Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 9 uku. 2-7
  • ‘Ita Bazee’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Ita Bazee’
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NI WAKATI GANI NJO TUNAPASWA ‘KUITA BAZEE’?
  • JUU YA NINI TUNAPASWA KUITA BAZEE?
  • BAZEE BANATUSAIDIA NAMNA GANI?
  • JAMBO YENYE KILA MUMOYA WETU ANAPASWA KUFANYA
  • Namna ya Kuonyesha Watenda-zambi Upendo na Rehema
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Namna Kutaniko Inapangwa
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Ndugu—Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Wazee?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Wachungaji Wenye Wanasaidia Watu wa Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 9 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 36

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

‘Ita Bazee’

“Aite wazee wa kutaniko.”—YAK. 5:14.

WAZO KUBWA

Namna bazee banatusaidia wakati tuko na lazima ya musaada.

1. Yehova anaonyesha namna gani kama anaona kondoo wake kuwa wa maana?

Yehova anaona kondoo wake kuwa wa maana sana. Alitoa Mwana wake juu yao na ameweka bazee ba kutaniko juu ya kuwahangaikia. (Mdo. 20:28) Yehova anapenda bazee batendee kondoo kwa upole. Bazee banafuata mwongozo wa Yesu, na banatia moyo na kulinda kondoo wa Mungu juu wasiangukie mu hatari ya kiroho.—Isa. 32:​1, 2.

2. Yehova anahangaikia zaidi sana nani? (Ezekieli 34:​15, 16)

2 Yehova anahangaikia kondoo wake wote, zaidi sana wale wenye wako nateseka. Kondoo fulani wako nateseka juu walifanya makosa, na Yehova anatumikisha bazee juu ya kuwasaidia. (Soma Ezekieli 34:​15, 16.) Yehova anapenda tutafute musaada wakati tuko nao lazima. Wakati ya vile haitoshe tu kuomba Yehova atusaidie, tunapaswa pia kuomba musaada “wachungaji na walimu” mu kutaniko.—Efe. 4:​11, 12.

3. Kujua namna Yehova iko natumikisha bazee kunaweza kutusaidia namna gani siye bote?

3 Mu hii habari, tutaona namna Yehova anatumikisha bazee juu ya kusaidia bale benye biko zaifu kiroho. Tutajibia hii maulizo: Ni wakati gani njo tunapaswa kutafuta musaada wa bazee? Juu ya nini tunapaswa kufanya vile? Na namna gani bazee banatusaidia? Hata kama hatuko mu magumu hii wakati, kujua majibu ya ile maulizo kutatusaidia tukuwe wenye shukrani juu ya namna Yehova anatumikisha bazee ili kutusaidia. Na siku tutakuwa na lazima ya musaada wa bazee tutajua bya kufanya.

NI WAKATI GANI NJO TUNAPASWA ‘KUITA BAZEE’?

4. Tunajua namna gani kama Yakobo 5:​14-16, 19, 20 inazungumuzia mutu mwenye anagonjwa kiroho? (Ona pia picha.)

4 Mwanafunzi Yakobo anafasiria namna Yehova anatumia bazee juu ya kutusaidia. Anauliza hivi: “Je, kuko mutu yeyote mwenye kuwa mugonjwa kati yenu? Aite wazee wa kutaniko.” (Soma Yakobo 5:​14-16, 19, 20.) Mu hii maandiko Yakobo iko nazungumuzia mutu mwenye anagonjwa kiroho. Juu ya nini tunasema vile? Juu anaambia mugonjwa aite bazee hapana munganga. Zaidi ya ile, Yakobo anasema kama mutu anapona wakati zambi zake zinasamehewa. Mambo yenye mutu anafanyaka juu apone kiroho inafanana na yenye mutu anafanyaka juu apone kimwili. Kwa mufano, wakati mutu anagonjwa anaendaka kuona munganga, anamufasiria vile iko najisikia, na anafuata mambo yenye munganga atamuambia. Vilevile, wakati tunagonjwa kiroho tunapaswa kuonana na bazee, tunabafasiria hali yetu, na tunafuata mashauri ya Biblia yenye banatupatia.

