HABARI YA KUJIFUNZA YA 34
WIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu
Namna ya Kuonyesha Watenda-zambi Upendo na Rehema
“Mungu kwa fazili zake anajaribu kukuongoza kwenye toba.” —RO. 2:4.
WAZO KUBWA
Namna wazee wanajaribu kusaidia wenye wanafanya zambi nzito.
1. Kuko tumaini kwa ajili ya batu benye bamefanya zambi nzito?
MU HABARI yenye ilitangulia, tuliona namna mutume Paulo alishugulikia mutu mwenye alifanya zambi mu kutaniko ya Korinto. Ule mutu hakutubu na aliondolewa mu kutaniko. Lakini vile andiko ya musingi ya hii habari inaonyesha, inawezekana kusaidia batu fulani benye bamefanya zambi nzito. Inawezekana kubasaidia juu bafikie kutubu. (Ro. 2:4) Namna gani wazee wanaweza kubasaidia juu bafikie kutubu?
2-3. Tukijua kama Mukristo mwenzetu amefanya zambi nzito tunapaswa kufanya nini, na juu ya nini?
2 Juu wazee wasaidie mutu, wanapaswa kwanza kujua kama iko na lazima ya musaada. Sasa, tutafanya nini tukijua kama Mukristo mwenzetu amefanya zambi nzito, zambi yenye inaweza kumufanya aondolewe mu kutaniko? Tunapaswa kumutia moyo aende kuona wazee juu wamusaidie.—Isa. 1:18; Mdo. 20:28; 1 Pe. 5:2.
3 Tutafanya nini kama mutu mwenye alifanya zambi nzito anakatala kuenda kuzungumuza na wazee? Siye wenyewe tutaenda kuonana na wazee juu ule mutu apate musaada wenye iko nao lazima. Kufanya vile kunaonyesha kama tunapenda ndugu ao dada yetu na hatupendi kumupoteza. Kama ule Mukristo anaendelea kufanya zambi, urafiki wake pamoya na Yehova utaendelea kuharibika. Tena anaweza kufanya batu baseme mubaya juu ya kutaniko. Kwa hiyo, juu tunamupenda Yehova na tunapenda ule mutu mwenye alifanya zambi, kwa uhodari tunakamata hatua ya kuzungumuza na wazee.—Zb. 27:14.
NAMNA WAZEE WANASAIDIA WENYE WANAFANYA ZAMBI NZITO
4. Wazee wanakuwaka na muradi gani wakati wanakutana na mutu mwenye alifanya zambi nzito?
4 Baraza ya wazee itachagula wazee tatu kati yao wenye watatumika pamoya kama halmashauri.a Bale banaume banapaswa kuwa na kiasi na unyenyekevu. Hata kama banajikaza kusaidia Mukristo mwenye alikosea atubu, banaelewa kama habawezi kukaza mutu abadilike. (Kum. 30:19) Wazee wanajua kama haiko watenda-zambi wote njo watakubali musaada sawa Mufalme Daudi. (2 Sa. 12:13) Wakosaji fulani wanaweza kuamua kukatala mashauri ya Yehova. (Mwa. 4:6-8) Hata vile, kusudi ya wazee ni kusaidia mukosaji atubu kama inawezekana. Ni kanuni gani zinapaswa kuongoza wazee wakati wanakutana na mukosaji?
5. Wazee wanapaswa kukumbuka nini wakati wanakutana na mukosaji? (2 Timoteo 2:24-26) (Ona pia picha.)
5 Wazee wanaona mukosaji kuwa kondoo wa maana wa Yehova mwenye amepotea. (Lu. 15:4, 6) Kwa hiyo wakati wanakutana naye hawapaswe kuzungumuza naye kwa ukali ao kumutendea bila upendo. Na hawaone mazungumuzo yenye wanafanya pamoya naye kuwa jambo ya kawaida yenye wanapaswa tu kufanya juu ya kujua vile mambo ilikuwa. Lakini, wataonyesha sifa zenye kuwa mu 2 Timoteo 2:24-26. (Soma.) Wazee wataendelea kuwa wapole wakati wako najikaza kugusa moyo wa mukosaji.
Sawa wachungaji wa zamani, wazee wanajikaza kutafuta kondoo mwenye amepotea (Ona fungu ya 5)
6. Namna gani wazee wanaweza kutayarisha moyo wao mbele ya kukutana na mukosaji? (Waroma 2:4)
6 Wazee wanatayarisha moyo wao. Wanajikaza kumuiga Yehova mu namna yao ya kushugulikia mutu mwenye alifanya zambi. Wanakumbuka hii maneno ya Paulo: “Mungu kwa fazili zake anajaribu kukuongoza kwenye toba.” (Soma Waroma 2:4.) Wazee wanapaswa kukumbuka kama kazi yao kubwa ni kuwa wachungaji chini ya muongozo wa Yesu. (Isa. 11:3, 4; Mt. 18:18-20) Mbele ya kukutana na mukosaji, halmashauri itasali na kufikiria muradi wao, ni kusema kusaidia mukosaji atubu. Watatafuta habari mu Maandiko na bichapo yetu, na watasali juu Yehova awapatie utambuzi. Watatafuta pia kujua habari juu ya maisha ya ule mutu yenye inaweza kuwasaidia waelewe juu ya nini pengine aliwaza ao kutenda mu njia fulani.—Mez. 20:5.
7-8. Namna gani wazee wanaweza kuiga uvumilivu wa Yehova wakati wanakutana na mukosaji?
7 Wazee wanaiga uvumilivu wa Yehova. Wanaendelea kukumbuka namna Yehova alitendea wakosaji zamani. Kwa mufano, kwa uvumilivu Yehova alifikiri na Kaini na kumuonya juu ya matokeo ya mubaya ya zambi, na alionyesha kama atamubariki ikiwa anabadilika. (Mwa. 4:6, 7) Yehova alituma nabii Natani juu ya kumushauria Daudi, na Natani alitumia mufano wenye uligusa moyo wa Daudi. (2 Sa. 12:1-7) Na Yehova ‘aliendelea kutuma’ manabii wake “tena na tena” kwa taifa ya Israeli wakati hawakumutii. (Yer. 7:24, 25) Yehova hakukuwa nangoya batu yake batubu njo abasaidie. Lakini, alikamata hatua ya kwanza ya kubaomba batubu.
8 Wazee wanafuata mufano wa Yehova wakati wanajikaza kusaidia wale wenye walifanya zambi nzito. Wanawatendea “kwa uvumilivu wote” sawa vile 2 Timoteo 4:2 inasema. Kwa hiyo, sikuzote muzee anapaswa kuwa mwenye kutulia juu asaidie mutenda-zambi apende kufanya mambo ya muzuri. Kama muzee anakasirika mutu anaweza kukatala kusikia mashauri ao kukatala kutubu.
9-10. Namna gani wazee wanaweza kusaidia mutenda-zambi afikirie mambo yenye ilimufikisha ku zambi?
9 Wazee wanajikaza kujua hali zenye zilifikisha mutu ku zambi. Kwa mufano, ule Mukristo alianza polepole kuacha kufanya funzo yake ya kipekee na kuhubiri? Hakukuwa nasali tena kwa ukawaida kwa Yehova ao alikuwa alishaanza kufanya sala za yulu-yulu? Alifuata tamaa yake ya mubaya? Alichagula barafiki ba babaya ao mambo ya kujifurahisha yenye haiko ya muzuri? Maamuzi yake imekuwa na matokeo gani juu ya moyo wake? Anaelewa kama maamuzi yenye alikamata na matendo yake inamuhuzunisha sana Baba yake Yehova?
10 Kama wazee wanauliza maulizo yenye kufaa bila kujiingiza mu maisha ya kipekee ya mutu, wanaweza kumusaidia afikiri juu ya mambo yenye ilimufikisha ku zambi. (Mez. 20:5) Zaidi ya ile, sawa vile Natani alisaidia Daudi, wazee wanaweza kutumia mufano juu ya kusaidia mutu afikiri na aelewe kama matendo yake ilikuwa ya mubaya. Pengine mu mazungumuzo ya kwanza yenye wazee watafanya na mutu mwenye alifanya zambi, ule mutu anaweza kuanza kuhuzunikia matendo yake na anaweza hata kutubu.
11. Yesu alitendea namna gani watenda-zambi?
11 Wazee wanajikaza kumuiga Yesu. Wakati fulani kisha Yesu kufufuliwa alizungumuza na Sauli na alimuuliza kwa hekima hii ulizo: “Sauli, Sauli, sababu gani unanitesa?” Kisha, Yesu akamusaidia kufikiri juu ya matendo yake ya mubaya. (Mdo. 9:3-6) Na kuhusu “ule mwanamuke Yezebeli,” Yesu alisema hivi: “Nilimupatia wakati wa kutubu.”—Ufu. 2:20, 21.
12-13. Namna gani wazee wanaweza kupatia mukosaji wakati wa kutubu? (Ona pia picha.)
12 Kama Yesu, wazee hawapaswe kuamua haraka-haraka kama mukosaji hatatubu. Wakosaji fulani wanaweza kutubu wakati wanakutana kwa mara ya kwanza na wazee. Lakini wengine wanaweza kuwa na lazima ya wakati zaidi. Kwa hiyo wazee wanapaswa kupanga kukutana na mukosaji zaidi ya mara moya. Pengine kisha mazungumuzo ya kwanza pamoya na wazee, ule Mukristo mwenye alifanya zambi anaweza kuanza kufikiri sana juu ya mambo yenye walimuambia. Anaweza kuonyesha unyenyekevu na kusali kwa Yehova amusamehe. (Zb. 32:5; 38:18) Kwa hiyo wakati atakutana na wazee mara ingine, anaweza kuwa alishabadilisha mawazo yake, tofauti na vile alikuwa wakati alikutana na wazee kwa mara ya kwanza.
13 Juu ya kusaidia mutenda-zambi atubu, wazee wanajitia pa nafasi yake, na wanamutendea muzuri. Wanasali kwa Yehova na kutumainia kama atabariki mambo yote yenye wako najikaza kufanya, na kama ule Mukristo mwenye alifanya zambi atarudia ku mustari na kutubu.—2 Ti. 2:25, 26.
Wazee wanaweza kukutana zaidi ya mara moya na mukosaji juu ya kumupatia wakati wa kutubu (Ona fungu ya 12)
14. Wakati mutenda-zambi anatubu ni nani njo anastahili sifa, na juu ya nini?
14 Kama mutenda-zambi anatubu ile inaletaka furaha sana! (Lu. 15:7, 10) Ni nani anastahili sifa? Ni wazee? Kumbuka mambo yenye Paulo aliandika kuhusu watenda-zambi, aliandika hivi: “Pengine Mungu atawapatia toba.” (2 Ti. 2:25) Ni Yehova njo anastahili sifa, hapana mwanadamu, juu ni yeye njo alisaidia ule Mukristo abadilishe mawazo yake na namna yake ya kuona mambo. Paulo alionyesha mambo ya muzuri yenye inatokeaka kisha mutu kutubu. Ule mutu anaweza kuelewa muzuri zaidi kweli, anarudia ku mustari, na anaweza kuepuka mitego ya Shetani.
15. Namna gani wazee wanaweza kuendelea kusaidia mukosaji mwenye ametubu?
15 Wakati mukosaji anatubu, halmashauri itapanga kumufanyia ziara za uchungaji juu aendelee kupata musaada wenye iko nao lazima ili aepuke mitego ya Shetani na aendelee kutembea mu njia yenye kuwa sawa. (Ebr. 12:12, 13) Wazee hawaambie mutu yeyote juu ya jambo yenye mutenda-zambi alifanya. Lakini, ni jambo gani njo wazee wanapaswa kujulisha kutaniko?
‘KARIPIA MBELE YA WATAZAMAJI WOTE’
16. Kulingana na 1 Timoteo 5:20, “watazamaji wote” wenye Paulo anazungumuzia ni nani?
16 Soma 1 Timoteo 5:20. Paulo aliandikia ile maneno muzee mwenzake Timoteo wakati alikuwa nazungumuzia namna ya kushugulikia “wenye wanazoea kufanya zambi.” Alimaanisha nini? Hakumaanisha kama “watazamaji wote” wanapaswa tu kuwa kutaniko yote. Lakini alimaanisha batu kidogo benye pengine banajua juu ya ile zambi. Pengine balijionea ao mukosaji alibaambia kuhusu zambi yake. Ni bale batu tu njo wazee wataambia kama walisharekebisha ule mutenda-zambi.
17. Kama zambi nzito inajulikana sana mu kutaniko ao inawezekana itajulikana ni tangazo gani njo itafanywa, na juu ya nini?
17 Mu hali fulani inawezekana zambi yenye mutu alifanya inajulikana sana mu kutaniko ao inawezekana itajulikana. Kama ni vile “watazamaji wote” ni kutaniko yote. Kwa hiyo wazee watatangazia kutaniko kama ndugu ao dada fulani amekaripiwa. Juu ya nini? Paulo alisema hivi: “Ili ikuwe onyo kwa wengine” juu wasiangukie mu zambi.
18. Wazee watashugulikia namna gani Wakristo wenye kubatizwa wenye kuwa chini ya miaka 18 wenye wamefanya kosa nzito? (Ona pia picha.)
18 Tuseme nini juu ya Wakristo wenye kubatizwa wenye kuwa chini ya miaka 18 wenye wamefanya kosa nzito? Baraza ya wazee itatuma wazee wawili wakutane na ule Mukristo na bazazi yake Mashahidi.b Wale wazee watauliza bazazi mambo yenye balishafanya juu ya kusaidia mutoto wao abadilike na atubu. Kama ule mutoto iko najikaza kubadilika na bazazi yake biko namusaidia, wale wazee wawili wanaweza kuamua kama haiko lazima ule mutoto pamoya na bazazi yake bakutane na halmashauri ya wazee. Kwa kweli, ni bazazi njo Yehova alipatia daraka ya kurekebisha batoto yao kwa upendo. (Kum. 6:6, 7; Mez. 6:20; 22:6; Efe. 6:2-4) Kisha pale wazee wataendelea kuzungumuza na bazazi juu ya kuhakikisha kama mutoto wao iko napata musaada wenye iko nao lazima. Lakini mambo itakuwa namna gani kama mutoto anakatala kutubu na anaendelea kufanya zambi? Mu ile hali, halmashauri ya wazee ni kusema wazee watatu watakutana naye pamoya na bazazi yake.
Wakati Mukristo wa chini ya miaka 18 anafanya zambi nzito, wazee wawili watakutana naye na bazazi yake (Ona fungu ya 18)
“YEHOVA NI MWENYE UPENDO MWINGI SANA NA MWENYE REHEMA”
19. Namna gani wazee wanajikaza kumuiga Yehova wakati wako nashugulikia wakosaji?
19 Yehova anaomba wazee walinde kutaniko juu iendelee kuwa safi. (1 Ko. 5:7) Lakini wazee wanafanya pia yao yote juu ya kusaidia mukosaji atubu wakati inawezekana. Njo maana wakati wazee wako nasaidia mukosaji wanatumainia kama atabadilika. Juu ya nini? Juu wanapenda kumuiga Yehova mwenye “upendo mwingi sana na mwenye rehema.” (Yak. 5:11) Ona namna mutume Yohana alionyesha kama anamuiga Yehova. Aliandika hivi: “Watoto wangu wadogo, ninawaandikia ninyi mambo haya ili musifanye zambi. Lakini, kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi kwa Baba, Yesu Kristo, mwenye haki.”—1 Yo. 2:1.
20. Tutazungumuzia nini mu habari ya mwisho ya mu hii gazeti?
20 Jambo ya kuhuzunisha ni kama, wakati fulani Mukristo anaweza kukatala kutubu. Na kama ni vile anapaswa kuondolewa mu kutaniko. Namna gani wazee wanashugulikia zile hali? Tutapata jibu ya ile ulizo mu habari ya mwisho ya mu hii gazeti.
WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji
a Zamani wale wazee tatu walikuwa naitwa halmashauri ya hukumu. Lakini juu kazi yao haiko tu kuhukumu hatutawaita tena vile. Tutawaita sasa halmashauri ya wazee.
b Mambo yenye inazungumuziwa juu ya wazazi inahusu pia wale wenye wanakubaliwa na sheria kuchunga ule mutoto ao wengine wenye wako natimiza daraka ya wazazi juu ya ule mutoto.