SURA YA 13
“Mufanye Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”
JUU tuko watumishi wa Yehova Mungu wenye walijitoa kwake, maneno na matendo yetu yote inapaswa kumutukuza. Mutume Paulo alituonyesha kanuni yenye inapaswa kutuongoza. Aliandika hivi: “Ikuwe munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Ko. 10:31) Kwa hiyo, tunapaswa kutii kabisa kanuni za Yehova za haki; zile kanuni njo zinaonyesha sifa zake kamilifu. (Kol. 3:10) Basi, tunapaswa kumuiga Mungu kwa kuwa watakatifu.—Efe. 5:1, 2.
2 Ili kusaidia Wakristo wafikirie sana ile jambo, mutume Petro aliandika hivi: “Kama watoto watiifu, muache kufinyangwa na tamaa zenye mulikuwa nazo zamani katika hali yenu ya kukosa kujua, lakini kama ule Mutakatifu mwenye aliwaita ninyi, ninyi wenyewe pia mukuwe watakatifu katika mwenendo wenu wote, kwa maana imeandikwa: ‘Munapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mutakatifu.’” (1 Pe. 1:14-16) Sawa vile mu Israeli ya zamani, leo pia ndugu na dada mu kutaniko ya Kikristo wanaombwa wakuwe watakatifu. Maana yake, wanapaswa kubakia safi, hawapaswe kuchafuliwa hata kidogo na zambi ao kuambukizwa na roho ya ulimwengu. Wao ni watu wenye kuchaguliwa na Mungu ili wafanye utumishi mutakatifu.—Kut. 20:5.
3 Ili mutu aendelee kuwa mutakatifu anapaswa kuendelea kutii kabisa sheria na kanuni za Yehova zenye kuonyeshwa wazi katika Maandiko Matakatifu. (2 Ti. 3:16) Kujifunza Biblia kulitusaidia kumujua Yehova na njia zake, na ile ilifanya tumukaribie zaidi. Tena, tuliona ulazima wa kutafuta kwanza Ufalme wake, na kuona kama kufanya mapenzi yake njo jambo ya maana sana mu maisha yetu. (Mt. 6:33; Ro. 12:2) Kwa hiyo, ilituomba kuvala utu mupya.—Efe. 4:22-24.
KUWA SAFI KIROHO NA KUWA NA MWENENDO SAFI
4 Haiko mwepesi kila siku kutii kanuni za haki za Yehova. Shetani Ibilisi, adui yetu, iko natupiganisha ili tuache kweli. Mambo ya mubaya yenye kuwa mu hii dunia na mielekeo ya zambi yenye tuko nayo njo inafanyaka wakati fulani mambo ikuwe nguvu. Ili kutimiza ahadi yenye tulimutolea Yehova wakati tulijitoa kwake, tunapaswa kupigana vita ya kiroho, ni kusema, tunapaswa kupiganisha kabisa ile mambo. Maandiko inatuambia kama hatupaswe kushangaa ikiwa watu wanatupinga ao kama tunapata majaribu. Tunateswa kwa sababu ya haki. (2 Ti. 3:12) Wakati tunapatwa na majaribu tunaweza kuwa wenye furaha juu tunajua kama ile majaribu iko naonyesha kwamba tuko nafanya mapenzi ya Mungu.—1 Pe. 3:14-16; 4:12, 14-16.
5 Yesu alikuwa mukamilifu. Lakini alijifunza kutii kupitia mateso yenye alipata. Kila mara alipinga majaribu yenye Shetani alimuletea, na hakuna hata siku yenye alitamani kuwa na vitu vyenye kuwa mu hii ulimwengu. (Mt. 4:1-11; Yoh. 6:15) Hakuna siku aliwaza kuacha kweli ao kuvunja sheria ya Mungu. Hata kama watu walimuchukia juu alikuwa muaminifu, Yesu aliendelea kutii kanuni za Yehova za haki. Wakati kidogo mbele akufe, Yesu aliambia wanafunzi wake kwamba nao watachukiwa. Kuanzia ile wakati, wafuasi wake wamepatwa na upinzani ao mateso. Lakini, kujua kama Mwana wa Mungu alishinda ulimwengu njo kuko nafanya wasivunjike moyo.—Yoh. 15:19; 16:33; 17:16.
6 Ili tusikuwe sehemu ya hii ulimwengu, tunapaswa kutii kabisa kanuni za Yehova sawa vile Bwana wetu alifanya. Zaidi tu ya kukatala kujiingiza mu mambo ya politike na mambo ingine ya mu maisha ya watu, tunapaswa pia kukatala mwenendo wowote mubaya wenye unaenea leo. Tunatii kabisa shauri yenye kuwa mu Yakobo 1:21: “Mutoshe uchafu wote na ubaya wote, na mupokee kwa upole kupandwa kwa lile neno lenye linaweza kuwaokoa ninyi.” Wakati tunajifunza Biblia na kukusanyika, tunaweza kujionea “kupandwa kwa lile neno” mu akili na moyo wetu, na hatutatamani hata kidogo mambo yenye kuwa mu ulimwengu. Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Je, hamujue kama urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu? Kwa hiyo, mutu yeyote mwenye anataka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya mwenyewe kuwa adui ya Mungu.” (Yak. 4:4) Njo maana, Biblia inatuambia tutii kabisa kanuni za Yehova na kuepuka kuwa sehemu ya ulimwengu.
7 Neno ya Mungu inatuomba tusijiingize mu mwenendo muchafu na wa haya. Inatuambia hivi: “Uasherati na kila namna ya ukosefu wa usafi ao pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu, kama vile inafaa watu watakatifu.” (Efe. 5:3) Kwa hiyo, hatupaswe kuwaza juu ya mambo machafu, ya haya ao ya kushushia heshima, na hatupaswe hata kuizungumuzia. Kuepuka ile mambo kunaonyesha kama tunapenda kutii kabisa kanuni za Yehova kuhusu mwenendo safi.
USAFI WA KIMWILI
8 Zaidi ya kuwa safi kiroho na kuwa na mwenendo safi, ni lazima pia Wakristo wakuwe safi kimwili. Ili kuonyesha kama yeye ni Mutakatifu, Mungu aliambia Waisraeli kwamba kambi yao ilipaswa kuwa safi. Na siye tunapaswa kuwa safi ili Yehova “asione kitu chochote chenye hakifae” ndani yetu.—Kum. 23:14
9 Kulingana na Biblia, kuko uhusiano wa karibu sana kati ya utakatifu na usafi wa kimwili. Kwa mufano, mutume Paulo aliandika hivi: “Wapendwa, tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho, tukikamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.” (2 Ko. 7:1) Kwa hiyo, Wakristo wote, wanaume na wanamuke wanapaswa kujikaza kuwa safi kimwili, kwa kunawa kwa ukawaida na kufula manguo yao. Hata kama hali ya maisha ya inchi fulani iko tofauti na ya inchi ingine, kwa kawaida kila mutu anaweza kupata sabuni na maji ili kunawa na kunawisha watoto juu wakuwe safi.
10 Kwa kawaida, fasi kwenye tunaishi, watu wengi wanatujua juu tunafanyaka kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, kama nyumba yetu iko safi inje na ndani na kama inapangwa muzuri, ile inaweza kutolea majirani wetu ushahidi. Juu ya kuweza kufanya vile, inaomba kila mutu mu familia asaidie. Baba wa familia anapaswa kuhangaikia sana hali ya nyumba yake; anapaswa kujua kwamba kama nyumba inatunzwa muzuri (kutia ndani kiwanja), ile inaweza kufanya wengine wajifunze kweli. Baba mwenye kufanya vile na pia mwenye kuhangaikia familia yake kiroho, anaonyesha kama iko nasimamia nyumba yake muzuri. (1 Ti. 3:4, 12) Na wadada pia wako na kazi ya kuangalia mambo fulani, zaidi sana usafi ndani ya nyumba. (Tit. 2:4, 5) Watoto wenye kufundishwa muzuri wako pia na sehemu ya kutimiza; wanajikaza kuwa na mwili safi na wanasafisha chumba na kupanga kila kitu muzuri. Kwa kufanya vile, familia yote inaendelea kuwa mu hali ya usafi, hali yenye itakuwa mu dunia mupya yenye itatawaliwa na Ufalme wa Mungu.
11 Leo, watumishi wengi wa Yehova wanatumia vyombo kama vile motokari, moto, ao kinga ili kuenda ku mikutano. Mu maeneo fulani, motokari ni ya lazima sana kwa ajili ya kazi ya kuhubiri. Inaomba ikuwe safi na mu hali ya muzuri. Manyumba yetu na vitu sawa vile motokari, moto ao kinga vinapaswa kuonyesha kama tuko kabisa watu wa Yehova wenye kuwa safi na watakatifu. Vilevile, Biblia na sakoshe yetu ya mahubiri vinapaswa kuwa safi.
12 Namna yetu ya kuvala na kujipamba inapaswa kupatana na kanuni za Mungu. Hatuwezi kuenda kuonana na mukubwa fulani ao mutu mwenye mamlaka na tulishavala ovyo-ovyo ao kuvala manguo yenye haifae. Kwa hiyo, hauone kama tunapaswa kuvala na kujipamba muzuri zaidi wakati tuko mu mahubiri ao wakati tuko nafundisha mu kutaniko? Namna yetu ya kuvala na kujipamba inaweza kufanya watu wafurahie ao waseme mubaya juu ya ibada ya Yehova. Vilevile haiko muzuri kuvala manguo ya kukosa kiasi ao yenye kuvunjia wengine heshima. (Mik. 6:8; 1 Ko. 10:31-33; 1 Ti. 2:9, 10) Kwa hiyo, wakati tuko najitayarisha ili kuenda mu mahubiri, ku mikutano ya kutaniko ao ku mikusanyiko yetu mikubwa, tunapaswa kukumbuka mashauri yenye kuwa mu Biblia kuhusu kuwa safi kimwili na kujipamba kwa kiasi. Tunapenda kumuheshimia na kumutukuza Yehova kila siku.
Juu tuko watumishi wa Yehova Mungu wenye walijitoa kwake, maneno na matendo yetu yote inapaswa kumutukuza
13 Tunapaswa pia kukumbuka ile jambo wakati tunatembelea makao makubwa ao Beteli fulani ya Mashahidi wa Yehova. Usisahau kwamba jina Beteli, maana yake, “Nyumba ya Mungu.” Kwa hiyo, wakati tunatembelea kule, tunapaswa kuvala na kujiendesha muzuri sawa vile tunafanyaka wakati tunaenda ku mikutano yetu mu Jumba ya Ufalme.
14 Hata wakati tuko nafanya mambo fulani ya kujifurahisha, inaomba kuchunguza muzuri namna tunavala na kujipamba. Tunaweza kujiuliza hivi, ‘Hata kama siko mu mahubiri, vile nilishavala inaweza kufanya nisikie haya ya kuhubiria mutu fulani?’
KUJIFURAHISHA
15 Kupumuzika na kujifurahisha, ni mambo ya lazima ili mutu aendelee kuwa na afya ya muzuri. Siku moya Yesu aliwaambia wanafunzi wake waende fasi kwenye hakuna watu ili ‘wapumuzike kidogo.’ (Mk. 6:31) Kupumuzika na kujifurahisha na mambo ya muzuri kunaweza kumaliza muchoko na kunaweza kufanya akili ipumuzike kidogo. Kunaweza kufanya tukuwe na nguvu ya kuendelea na kazi yetu kama kawaida.
16 Juu leo kuko namna mingi ya kujifurahisha, Wakristo wanapaswa kutumia hekima ya Mungu ili kuchagua namna ya kujifurahisha yenye kufaa. Hata kama kujifurahisha kuko na faida fulani, tujue kwamba haiko njo jambo kubwa mu maisha. Biblia inasema kama mu “siku za mwisho,” watu wangekuwa “wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu.” (2 Ti. 3:1, 4) Leo, mambo mingi ya kujifurahisha haifae na inachukiza watu wenye kupenda kutii kanuni za Yehova.
17 Wakristo wa kwanza walikatala kabisa mambo ya kujifurahisha yenye haifae yenye watu wengine walikuwa wanafuatilia. Mu Roma, mulikuwa majengo ya michezo mbalimbali. Mule watu walikuwa wanajifurahisha kwa kuangalia namna watu wengine walikuwa wanateswa. Watu walikuwa pia wanaangalia mambo ya umwangaji wa damu ao kuuana, na mambo ya uasherati. Lakini Wakristo walijiepusha kabisa na mambo ya vile. Leo pia, kuko mambo mingi ya kujifurahisha yenye inachocheaka ao kulamusha hamu ao tamaa ya kufanya mambo machafu sana. Tunapaswa kuwa “waangalifu sana” mu namna yetu ya kutembea, na tunapaswa kujiepusha kabisa na mambo ya kujifurahisha yenye inaweza kuharibisha hali yetu ya kiroho ao mwenendo wetu. (Efe. 5:15, 16; Zb. 11:5) Hata kama pengine namna fulani ya kujifurahisha haiko mubaya kabisa, watu wenye tuko najifurahisha nao, hali ao fasi kwenye tuko najifurahishia inaweza kuwa ya mubaya.—1 Pe. 4:1-4.
18 Kuko namna mbalimbali za muzuri za kujifurahisha zenye Wakristo wanaweza kufurahia. Ndugu na dada wengi wanapata faida juu wako natii mashauri yenye kupatikana mu Biblia na mu vichapo vyetu kuhusu mambo ya kujifurahisha.
19 Wakati fulani, Mukristo anaweza kualika kwake familia fulani za Wakristo wenzake. Ndugu ao dada anaweza kualikwa ku karamu ya ndoa ao ku mambo ingine. (Yoh. 2:2) Ni wazi kwamba mambo yote yenye itapita ku ile karamu iko juu ya kichwa ya mwenye alialika watu. Kwa hiyo, inaomba kuwa waangalifu kama tuko wengi ku mukutano fulani kwenye tulialikwa juu ya kujifurahisha. Kujifurahishia fasi na mu hali yenye haifae kulishafanya Wakristo fulani waangukie mu mwenendo ya mubaya, sawa vile kula na kunywa kupita kiasi, na hata kufikia kufanya zambi zingine nzito. Kwa hiyo, Wakristo wenye kuwa na hekima na wenye kuona mbali wako naamua kualika watu kidogo na kujifurahisha tu kwa wakati kidogo. Na kama watu watakunywa pombe ile wakati, hawapaswe kuvuka mipaka. (Flp. 4:5) Kama Wakristo wanajikaza kabisa ili kufanya ile wakati ya kujifurahisha ikuwe yenye kujenga na ya kutiana nguvu kiroho, basi pombe na chakula havitaonekana kuwa njo mambo ya lazima sana.
20 Ni muzuri sana kuwa wakaribishaji. (1 Pe. 4:9) Lakini wakati tunaalika ndugu na dada kwetu kwa ajili ya chakula, kinywaji, kujifurahisha na kuwa na mazungumuzo pamoya, ni muzuri tusisahau pia ndugu na dada maskini ao wenye hawana uwezo. (Lu. 14:12-14) Ikiwa tunaalikwa, mwenendo wetu unapaswa kupatana na mashauri yenye kupatikana mu andiko ya Marko 12:31. Kila mara, wakati ndugu na dada wanatufanyia mambo ya muzuri, ni jambo ya lazima kuwashukuru.
21 Wakristo wanafurahia zawadi mbalimbali zenye Mungu anawatolea, na wanajua kama kila mutu anaweza “kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu.” (Muh. 3:12, 13) Wakati “tunafanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu,” ndugu wenye kualika wengine na wale wenye kualikwa, wanaweza kukumbuka kwa furaha ile wakati yenye walipitisha pamoya ili kutiana nguvu kiroho.
KU MASOMO
22 Masomo ya musingi yenye watoto wa Mashahidi wa Yehova wanasoma, inawaleteaka faida. Inawasaidiaka wajifunze kusoma na kuandika muzuri. Mambo ingine yenye inafundishwa ku masomo inaweza kusaidia vijana wenye kuwa na miradi ao mipango fulani ya kiroho ya kufanya mu maisha yao. Miaka yote yenye watapitisha ku masomo watajikaza sana ‘kumukumbuka Muumbaji wao mukubwa’ kwa kuendelea kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza.—Muh. 12:1.
23 Kama uko kijana Mukristo na ungali unasoma, ukuwe mwangalifu. Usifanye urafiki bila sababu yoyote ya lazima na vijana wenye hawamutumikie Yehova. (2 Ti. 3:1, 2) Vile Yehova alishatutolea mambo mingi ili kutulinda, weye pia unaweza kutumia ile mambo ili kujilinda usiambukizwe na tabia za mubaya zenye vijana fulani mu hii dunia wako nazo. (Zb. 23:4; 91:1, 2) Kwa hiyo, ili ujilinde tumikisha mashauri yote yenye Yehova anaendelea kutupatia leo.—Zb. 23:5.
24 Ili kuepuka kuwa sehemu ya ulimwengu, vijana wengi Mashahidi wa Yehova wanaepuka kufanya ao kujiingiza mu mambo fulani yenye wanafunzi wenzao wanafanyaka kisha masomo. Hata kama wanafunzi wenzako ao walimu hawakuelewe, jambo ya maana sana ni kumufurahisha Mungu. Kwa hiyo, itakuomba utumie zamiri yako yenye kufundishwa na Biblia na kuazimia kabisa kuepuka kujiingiza mu mambo ya kushindana yenye kuonyesha roho ya ulimwengu ao mambo ya kutukuza taifa. (Gal. 5:19, 26) Vijana, kama munaendelea kutii mashauri yenye kuwa mu Biblia yenye wazazi wenu wenye kumuogopa Mungu wanawatolea, na kama munachagua marafiki wazuri mu kutaniko, munaweza kuendelea kushika kabisa kanuni za haki za Yehova.
KAZI YA KIMWILI NA MARAFIKI
25 Biblia inasema kama kila kichwa ya familia anapaswa kupatia familia yake mambo yenye wako nayo lazima. (1 Ti. 5:8) Hata vile, kwa sababu ni muhubiri wa habari njema, anaelewa kama anapaswa kutia mambo ya Ufalme pa nafasi ya kwanza kuliko kazi ya kimwili. (Mt. 6:33; Ro. 11:13) Ili kuepuka mahangaiko na tamaa ya kupenda vitu vya kimwili, ni muzuri kuendelea kushikamana na Mungu na kutosheka kama tuko na chakula na manguo.—1 Ti. 6:6-10.
26 Kila Mukristo mwenye alijitoa kwa Mungu, na mwenye iko na kazi fulani ya kimwili, anapaswa kukumbuka kila siku kanuni zenye kuwa mu Maandiko. Wakati tunatafuta mambo yenye tuko nayo lazima mu maisha, tunapaswa kuepuka kudanganya ao kufanya mambo yenye kuvunja sheria ya Mungu ao sheria ya inchi. (Ro. 13:1, 2; 1 Ko. 6:9, 10) Tunajua kama ni hatari kuwa na marafiki wabaya. Juu tuko maaskari wa Kristo, tunaepuka kujiingiza mu mambo ya biashara yenye kuvunja kanuni za Mungu na yenye inaweza kufanya tuunge mukono mambo ya politike. Zaidi ya ile tunaepuka biashara yenye inaweza kufanya hali yetu ya kiroho ikuwe mu hatari. (Isa. 2:4; 2 Ti. 2:4) Tena, hatupende hata kidogo kuwa na uhusiano na adui wa Mungu, ni kusema “Babiloni Mukubwa.”—Ufu. 18:2, 4; 2 Ko. 6:14-17.
27 Kutii kanuni za haki za Mungu kunafanya tuepuke kuzungumuzia mambo ya biashara wakati tuko ku mikutano ya Kikristo ao kutafuta faida zetu za kipekee. Kusudi yetu ya kukutana na Wakristo wenzetu ku mikutano ao mikusanyiko ni moya tu, ni kusema kumuabudu Yehova. Wakati wa ile mikutano ao mikusanyiko, ni saa ya kula ku meza ya kiroho na kufurahia “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Ro. 1:11, 12; Ebr. 10:24, 25) Ile inapaswa kuwa wakati ya kuzungumuzia mambo ya kiroho.
TUENDELEE KUISHI KWA UMOJA
28 Kufuata kanuni za haki za Yehova kunatia ndani pia kuendeleza “umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:1-3) Kila mutumishi wa Yehova anapaswa kutafuta faida ya wengine, hapana tu kutafuta kujipendeza yeye mwenyewe. (1 Te. 5:15) Bila shaka, ile njo uko najionea mu kutaniko yenu. Hata kama tuko wa rangi gani, taifa gani, kabila gani, ikuwe tuko matajiri ao maskini, tulisoma sana ao hapana, siye wote tunaongozwa na kanuni zilezile za haki. Hata watu wenye hawako Mashahidi wako najionea ile umoja ya pekee yenye inafanya kukuwe tofauti kati ya watu wa Yehova na watu wengine.—1 Pe. 2:12.
29 Ili kukazia sana sababu yenye inapaswa kutusukuma tukuwe na umoja, mutume Paulo aliandika hivi: “Kuko mwili mumoja, na roho moja, kama vile muliitwa kwenye tumaini moja la mwito wenu; Bwana mumoja, imani moja, ubatizo moja; Mungu mumoja na Baba ya wote, mwenye kuwa juu ya wote na kupitia wote na katika wote.” (Efe. 4:4-6) Kwa hiyo, inaomba siye wote tukuwe na ujuzi uleule kuhusu mafundisho ya musingi ya Biblia na pia mafundisho mazito ya Biblia ili tuweze kutii mamlaka makubwa ya Yehova. Bila shaka, Yehova alishapatia watumishi wake luga safi, ni kusema, ile kweli. Ile inawasaidia wamutumikie bega kwa bega ao kwa umoja.—Sef. 3:9.
30 Umoja na amani yenye kuwa mu kutaniko ya Kikristo inawafanya wale wote wenye kumuabudu Yehova wakuwe na furaha. Tunaona kama Yehova iko natimiza ahadi yake yenye kusema: “Nitawaunganisha, kama kondoo katika zizi.” (Mik. 2:12) Tunapenda kuchunga ile umoja yenye amani kwa kuendelea kutii kabisa kanuni za haki za Yehova.
31 Inafurahisha sana kujua kama Yehova alituleta mu kutaniko yake yenye kuwa safi! Tunapaswa kukubali kujiima kila kitu juu tuko na pendeleo ya kuitwa kwa jina yake. Tuchunge kabisa urafiki wetu wa maana sana wenye tuko nao na Yehova. Tena, tujikaze kutii kabisa kanuni zake za haki na kuwafundisha wengine zile kanuni.—2 Ko. 3:18.