HABARI YA KUJIFUNZA YA 33
WIMBO 130 Tusameheane
Namna Kutaniko Inaweza Kuwa na Mawazo ya Yehova Juu ya Watenda-zambi
“Kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi.”—1 YO. 2:1.
WAZO KUBWA
Mambo yenye tunajifunza wakati tunachunguza namna kutaniko ya Korinto ya mu karne ya kwanza ilishugulikia mutu mwenye alifanya zambi nzito.
1. Yehova anapenda batu yote bafanye nini?
WAKATI Yehova aliumba wanadamu aliwapatia uhuru wa kuchagua. Tunatumikishaka ile zawadi kila wakati wenye tunakamata maamuzi. Uamuzi wa maana zaidi wenye mutu anaweza kukamata ni uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kuingia mu familia ya waabudu wake. Yehova anapenda batu yote bafanye vile. Juu ya nini? Juu anapenda batu na anapenda bakuwe na maisha ya muzuri. Anapenda bakuwe barafiki yake na baishi milele.—Kum. 30:19, 20; Gal. 6:7, 8.
2. Yehova anapenda watenda-zambi wenye hawayatubu wafanye nini? (1 Yohana 2:1)
2 Lakini, Yehova hakaze mutu kumutumikia. Anaacha kila mutu aamue mambo yenye atafanya. Sasa mambo itakuwa namna gani kama Mukristo mwenye kubatizwa anavunja sheria ya Mungu na kufanya zambi nzito? Kama hatubu, anapaswa kuondolewa mu kutaniko. (1 Ko. 5:13) Hata vile, Yehova anatumainia kabisa kama ule mutenda-zambi atamurudilia. Na ile njo sababu kubwa yenye ilifanya Yehova atoe zabihu ya ukombozi, juu watenda-zambi wenye kutubu waweze kusamehewa. (Soma 1 Yohana 2:1.) Yehova ni Mungu mwenye upendo sana, anaomba watenda-zambi watubu.—Zek. 1:3; Ro. 2:4; Yak. 4:8.
3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Yehova anapenda tukuwe na mawazo sawa yake kuhusu zambi na watenda-zambi. Mu hii habari, tutazungumuzia namna ya kufanya vile. Wakati uko nasoma hii habari, ona namna (1) kutaniko ya Korinto ya mu karne ya kwanza ilishugulikia mwanaume mwenye alifanya zambi nzito, (2) muongozo wenye mutume Paulo alipatia kutaniko ya Korinto wakati ule mwanaume alitubu, na (3) mambo yenye ile habari ya Biblia inatufundisha juu ya namna Yehova anaona Mukristo mwenye anafanya zambi nzito.
NAMNA KUTANIKO YA MU KARNE YA KWANZA ILIPASWA KUSHUGULIKIA MUTU MWENYE ALIFANYA ZAMBI NZITO
4. Ni nini ilitokea mu kutaniko ya Korinto mu karne ya kwanza? (1 Wakorinto 5:1, 2)
4 Soma 1 Wakorinto 5:1, 2. Wakati Paulo alikuwa mu safari yake ya tatu ya umisionere, alisikia habari fulani ya mubaya sana yenye ilikuwa natendeka mu kutaniko ya Korinto, kutaniko yenye ilitoka tu kuanzishwa. Ndugu fulani mu ile kutaniko alikuwa nafanya ngono na bibi ya baba yake. Ile ilikuwa mwenendo muchafu sana wenye ulikuwa “haujatokea hata kati ya watu wa mataifa”! Lakini kutaniko iliona tu ni sawa ule ndugu aendelee kubakia mu kutaniko. Pengine bamoya mu kutaniko baliwaza kama ile inaonyesha kuwa Yehova iko na huruma sana na anaelewa sana wanadamu wenye hawakamilike. Lakini Yehova haruhusu matendo ya mubaya kati ya watu wake. Ni wazi kama, ile matendo ya buchafu ya ule mwanaume ilifanya batu baseme mubaya juu ya kutaniko. Na bengine mu kutaniko, bangeanza kumuiga. Sasa, Paulo aliambia kutaniko ifanye nini?
5. Paulo aliambia kutaniko ifanye nini, na alimaanisha nini? (1 Wakorinto 5:13) (Ona pia picha.)
5 Soma 1 Wakorinto 5:13. Kwa muongozo wa roho ya Mungu, Paulo aliandika barua, na mu ile barua alionyesha kama ule mutenda-zambi mwenye hakutubu, alipaswa kuondolewa mu kutaniko. Wakristo waaminifu walipaswa kumutendea namna gani? Paulo aliwaambia hivi: “Muache kushirikiana” pamoya naye. Maana yake nini? Paulo alifasiria kama ile ilimaanisha kama hawakupaswa ‘hata kula chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.’ (1 Ko. 5:11) Kwa kawaida, saa ya kula njo batu banaongeaka, na ile inaweza kufanya baanze kupitisha wakati pamoya. Mambo iko wazi, Paulo alimaanisha kama kutaniko haikupaswa kupitisha wakati na ule mwanaume. Ile ingelinda kutaniko juu tabia yake isiambukie bengine. (1 Ko. 5:5-7) Zaidi ya ile, kuepuka kuwa karibu na ule mwanaume kungemusaidia aelewe kama alifanya mambo yenye ilimuumiza sana Yehova, kisha angehuzunika, na ile ingemuchochea atubu.
Kwa muongozo wa roho ya Mungu, Paulo aliandika barua, na mu ile barua alionyesha kama ule mutenda-zambi mwenye hakutubu alipaswa kuondolewa mu kutaniko (Ona fungu ya 5)
6. Kutaniko ilifanya nini kisha kupata barua ya Paulo, na ule mutenda-zambi alifanya nini?
6 Kisha Paulo kutumia Wakristo wa Korinto barua yake, alianza kujiuliza kutaniko itatenda namna gani kisha kuipata. Kisha, Tito akamuletea habari ya muzuri. (2 Ko. 7:6, 7) Kutaniko ilifuata mashauri yenye ilikuwa mu barua yake na ilitosha ule mwanaume mu kutaniko. Zaidi ya ile, mu miezi yenye ilifuata tangu Paulo atume barua yake, ule mwanaume alikuwa alishatubu, alikuwa alishabadilisha mawazo yake na tabia yake, na alianza kufuata kanuni za Yehova zenye haki. (2 Ko. 7:8-11) Paulo aliambia kutaniko ifanye sasa nini?
NAMNA KUTANIKO ILITENDEA MUTENDA-ZAMBI MWENYE ALITUBU
7. Kuondoa ule mutenda-zambi mu kutaniko kulikuwa na matokeo gani ya muzuri? (2 Wakorinto 2:5-8)
7 Soma 2 Wakorinto 2:5-8. Paulo alisema kama “kemeo lenye linatolewa na wenye kuwa wengi linatosha kwa mutu wa namna hiyo.” Mu maneno ingine, ni kusema nizamu yenye balimupatia ilitimiza kusudi yake. Kusudi gani? Ilimuongoza kwenye toba.—Ebr. 12:11.
8. Paulo aliambia kutaniko ifanye nini sasa?
8 Kwa hiyo, Paulo aliambia kutaniko hivi: “Munapaswa kumusamehe kwa fazili na kumufariji” ule ndugu mwenye alikuwa amekosea, na “mumuhakikishie upendo wenu.” Ona kama Paulo hakuomba tu kutaniko imukubali tena kati ya watu wa Mungu, lakini ilipaswa kufanya mambo mingi zaidi. Paulo alipenda ndugu na dada wahakikishie ule mwanaume mwenye alitubu, kupitia maneno na matendo yao, kama wamemusamehe kabisa na wanamupenda. Kwa kufanya vile, wangeonyesha wazi kama wanamukaribisha tena mu kutaniko.
9. Juu ya nini pengine ilikuwa nguvu kwa Wakristo fulani kusamehe ule mutenda-zambi mwenye alitubu?
9 Ilikuwa nguvu kwa Wakristo fulani kukaribisha tena ule mutenda-zambi mu kutaniko? Biblia haiseme, lakini inaonekana haikukuwa mwepesi kwa Wakristo fulani. Matendo yake ililetea kutaniko yote magumu na pengine iliumiza kipekee ndugu ao dada fulani mu kutaniko. Pengine Wakristo wenye walijikaza sana kuendelea kuwa na mwenendo muzuri, waliona kama haiko muzuri kukaribisha tena mu kutaniko mwanaume mwenye alifanya mambo ya vile. (Linganisha na Luka 15:28-30.) Juu ya nini ilikuwa jambo ya maana kutaniko ionyeshe upendo wa kweli ule ndugu mwenye alikuwa ametubu?
10-11. Nini ingetokea kama wazee wangekatala kusamehe ule mutenda-zambi mwenye alitubu?
10 Wazia namna mambo ingekuwa kama wazee wangekatala kurudisha mu kutaniko ule mwanaume mwenye alitubu, ao kama kisha kumurudisha kutaniko ingekatala kumuonyesha upendo. Ule mwanaume angelemewa na “huzuni yenye kupita kiasi.” Angeona kama hatamutumikiaka Yehova tena. Na hata angeacha kujikaza kurudisha uhusiano wake pamoya na Yehova.
11 Jambo ya mubaya zaidi ni: kama ndugu na dada mu kutaniko wangekatala kusamehe ule mutenda-zambi mwenye alitubu, urafiki wao pamoya na Yehova ungekuwa mu hatari. Juu ya nini? Juu kwa kufanya vile, hawangekuwa naiga Yehova mwenye anakuwaka tayari kusamehe watenda-zambi wenye kutubu, lakini wangekuwa naiga Shetani mwenye hakuwake na huruma na mwenye ni mukali. Wangekuwa sasa vyombo vyenye Shetani anatumikisha juu ya kuharibu hali ya kiroho ya ule mwanaume.—2 Ko. 2:10, 11; Efe. 4:27.
12. Kutaniko ingemuiga Yehova namna gani?
12 Sasa, namna gani kutaniko ya Korinto ingemuiga Yehova, hapana Shetani? Kwa kutendea watenda-zambi wenye wanatubu namna Yehova anawatendeaka. Ona mambo yenye waandikaji fulani wa Biblia walisema juu ya Yehova. Daudi alisema hivi juu ya Yehova: “Uko mwema na uko tayari kusamehe.” (Zb. 86:5) Mika aliandika hivi: “Ni Mungu gani mwenye kuwa kama wewe, mwenye kusamehe makosa na mwenye haangalie makosa?” (Mik. 7:18) Na Isaya alisema: “Mutu muovu aache njia yake na mutu mubaya mawazo yake; na amurudilie Yehova, mwenye atamuonyesha rehema, kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.”—Isa. 55:7.
13. Juu ya nini ilikuwa muzuri kurudisha mu kutaniko ule mutenda-zambi mwenye alitubu? (Ona kisanduku “Ule Mwanaume wa mu Korinto Alirudishwa Wakati Gani?”)
13 Ili kumuiga Yehova, kutaniko ya Korinto ilipaswa kukaribisha mu kutaniko ule mwanaume mwenye alitubu na kumuhakikishia kama wanamupenda. Kutaniko ilifuata muongozo wa Paulo na kukaribisha tena ule mutenda-zambi mwenye alitubu. Kwa kufanya vile ndugu na dada walionyesha kama walikuwa “watiifu katika mambo yote.” (2 Ko. 2:9) Kusema kweli, kulipita tu miezi tangu ule mwanaume aondolewe mu kutaniko, lakini nizamu ilimuongoza kwenye toba. Kwa hiyo hakukukuwa sababu ya kukawia kumurudisha mu kutaniko.
NAMNA TUNAWEZA KUIGA HAKI NA REHEMA YA YEHOVA
14-15. Namna kutaniko ya Korinto ya zamani ilishugulikia mutu mwenye alifanya zambi nzito inatufundisha nini? (2 Petro 3:9) (Ona pia picha.)
14 Habari juu ya namna kutaniko ya zamani ya Korinto ilishugulikia mutu mwenye alifanya zambi nzito iliandikwa mu Biblia “ili kutufundisha.” (Ro. 15:4) Kupitia ile habari, tunajifunza kama Yehova haruhusu zambi nzito kati ya watu wake. Watu fulani wanaweza kuwaza kama juu Yehova ni Mungu mwenye “rehema,” watenda-zambi wenye hawatubu wanapaswa kuruhusiwa kuendelea kujiunga na waabudu waaminifu. Lakini ile haiko rehema ya Yehova; Yehova iko na rehema lakini haachiliake mambo, hapunguzake uzito wa kanuni zake. (Yud. 4) Kuruhusu watenda-zambi wenye hawatubu wabakie mu kutaniko, haiko kuonyesha rehema juu ile inaweza kutia kutaniko yote mu hatari.—Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33.
15 Lakini, tumejifunza kama Yehova hapendi mutu yeyote aharibiwe. Anapenda kuokoa watu kila wakati wenye inawezekana. Anaonyesha rehema watu wenye wanabadilisha moyo wao na wenye wanapenda tena kuwa na urafiki muzuri pamoya naye. (Eze. 33:11; soma 2 Petro 3:9.) Njo maana, wakati ule mwanaume wa Korinto alitubu na kuacha zambi yake, Yehova alitumia Paulo juu ya kufasiria kutaniko kama ule mwanaume alipaswa kusamehewa na kukaribishwa tena mu kutaniko.
Kutaniko inaonyesha upendo na rehema ya Yehova kwa kukaribisha kwa furaha wale wenye wanarudishwa mu kutaniko (Ona fungu ya 14-15)
16. Kuona namna kutaniko ya Korinto ilishugulikia mwanaume mwenye alifanya zambi nzito, inakufundisha nini juu ya Yehova?
16 Kuchunguza namna kutaniko ya Korinto ilishugulikia mwanaume mwenye alifanya zambi nzito, kunatusaidia kuona kama Yehova iko na upendo, anapenda mambo yenye kuwa sawa na ni mwenye haki. (Zb. 33:5) Kujua ile kunapaswa kukuchochea umusifu Yehova zaidi. Kusema kweli, siye wote tuko watenda-zambi na tuko na lazima ya musamaha wa Yehova. Kila mumoya wetu anapaswa kuonyesha Yehova shukrani juu ya bei ya ukombozi, yenye inafanya iwezekane tusamehewe. Inatia moyo sana kujua kama Yehova anapenda sana batu yake na anapenda bakuwe na maisha ya muzuri!
17. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?
17 Sasa, mambo inakuwaka namna gani juu ya wale wenye wanafanya zambi nzito leo? Kama Yehova, namna gani wazee wanaweza kuonyesha kama wanapenda kusaidia mutenda-zambi atubu? Kutaniko inapaswa kutenda namna gani wakati wazee wanaamua kuondoa ao kurudisha mutu mu kutaniko? Tutapata majibu ya ile maulizo mu habari zenye kufuata.
WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo