Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 11 uku. 30-uku. 31 fu. 14
  • Yohana Mubatizaji Anatayarisha Njia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yohana Mubatizaji Anatayarisha Njia
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yesu Anakuwa Masiya
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yesu Anabatizwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yohana Anapenda Kupata Habari Juu ya Yesu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 11 uku. 30-uku. 31 fu. 14
Yohana Mubatizaji anahubiri kuhusu kutubu

SURA YA 11

Yohana Mubatizaji Anatayarisha Njia

MATAYO 3:1-12 MARKO 1:1-8 LUKA 3:1-18 YOHANA 1:6-8, 15-28

  • YOHANA ANAFANYA KAZI YA KUHUBIRI NA KUBATIZA

  • WATU WENGI WANABATIZWA, LAKINI HAIKO WOTE

Kumepita miaka 17 hivi tangu wakati Yesu alikuwa anauliza walimu maulizo katika hekalu na angali na miaka 12. Sasa tuko katika mwaka wa 29 wakati wetu. Watu wengi wanazungumuza juu ya Yohana, mutu wa jamaa ya Yesu, mwenye iko anahubiri katika inchi yote katika eneo la mangaribi mwa Muto Yordani.

Yohana ni mwanaume mwenye kupendeza, kimwili na katika maneno. Nguo yake inatengenezwa na manyoya ya ngamia, na anavaa mukaba wa ngozi kuzunguka kiuno chake. Chakula chake ni nzige—aina fulani ya panzi—na asali ya pori. Ujumbe wake ni gani? “Mutubu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”—Matayo 3:2.

Ujumbe wa Yohana unafurahisha sana wale wenye wamekuja kumusikiliza. Wengi wanatambua kuwa wako na lazima ya kutubu, ni kusema, kubadilisha tabia na njia zao, kuacha maisha yao ya zamani ya mubaya. Wale wenye wanakuja kumuona wanatoka “Yerusalemu na Yudea yote na inchi yote yenye kuwa karibu na Yordani.” (Matayo 3:5) Wengi kati ya wale wenye wanakuja kumuona Yohana wanatubu. Anawabatiza, kwa kuwazamisha katika maji ya Yordani. Sababu gani?

Wayahudi wenye wametubu wanakuja kwa Yohana ili wabatizwe

Ubatizo wake ni alama, ao onyesho la kwamba watu hao wametubu kutoka moyoni zambi yenye walifanya kwa kuvunja agano la Sheria ya Mungu. (Matendo 19:4) Lakini, haiko wote ndio wanastahili kubatizwa. Wakati viongozi wa dini, Wafarisayo na Wasadukayo, wanakuja kumuona, Yohana anawaita “wazao wa nyoka-vipiri.” Anasema hivi: “Muzae matunda yenye kuonyesha kama mumetubu. Musijidanganye kwa kusema, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu anaweza kumuinulia Abrahamu watoto kutoka katika majiwe haya. Tayari shoka limewekwa kwenye muzizi wa miti. Basi, kila muti wenye hauzae matunda ya mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.”—Matayo 3:7-10.

Kwa sababu watu wengi wanamusikiliza kwa uangalifu, iko na ujumbe wenye nguvu, na iko anabatiza watu wengi, makuhani na Walawi wanatumwa ili wamuulize hivi: “Wewe ni nani?”

Anajibu waziwazi kwa kusema, “Mimi siko Kristo.”

Wanamuuliza, “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”

Anajibu: “Haiko mimi.”

Wanawazia Nabii mukubwa mwenye Musa alisema kuwa angekuja; kwa hiyo, wanamuuliza, “Je, wewe ndiye ule Nabii?”—Kumbukumbu la Torati 18:15, 18.

Yohana anajibu, “Hapana!”

Wanaendelea kumuuliza: “Wewe ni nani? Tuambie ili tujibu wale wenye walitutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?” Yohana anajibu hivi: “Mimi ni sauti ya mutu mwenye kusema kwa sauti kubwa katika jangwa, ‘Munyooshe njia ya Yehova,’ kama vile nabii Isaya alisema.”—Yohana 1:19-23.

Wanapenda kujua; kwa hiyo wanamuuliza, “Sababu gani unabatiza kama wewe hauko Kristo ao Eliya ao ule Nabii?” Anawatolea jibu lenye kuwa na maana kwa kusema: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuko mutu mwenye amesimama katikati yenu mwenye ninyi hamujue, ule mwenye anakuja nyuma yangu.”—Yohana 1:25-27.

Kwa kweli, Yohana anajua kuwa anatayarisha njia kwa kusaidia watu wakuwe na hali nzuri ya moyoni ili kumupokea Masiya mwenye aliahidiwa, ule mwenye anapaswa kuwa Mufalme. Kuhusu mutu huyo, Yohana anasema hivi: “Ule mwenye anakuja kisha mimi iko na nguvu kunipita, na sistahili kutosha viatu vyake.” (Matayo 3:11) Bila shaka, Yohana anafikia hata kusema hivi: “Ule mwenye anakuja nyuma yangu ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.”—Yohana 1:15.

Kwa hiyo, ujumbe wa Yohana “Mutubu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia” ni wenye kufaa kabisa. (Matayo 3:2) Unasaidia kuonyesha waziwazi kuwa utumishi wa Mufalme wa Yehova mwenye iko anakuja, ni kusema, Yesu Kristo, uko karibu kuanza.

  • Yohana ni mutu wa namna gani, na iko anafanya kazi gani?

  • Sababu gani Yohana anabatiza watu?

  • Ujumbe wa Yohana ni gani, na sababu gani ni wenye kufaa?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine