Bibi na bwana wanazungumuza jambo fulani; bibi na bwana wanatolea wazazi wao zawadi

MAMBO YA KUFANYA:

  • Ikiwa unasumbuliwa na namna watu wa jamaa wanajiingiza katika mambo ya ndoa yenu, zungumuzia jambo hilo na bibi ao bwana yako wakati hali iko muzuri

  • Mukubaliane juu ya namna mutashugulikia mambo hayo

MUJIKAZE KUWAELEWA WAZAZI WENU

Ni jambo la lazima kuelewa mawazo ya wazazi wenu na namna wanajisikia. Wakati wanajiingiza katika mambo yenu, kusudi lao si kuharibu uhusiano wenu. Wanawahangaikia kabisa. Wazazi wenu wanaweza kufikiri kwamba hamujakuwa na uwezo wa kujitegemea. Wanaweza hata kufikiri kama mumewatupa. Lakini ikiwa munafuata kanuni za Biblia na kuzungumuza waziwazi na wazazi wenu, mutaendelea kuwaheshimia bila kuhatarisha ndoa yenu.

JIULIZE . . .

  • Sababu gani sipaswe kushangaa wakati wazazi wa bibi ao bwana yangu wanajiingiza katika mambo ya ndoa yetu?

  • Namna gani ninaweza kumushugulikia kwanza bibi ao bwana yangu, na kuendelea kuheshimia wazazi wangu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine