Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 1 uku. 10-uku. 11 fu. 8
  • Ujumbe Mbili Kutoka kwa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ujumbe Mbili Kutoka kwa Mungu
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Elizabeti Anakuwa na Mutoto
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Mutu Fulani wa Kutayarisha Njia Anazaliwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anapewa Heshima Mbele ya Kuzaliwa Kwake
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Gabrieli Anatembelea Maria
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 1 uku. 10-uku. 11 fu. 8
Gabrieli anamutokea Zekaria; Elizabeti iko na mimba

SURA YA 1

Ujumbe Mbili Kutoka Kwa Mungu

LUKA 1:5-33

  • MALAIKA GABRIELI ANATABIRI KUZALIWA KWA YOHANA MUBATIZAJI

  • GABRIELI ANAMUAMBIA MARIA KAMA ATAZAA YESU

Tunaona Biblia nzima kuwa ni ujumbe wenye kutoka kwa Mungu. Baba yetu wa mbinguni ametutolea Biblia ili itufundishe. Tuchunguze basi ujumbe mbili wa pekee wenye ulitolewa kumepita miaka zaidi ya 2000. Ujumbe huo ulitolewa na malaika Gabrieli, mwenye “kusimama karibu mbele ya Mungu.” (Luka 1:19) Ni katika hali gani malaika huyo alitoa ujumbe huo wa maana?

Ilikuwa karibu na mwaka wa 3 mbele ya wakati wetu. Ni wapi kwenye Gabrieli alitoa ujumbe wa kwanza? Katika milima ya Yudea, pengine karibu na Yerusalemu, mahali penye kuhani mumoja wa Yehova mwenye kuitwa Zekaria alikuwa anaishi. Yeye na bibi yake Elizabeti wamekwisha kuzeeka na hawana watoto. Ni wakati wa kuhani Zekaria kutumika katika hekalu la Mungu katika Yerusalemu. Wakati Zekaria iko kwenye hekalu, Gabrieli anamutokea kwa kushitukia karibu na mazabahu ya uvumba.

Bila shaka, jambo hilo linamuogopesha Zekaria. Lakini malaika anamutuliza, anamuambia hivi: “Usiogope, Zekaria, kwa sababu Mungu amesikia sala yako ya kumulilia na ameikubali, na bibi yako Elizabeti atakuzalia mwana, na utamuita Yohana.” Gabrieli anamuambia tena kama Yohana “atakuwa mukubwa katika macho ya Yehova” na ‘ataweka tayari kwa ajili ya Yehova watu wenye wametayarishwa.’—Luka 1:13-17.

Zekaria anafanya ishara kwa mikono yake

Zekaria anaona kuwa jambo hilo haliwezekane. Sababu gani? Kwa sababu ya miaka yake na miaka ya Elizabeti. Kwa hiyo, Gabrieli anamuambia hivi: “Utakuwa kimya na hautaweza kusema mupaka siku mambo hayo yatatendeka, kwa sababu haukuamini maneno yangu.”—Luka 1:20.

Wakati uleule, watu wenye kuwa inje wanaanza kujiuliza sababu gani Zekaria anakawia ndani ya hekalu. Mwishowe anatoka inje, lakini hawezi kusema. Zekaria anaweza kufanya tu ishara kupitia mikono yake. Inaonekana wazi kuwa ameona jambo fulani lenye haliko la kawaida wakati alikuwa katika hekalu.

Kisha Zekaria kumaliza kazi yake kwenye hekalu, anarudia kwenye nyumba yake. Kisha muda mufupi, Elizabeti anapata mimba! Kwa muda wa miezi tano, wakati alikuwa anangojea kuzaa mutoto wake, Elizabeti anabakia nyumbani mbali na watu.

Gabrieli anamutokea Maria

Kisha Gabrieli anatokea kwa mara ya pili. Anamutokea nani? Maria, mwanamuke mumoja kijana, mwenye alikuwa hajaolewa, ambaye alikuwa anaishi Galilaya eneo la kaskazini mwa Yerusalemu, katika muji wa Nazareti. Malaika anamuambia nini? Anamuambia hivi: “Umekubaliwa na Mungu.” Gabrieli anaendelea kumuambia Maria hivi: “Angalia! utapata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, na utamupatia jina Yesu.” Gabrieli akamuambia tena: “Huyo atakuwa mukubwa na ataitwa Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, . . . na atatawala akiwa Mufalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”—Luka 1:30-33.

Ni kweli kwamba Gabrieli alifurahia sana pendeleo hilo lenye alipewa la kutoa ujumbe huo mbili. Wakati tutakuwa tunasoma habari zaidi juu ya Yohana na Yesu, tutaelewa muzuri sababu gani ujumbe huo mbili kutoka mbinguni ni wa maana sana.

  • Ni nani anatoa ujumbe mbili wa maana kutoka mbinguni?

  • Ni nani walipokea ujumbe huo mbili?

  • Sababu gani unawaza kama ni vigumu kuamini ujumbe wenye kutoka mbinguni?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine