SURA YA 14
Kulinda Amani na Usafi wa Kutaniko
KAMA vile Biblia ilitabiri, kila mwaka maelfu ya watu wanamiminika kwenye nyumba ya ibada safi ya Yehova. (Mik. 4:1, 2) Tunafurahi sana kuwakaribisha mu “kutaniko la Mungu.” (Mdo. 20:28) Wanafurahia sana pendeleo ya kumutumikia Yehova pamoya na siye. Pia, wanafurahia kuwa na siye mu paradiso yetu ya kiroho, ni kusema, fasi kwenye kuko safi na kwenye kuko amani. Roho takatifu ya Mungu na mashauri yenye kuwa mu Neno yake, njo mambo yenye inatusaidia tuendelee kuwa na amani na usafi mu kutaniko.—Zb. 119:105; Zek. 4:6.
2 Wakati tunatumia kanuni za Biblia mu maisha yetu, tunaonyesha kama tunavala “utu mupya.” (Kol. 3:10) Hatuache uzaifu wa wengine ao mabishano ya kidogo-kidogo kati yetu itutenganishe. Kuona mambo vile Yehova anaiona, inatusaidia kuachana kabisa na mambo yenye inatenganisha watu mu dunia. Kwa hiyo, tunatumika pamoya tukiwa familia ya ndugu na dada mu dunia yote.—Mdo. 10:34, 35.
3 Lakini, mara kwa mara, mambo yenye inaweka mu hatari amani na umoja wetu mu kutaniko inatokeaka. Juu ya nini? Mara mingi ni juu ya kukosa kutumikisha mashauri ya Biblia mu maisha. Tungali napambana na mielekeo yetu ya kukosa kukamilika. Siye wote tuko watenda-zambi. (1 Yo. 1:10) Ndugu ao dada anaweza kufanya jambo fulani yenye inaweza kuchafua mwenendo na usafi wa kiroho wa kutaniko. Tunaweza kosea ndugu ao dada fulani kwa kutenda ao kusema bila kufikiri, ao tunaweza kukwazika juu ya jambo fulani yenye Mukristo mwenzetu alisema ao kufanya. (Ro. 3:23) Kama hali za vile zinatokea, tunaweza kufanya nini juu ya kutengeneza mambo?
4 Kwa upendo, tayari Yehova ashakafikiria ile yote. Neno yake inatupatia mashauri ya muzuri yenye tunaweza kutumia wakati magumu inatokea kati yetu. Wachungaji wenye upendo, ni kusema, wazee mu kutaniko, wanaweza kusaidia kila mumoja wetu. Kama tunatumikisha mashauri ya Biblia, tunaweza kuwa na urafiki wa muzuri pamoya na wengine na kuendelea kuwa na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova. Kama tunapewa nizamu ao tunakaripiwa juu ya kosa fulani, tukuwe hakika kama musaada ao shauri yenye tunapewa ni alama yenye kuonyesha kama Baba yetu wa mbinguni anatupenda.—Mez. 3:11, 12; Ebr. 12:6.
KUMALIZA KUKOSA KUELEWANA MU MAMBO YA KIDOGO-KIDOGO
5 Mu kutaniko, inawezekana Wakristo wabishane ao wakose kuelewana juu ya mambo ya kidogo-kidogo. Ndugu wanapaswa kutenda haraka juu ya kumaliza ile hali kwa roho ya upendo. (Efe. 4:26; Flp. 2:2-4; Kol. 3:12-14) Kama unakosa kuelewana na ndugu ao dada fulani mu kutaniko, bila shaka utaona kama juu ya kumaliza ile tatizo, ni muzuri kufuata hii shauri ya mutume Petro: “Mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.” (1 Pe. 4:8) Biblia inasema pia hivi: “Kwa maana sisi wote tunajikwaa mara nyingi.” (Yak. 3:2) Kama tunatumia kanuni yenye inajulikana kuwa Kanuni ya Muzuri Sana, ni kusema, kutendea wengine vile tunataka watutendee, inaweza kuwa mwepesi kwetu kusamehe na kusahau makosa ya kidogo-kidogo.—Mt. 6:14, 15; 7:12.
6 Kama tu unatambua kama jambo fulani yenye ulisema ao kufanya imekwaza Mukristo mwenzako, bila kukawia unapaswa kuchukua hatua ya kwanza ya kuenda kufanya amani pamoya naye. Kumbuka kama, ikiwa haufanye vile, urafiki wako pamoya na Yehova unaweza pia kuharibika. Yesu alishauria hivi wanafunzi wake: “Basi, kama unaleta zawadi yako kwenye mazabahu na pale unakumbuka kama ndugu yako iko na jambo fulani juu yako, acha zawadi yako pale mbele ya mazabahu, na uende. Fanya kwanza amani na ndugu yako, na kisha urudie na utoe zawadi yako.” (Mt. 5:23, 24) Pengine ni yeye njo hakukuelewa muzuri. Kwa hiyo, uzungumuze naye. Kama ndugu wanasikilizana muzuri mu kutaniko, ile itazuia kukosa kuelewana na itasaidia pia kumaliza magumu yenye inatokeaka kati yetu juu ya kukosa kukamilika.
KUTOA SHAURI YA MAANDIKO
7 Wakati fulani, waangalizi wanaweza kuona kama ni jambo ya lazima kushauria Mukristo fulani juu ya kumusaidia akuwe tena na mawazo ya muzuri. Lakini, mara mingi ile haikuwake mwepesi. Mutume Paulo aliandikia hivi Wakristo wa mu kutaniko ya Galatia: “Ndugu, hata kama mutu anafanya hatua fulani ya mubaya mbele ajue jambo hilo, ninyi wenye muko na sifa za kustahili kiroho mujaribu kumurekebisha upya mutu huyo kwa roho ya upole.”—Gal. 6:1.
8 Waangalizi wanapaswa kuchunga muzuri kundi. Ile inasaidia ndugu na dada waendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, na inaweza kufanya matatizo makubwa isitokee mu kutaniko. Wazee wanapaswa kujikaza kutumikia kutaniko sawa vile Yehova aliahidi kupitia nabii Isaya. Alisema hivi: “Kila mumoja atakuwa kama mahali pa kujificha kwa sababu ya upepo, mahali pa kujificha kwa sababu ya zoruba ya mvua, kama mito midogo ya maji katika inchi yenye haina maji, kama kivuli cha mwamba mukubwa katika inchi yenye kukauka.”—Isa. 32:2.
KUTIA ALAMA WALE WENYE KUTEMBEA BILA UTARATIBU
9 Mutume Paulo alionya Wakristo juu ya wamoya kati yao wenye walikuwa na uvutano mubaya mu kutaniko. Aliwaandikia hivi: “Tunawapatia ninyi maagizo . . . mujiepushe na kila ndugu mwenye anajiendesha bila utaratibu na hatembee kupatana na pokeo lenye mulipata kutoka kwetu.” Alionyesha waziwazi hatua ya kufuata kwa kusema hivi: “Kama mutu yeyote hatii neno letu kupitia barua hii, mumutie mutu huyo alama na muache kushirikiana naye, ili apate haya. Hata hivyo, musimuone mutu huyo kama adui, lakini muendelee kumuonya kama ndugu.”—2 Te. 3:6, 14, 15.
10 Pengine ndugu ao dada fulani hazoee kufanya zambi nzito yenye inaweza kumufanya atengwe na kutaniko, lakini inawezekana iko navunja kimakusudi kanuni za Mungu zenye kila Mukristo anapaswa kutii. Zile kanuni zinaweza kutia ndani, mambo kama vile kuwa muvivu kupita kiasi, kuchambua-chambua wengine, kuwa muchafu sana, ao kuwa mutu mwenye ‘anajiingizaka mu mambo yenye haimuangalie.’ (2 Te. 3:11) Pengine tena ni mutu mwenye anatumia udanganyifu juu apate kitu ya mutu mwingine ao anazoea kujifurahisha na mambo yenye kuonekana kabisa kuwa haifae. Mwenendo ya vile, ya kutembea bila utaratibu, ni jambo nzito kabisa yenye inaweza kuharibisha sifa ya muzuri ya kutaniko, na ni hatari juu inaweza kuambukiza Wakristo wengine.
11 Kama ndugu ao dada anajiendesha vile, wazee watajaribu kwanza kumutolea mashauri ya Biblia. Lakini, kama anaendelea kuzarau kanuni za Biblia hata kama alishashauriwa tena na tena, wazee wanaweza kuamua hotuba ya kuonya juu ya ile mwenendo itolewe mu kutaniko. Mbele ya kutoa ile hotuba, wazee watachunguza kwanza juu ya kuona kama ile hali ni ya nguvu sana na kama inasumbua wengine. Mu ile hotuba, musemaji atazungumuzia mashauri yenye kufaa juu ya ile mwenendo mubaya, lakini hatataya jina ya ndugu ao dada mwenye iko na ile mwenendo. Kwa hiyo, wale wenye wanajua ndugu ao dada mwenye iko na ile mwenendo, wataepuka kufanya urafiki naye, hata kama wataendelea kushirikiana naye mu mambo ya kiroho na ‘kumuonya kama ndugu.’
12 Namna ndugu na dada waaminifu mu kutaniko watajiendesha naye, inaweza kumufanya asikie haya juu ya mwenendo yake na inaweza kumuchochea afanye mabadiliko. Wakati inaonekana wazi kama ameacha mwenendo yake ya mubaya, haitakuwa tena lazima kuendelea kumuona sawa mutu mwenye kutiwa alama.
KUSHUGULIKIA MAKOSA MAZITO
13 Kuacha makosa ya kidogo-kidogo ya ndugu zetu na kuzoea kuwasamehe, haimaanishe kama tunaunga mukono zambi ao kuifungia macho. Hatuwezi kusema kama kila kosa yenye mutu anafanya ni juu ya kukosa kukamilika, na haiwezi kuwa muzuri kuachilia ao kufunga macho wakati mutu anafanya zambi nzito. (Law. 19:17; Zb. 141:5) Agano ya Sheria ilionyesha kama kuko zambi zenye kuwa nzito kuliko zingine, na ni vile pia mu kutaniko ya Kikristo.—1 Yo. 5:16, 17.
14 Yesu alionyesha waziwazi hatua za kufuata juu ya kumaliza matatizo mazito yenye inaweza kutokea kati ya Wakristo. Alisema hivi: “Kama ndugu yako anatenda zambi, [1] uende ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yake. Kama anakusikiliza, umemupata ndugu yako. Lakini kama hasikilize, [2] chukua pamoja na wewe mutu mumoja ao wawili zaidi, ili kila jambo lihakikishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili ao watatu (3). Kama hawasikilize hao, [3] uambie kutaniko. Kama hasikilize hata kutaniko, acha akuwe kwako kama mutu wa mataifa na kama mukusanya-kodi.”—Mt. 18:15-17.
15 Mufano wenye kuwa mu Matayo 18:23-35, wenye Yesu alitoa kisha kuzungumuzia zile hatua, unatusaidia kuona kama zambi moya kati ya zambi zenye kuzungumuziwa mu andiko ya Matayo 18:15-17, inahusu mambo ya mali ao makuta, sawa viile, kukosa kulipa deni ao kudanganya juu ya kupata kitu ya mutu mwingine. Inaweza kuwa pia kuharibisha sana sifa ya mutu kwa kusema mambo ya uongo juu yake.
16 Pengine unasema, kuko mutu ashanitendea vile mu kutaniko. Kama ni vile, usiende haraka kuambia wazee juu wakusaidie. Yesu alisema kama unapaswa kuzungumuza kwanza na mutu mwenye alikukosea. Mujikaze kumaliza ile shida nyie wawili. Kumbuka, Yesu hakusema ‘uende funua kosa yake, mara moya tu.’ Kwa hiyo, kama hakubali kosa yake na haombe musamaha, inaweza kuwa muzuri ufikirie kuenda muona tena kisha muda fulani. Kama munamaliza shida mu ile njia, ule mwenye alikukosea atafurahi sana juu haukuambia wengine kosa yake na haukuchafua jina yake mu kutaniko. Utakuwa “umemupata ndugu yako.”
17 Kama mwenye alikukosea anakubali kosa yake na anakuomba musamaha, na kama anachukua hatua fulani ya kutengeneza kosa yake, hakutakuwa lazima ya kufanya hatua ingine. Hata kama kosa yenye alikutendea iko nzito, kosa ya vile inaweza kumalizwa na watu wawili wenye walikoseana.
18 Kama unashindwa kumupata ndugu yako kwa kumuonyesha kosa yake “kati yako na yeye peke yake,” pale sasa unaweza kufanya vile Yesu alisema, “chukua pamoja na wewe mutu mumoja ao wawili zaidi,” juu ya kuzungumuza tena na ndugu yako. Wale wenye unachagua ili kuenda kuzungumuza na ndugu yako, wanapaswa pia kuwa na kusudi ya kumupata ndugu yako. Inaweza kuwa muzuri wakuwe watu wenye walijionea ile jambo wakati ilifanyika. Lakini, kama hakuna, unaweza kuchagua ndugu moya ao wawili juu wakuwe sasa washuhuda wa mazungumuzo yenu. Wanaweza kuwa na uzoefu ya kumaliza mambo ya vile na wanaweza kujua kama jambo yenye ilitendeka ni kosa kabisa ao hapana. Kama unachagua wazee fulani wakuwe washuhuda wako, ujue kama ile wakati hawatumwe na kutaniko, juu haiko baraza ya wazee njo iliwatuma moja kwa moja kufanya vile.
19 Kama umefanya yako yote, ni kusema, umeenda kumuona mara mingi, umeenda kumuona na mutu mumoya ao wawili zaidi, lakini tatizo yenu haiishe, na unaona kama hauwezi kuachilia ile jambo, basi uipeleke kwa wachungaji wa kutaniko. Kumbuka, kusudi ya wazee mu kutaniko ni kulinda amani na usafi mu kutaniko. Kisha kuelezea wazee ile jambo, unaweza sasa kuiacha mu mikono yao na kumutumainia Yehova. Usiruhusu hata kidogo mwenendo mubaya ya mutu mwingine ikukwaze ao ikufanye upoteze furaha yako wa kazi ya Yehova.—Zb. 119:165.
20 Wachungaji wa kundi watachunguza ile jambo. Kama inaonekana wazi kabisa kama ule mutu alikufanyia kosa nzito, hapendi kutubu, na hapendi kutengeneza kosa yake vile inaomba, wazee wanaweza kuona kama ni lazima atengwe na kutaniko. Kufanya vile, inasaidia kulinda kondoo wa Mungu na pia usafi wa kutaniko.—Mt. 18:17.
KUSHUGULIKIA ZAMBI NZITO
21 Kuhusu zambi nzito, kama vile, uasherati, uzinifu, mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke, kukufuru, uasi-imani, kuabudu sanamu, na zambi zingine nzito, haitoshe tu kusamehewa na mutu mwenye alikosewa. (1 Ko. 6:9, 10; Gal. 5:19-21) Juu ya nini? Juu, ni zambi zenye zinaweza kutia hali ya kiroho ya kutaniko mu hatari na kuichafua. Kwa hiyo, wazee wanapaswa kujulishwa juu wazishugulikie. (1 Ko. 5:6; Yak. 5:14, 15) Wakristo fulani wanaweza kuwaendea wazee juu ya kutubu zambi zao wenyewe ao juu ya kuwajulisha kuhusu zambi za Wakristo wengine. (Law. 5:1; Yak. 5:16) Ikuwe ni mu njia gani yenye wazee wanapata habari ya kama ndugu ao dada fulani mwenye kubatizwa amefanya zambi nzito, baraza ya wazee itachagua wazee wawili ili kufanya kwanza uchunguzi. Kama ile habari inahakikishwa kuwa ya kweli na kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama zambi nzito imefanywa, baraza ya wazee itafanya halmashauri ya hukumu yenye kufanyizwa na wazee watatu ao zaidi ili kushugulikia ile zambi.
22 Wazee wanapaswa kuwa macho juu ya kuchunga kundi ya Mungu isiharibiwe kiroho na kitu yoyote. Wanapaswa pia kujikaza kutumia kwa ufundi Neno ya Mungu ili kukaripia kila mutu mwenye ametenda zambi na kumusaidia akuwe tena na afya muzuri ya kiroho. (Yud. 21-23) Ile inapatana na maagizo yenye mutume Paulo alitoleaka Timoteo. Alimuandikiaka hivi: “Ninakuagiza kwa uzito mbele ya Mungu na Kristo Yesu, mwenye atahukumu wazima na wafu, . . . karipia, kemea, chochea, kwa uvumilivu wote na ufundi wa kufundisha.” (2 Ti. 4:1, 2) Kufanya vile, inaweza kuomba wakati mingi, lakini ni sehemu ya kazi ya nguvu yenye wazee wa kutaniko wamepewa. Ndugu na dada wanapendezwa na bidii yao na wanaona kama wanastahili kupewa “heshima mara mbili.”—1 Ti. 5:17.
23 Mu kila hali yenye inaonyesha wazi kama zambi nzito imefanywa, kusudi ya kwanza ya wazee ni kusaidia mutu mwenye alifanya zambi akuwe tena na afya ya muzuri kiroho. Kama anatubu kwelikweli na anakubali musaada ya wazee, atakaripiwa kwa siri ao mbele ya wale wote wenye walishuhudia wakati halmashauri ya hukumu ilikuwa namusikiliza. Ile karipio, itamupatia somo na itasaidia watazamaji pia waogope kufanya zambi. (2 Sa. 12:13; 1 Ti. 5:20) Kila mara, wakati halmashauri ya hukumu inakaripia mutu, ule mutu anapaswa kuwekewa vizuizi fulani. Ile inaweza kusaidia mutenda-zambi afanyie miguu yake “njia zenye kunyooka.” (Ebr. 12:13) Kisha wakati fulani, ikionekana wazi kama amefanya maendeleo ya kiroho, vile vizuizi vitaondolewa.
KUTANGAZA KARIPIO
24 Kama halmashauri ya hukumu inaona kama mutenda-zambi ametubu kabisa, lakini kile alifanya kinaweza kujulikana ndani ao inje ya kutaniko, ao itaomba ndugu na dada wafanye angalisho naye, tangazo ya mufupi itatolewa ku Mukutano Utumishi na Maisha. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya mutu] amekaripiwa.”
KAMA UAMUZI NI KUTENGA MUTU NA KUTANIKO
25 Mu hali fulani, inawezekana mukosaji alishazoea sana kufanya zambi, na wazee wanajikaza kumusaidia lakini anakatala. Itaomba kufanya nini, halmashauri ya hukumu ikiona kama mutenda-zambi hana kabisa ‘matendo yenye inaonyesha kama ametubu’? (Mdo. 26:20) Mu hali ya vile, itaomba kumutosha mu kutaniko, juu asiendelee tena kushirikiana na watu wa Yehova wenye kuwa safi. Ile, inasaidia kutosha uvutano mubaya mu kutaniko, inafanya kutaniko iendelee kuwa mu hali ya muzuri na yenye kuwa safi kiroho, na inalinda sifa ya muzuri ya kutaniko. (Kum. 21:20, 21; 22:23, 24) Wakati mutume Paulo alipata habari ya mutu fulani mwenye alikuwa na mwenendo ya haya kabisa mu kutaniko ya Korinto, alishauria wazee wa ile kutaniko kama ‘wamutoe mutu wa namna hiyo kwa Shetani . . . , ili roho [ya kutaniko] iokolewe.’ (1 Ko. 5:5, 11-13) Mutume Paulo aliandika pia juu ya watu fulani wenye walitengwa na kutaniko wakati wa mitume juu walipinga mafundisho ya ile kweli.—1 Ti. 1:20.
26 Kama halmashauri ya hukumu inachukua uamuzi wa kutenga mukosaji mwenye hatubu, inapaswa kumujulisha ile uamuzi na kumuonyesha waziwazi sababu za Maandiko zenye zinafanya atengwe na kutaniko. Kisha kumujulisha, halmashauri ya hukumu inapaswa kumuambia kama ikiwa anaona kumetokea kosa kubwa mu ile hukumu, anaweza kutumia halmashauri ya hukumu barua ya kuomba uamuzi ichunguzwe tena, na kufasiria waziwazi juu ya nini anapenda vile. Na atapewa siku saba ili kufanya vile, kuanzia siku yenye alijulishwa uamuzi wa kutengwa. Wakati wazee wanapokea ile barua, baraza ya wazee itazungumuza na mwangalizi wa muzunguko. Mwangalizi atachagua wazee wenye kuwa na uzoefu ili wafanyize halmashauri ya kuchunguza tena uamuzi. Wale wazee watajikaza kufanya vile, mbele juma moya ipite kisha kupokea ile barua ya kuomba uamuzi uchunguzwe tena. Kama mukosaji aliomba uamuzi uchunguzwe tena, tangazo ya kutengwa kwake haitatolewa kwanza. Lakini, atazuiwa kutoa maelezo na kusali ku mikutano, na hataachiwa mapendeleo ya pekee ya utumishi.
27 Kuachia mukosaji nafasi ya kuomba uamuzi ichunguzwe tena, ni kumuonyesha wema. Kwa hiyo, kama anakatala kimakusudi kufika ili asikilizwe na halmashauri ya kuchunguza tena uamuzi, tangazo ya kutengwa na kutaniko itafanywa kisha wazee kufanya yao yote ili kukutana naye.
28 Kama mukosaji hapendi kuomba uamuzi ichunguzwe tena, halmashauri ya hukumu itamufasiria faida ya kutubu na kumuonyesha hatua zenye anaweza kufanya juu siku ingine arudishwe tena mu kutaniko. Kusudi ya wazee ni kumusaidia, na watafanya vile kwa wema. Watatumainia kama mashauri yenye wanamupatia itamusaidia abadilishe mwenendo yake ili astahili kurudishwa mu tengenezo ya Yehova.—2 Ko. 2:6, 7.
TANGAZO YA KUTENGWA NA KUTANIKO
29 Wakati inaonekana kama ni lazima kutenga mutu na kutaniko, tangazo ya mufupi itatolewa. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya mutu] haiko tena mumoja wa Mashahidi wa Yehova.” Ile tangazo itasaidia ndugu na dada waaminifu mu kutaniko waache kushirikiana naye.—1 Ko. 5:11
KUJITENGA NA KUTANIKO
30 Maneno “kujitenga na kutaniko” inatumiwa wakati mutu mwenye kubatizwa anakatala kimakusudi musimamo wake wa Kikristo kwa kusema kama hapendi tena kuitwa ao kujulikana kuwa Shahidi wa Yehova. Ao anaweza kuacha kutaniko ya Kikristo kupitia matendo yake, kwa mufano, anaweza kujiunga na shirika fulani ya kiulimwengu yenye Yehova Mungu atahukumu, juu mambo yenye ile shirika inafanyaka inapingana na mafundisho ya Biblia.—Isa. 2:4; Ufu. 19:17-21.
31 Mutume Yohana aliandika hivi juu ya watu wa siku zake wenye walikatalaka imani yao ya Kikristo: “Walitoka katikati yetu, lakini hawakukuwa wa namna yetu; kwa maana kama wangekuwa wa namna yetu, wangebakia pamoja na sisi. Lakini walitoka ili ionekane kwamba haiko wote ndio wa namna yetu.”—1 Yo. 2:19.
32 Yehova anaona hali ya mutu mwenye anajitenga na kutaniko kuwa tofauti sana na ya Mukristo mwenye hatende tena. Mukristo fulani anaweza kuacha kuhubiri juu hajifunze tena kwa ukawaida Neno ya Mungu, Biblia. Ao amepoteza bidii yake mu kazi ya Yehova juu ya magumu ao majaribu yenye anapata mu maisha. Wazee na wengine mu kutaniko wataendelea kumutolea Mukristo wa vile musaada ya kiroho yenye kufaa.—Ro. 15:1; 1 Te. 5:14; Ebr. 12:12.
33 Lakini, kama Mukristo anaamua yeye mwenyewe kujitenga na kutaniko, tangazo ya mufupi itatolewa mu kutaniko. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya mutu] haiko tena mumoja wa Mashahidi wa Yehova.” Ule mutu atatendewa sawasawa na mutengwa.
KURUDISHWA MU KUTANIKO
34 Mutu mwenye kutengwa na kutaniko ao mwenye kujitenga anaweza kurudishwa tena mu kutaniko. Lakini, anapaswa kwanza kuonyesha wazi kama ametubu, na wakati ya kutosha inapaswa kuwa imepita ili ionekane waziwazi kama alishaachana kabisa na mwenendo yake ya mubaya. Anapaswa kuonyesha kama anapenda kabisa kuwa tena na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova. Wazee wanapaswa kuwa waangalifu kwa kuacha wakati ya kutosha ipite, kwa mufano, miezi, mwaka, ao zaidi, kupatana na hali, ili mutu mwenye kutengwa aonyeshe kabisa kama ametubu. Wakati wazee wanapata barua ya mutu ya kuomba kurudishwa, halmashauri ya kurudisha itazungumuza naye. Ile halmashauri itachunguza juu ya kuona kama ule mutu amekuwa na ‘matendo yenye inaonyesha kama ametubu’ na itaamua kama anaweza kurudishwa mu kutaniko ile wakati ao hapana.—Mdo. 26:20.
35 Kama mutu mwenye anaomba kurudishwa alitengwa na iko mu kutaniko ingine, halmashauri ya kurudisha ya kutaniko ya sasa njo itazungumuza naye na kuchunguza barua yake ya kupenda kurudishwa. Kisha, ile halmashauri itaandikia baraza ya wazee wa kutaniko yenye ilishugulikiaka ile kisa, na kuitolea mawazo ao mapendekezo yao. Halmashauri zote mbili zitatumika pamoya juu ya kuhakikisha kama mambo yote imechunguzwa muzuri, juu ya kufanya uamuzi wenye kufaa. Lakini, ni halmashauri ya kurudisha ya kutaniko yenye ilishugulikiaka ile kisa njo itaamua tena kama anaweza kurudishwa mu kutaniko ao hapana.
TANGAZO YA KURUDISHWA MU KUTANIKO
36 Kama halmashauri ya kurudisha iko hakika kabisa kama mutu mwenye kutengwa ametubu kwelikweli na kama anapaswa kurudishwa tena mu kutaniko, tangazo ya kurudishwa kwake itatolewa mu kutaniko yenye ilishugulikiaka kisa yake. Kama sasa iko mu kutaniko ingine, tangazo itafanywa pia mu ile kutaniko. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya Mutu] amerudishwa kama mumoja wa Mashahidi wa Yehova.”
ZAMBI NZITO YA MUTOTO MUDOGO MWENYE KUBATIZWA
37 Wazee wa kutaniko wanapaswa kujulishwa zambi nzito ya mutoto mudogo (mwenye kuwa chini ya miaka 18) mwenye kubatizwa. Wakati wazee wanashugulikia zambi nzito ya mutoto mudogo mwenye kubatizwa, ni muzuri sana wazazi wake wenye kubatizwa wakuwe pale. Itakuwa muzuri washirikiane na halmashauri ya hukumu, na wasijaribu kutetea mutoto wao, juu ile inaweza kumuzuia kupata musaada yenye inaweza kumusaidia kiroho. Vile halmashauri ya hukumu inafanyaka kuhusu watu wazima, ni vile itafanya ili kukaripia na kusaidia kiroho mutoto mwenye amefanya zambi. Lakini, kama ule mutoto hapendi kutubu, halmashauri ya hukumu itachukua uamuzi ya kumutenga na kutaniko.
ZAMBI NZITO YA MUHUBIRI MWENYE HAYABATIZWA
38 Wazee wanapaswa kufanya nini wakati muhubiri mwenye hayabatizwa anafanya zambi nzito? Juu hayakuwa Shahidi mwenye kubatizwa, hawezi kutengwa na kutaniko. Pengine hayaelewa muzuri kabisa kanuni za Biblia. Kwa hiyo, shauri yenye inatolewa kwa njia ya upendo inaweza kumusaidia afanyie miguu yake “njia yenye kunyooka.”—Ebr. 12:13.
39 Kama mutenda-zambi mwenye hayabatizwa anakosa kutubu wakati wazee wawili wamejikaza kumusaidia kiroho, ni jambo ya lazima kujulisha kutaniko. Tangazo fupi itatolewa mu kutaniko. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya mutu] hatambuliwe tena kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa.” Kuanzia pale, kutaniko itaanza kumuona sawa tu mutu wa ulimwengu. Hata kama hakutengwa kabisa na kutaniko, ndugu na dada wanapaswa kuepuka kufanya urafiki naye. (1 Ko. 15:33) Ripoti yake ya mahubiri haitakubaliwa tena.
40 Wakati fulani, mutu mwenye alikuwa muhubiri mwenye hayabatizwa anaweza kupenda tena kuwa muhubiri. Kama ni vile, wazee wawili watazungumuza naye ili wajue muzuri kama amefanya maendeleo ya kiroho. Wakiona kama anastahili kuwa tena muhubiri, tangazo ya mufupi itatolewa kutaniko. Ile tangazo itasomwa hivi: “[Jina ya mutu] amekuwa tena muhubiri mwenye hayabatizwa.”
YEHOVA ANABARIKI IBADA SAFI NA YENYE KUFANYWA MU AMANI
41 Kila mutu mwenye kuwa mu kutaniko ya Mungu leo, anaweza kufurahia hali ya muzuri sana ya kiroho yenye Yehova amepatia watu wake. Tuko na chakula mingi ya kiroho, na tuko na maji mingi ya ile kweli yenye kutufurahisha. Tena Yehova anatuhangaikia na kututunza kupitia mipango ya kiteokrasi yenye kuongozwa na Kristo. (Zb. 23; Isa. 32:1, 2) Hata kama tunaishi mu siku za mwisho zenye kuwa na magumu mingi sana, tunajisikia kuwa salama juu tuko mu paradiso ya kiroho.
Wakati tunajikaza kulinda usafi na amani mu kutaniko, tunafanya mwangaza ya kweli juu ya Ufalme iendelee kuangaza
42 Wakati tunajikaza kulinda usafi na amani mu kutaniko, tunafanya mwangaza ya kweli juu ya Ufalme iendelee kuangaza. (Mt. 5:16; Yak. 3:18) Kwa musaada wa Yehova Mungu, tutafurahi kuona watu wengi sana wanafikia kumujua na kutumika pamoya na siye ili kufanya mapenzi yake.