Picha: 1. Mwanaume iko nafasiria munganga tatizo yenye iko nayo ku mabega. 2. Ndugu iko nafasiria muzee hali yake wakati banaikala inje.

Wakati tunagonjwa kimwili, tunaenda kwa munganga. Na wakati tunagonjwa kiroho, tunatafuta bazee (Ona fungu ya 4)


5. Tutajua namna gani kama tulishaanza kugonjwa kiroho?

5 Mu Yakobo sura ya 5, Yakobo anatutia moyo tuonane na bazee kama tuko na ugonjwa fulani wa kiroho. Lakini, ni jambo ya hekima tutafute musaada wa bazee mbele tufanye jambo yenye inaweza kuharibisha urafiki wetu pamoya na Yehova! Tukuwe baangalifu. Tunaweza kuwaza kama hali yetu ya kiroho iko muzuri kumbe hapana. (Yak. 1:22) Bakristo fulani ba kwanza-kwanza ba mu kutaniko ya Sardi baliangukia mu ile mutego, na Yesu alibaonya juu ya hali yabo ya kiroho. (Ufu. 3:​1, 2) Juu ya kujua kama hali yetu ya kiroho iko muzuri ao hapana, tunaweza kulinganisha bidii yenye tulikuwaka nayo zamani mu mambo ya kiroho na yenye tuko nayo leo. (Ufu. 2:​4, 5) Tunaweza kujiuliza maulizo sawa vile: Ningali nafurahia kusoma Biblia na kutafakari sawa zamani? Ninafikaka ku mikutano yote? Na hata kama ninafikaka, ninatayarishaka mikutano yote? Bidii yangu mu mahubiri ilishapunguka? Ninaanzaka pitisha wakati mingi na niko nafikiria makuta na mambo ya kujifurahisha? Kama unajibia ndiyo ku ulizo hata moya, ile inaweza kuonyesha kama uko na uzaifu fulani. Na kama haufanye kitu juu ya kutengeneza mambo, ule uzaifu unaweza kukufikisha mbali. Kama unashindwa kumaliza ule uzaifu weye peke ao kama tayari ulishavunja kanuni fulani ya Mungu, unapaswa kuomba bazee bakusaidie.

6. Benye bamefanya zambi nzito banapaswa kufanya nini?

6 Bale benye bamefanya zambi nzito yenye inaweza kufanya mutu aondolewe mu kutaniko banapaswa kuzungumuza na bazee. (1 Ko. 5:​11-13) Mutu mwenye amefanya zambi nzito iko na lazima ya musaada juu akuwe tena na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova. Juu Yehova amusamehe kupitia bei ya ukombozi, anapaswa kuonyesha ‘matendo yenye yanaonyesha kwamba ametubu.’ (Mdo. 26:20) Kuzungumuza na bazee ni kati ya ile matendo ya kutubu.

7. Ni ba nani bengine njo biko na lazima ya musaada wa bazee?

7 Ni kweli kama bazee banasaidia bale benye balifanya zambi nzito, lakini banasaidia pia benye biko zaifu kiroho. (Mdo. 20:35) Kwa mufano, pengine unaona kama unashindwa kupiganisha tamaa za mubaya. Inaweza kuwa nguvu zaidi sana kwa bale benye mbele bajifunze kweli balikuwa natumikisha dawa za kulewesha, balikuwa naangalia pornografia, ao balikuwa nafanya uasherati. Usiogope kuomba musaada. Unaweza kuamua kuzungumuza na muzee fulani. Atakusikiliza, atakupatia mashauri kuhusu mambo yenye unaweza kufanya, na atakuhakikishia kama utamufurahisha Yehova ikiwa unaendelea kupiganisha tamaa za mubaya. (Muh. 4:12) Ikiwa umevunjika moyo juu hauyaweza kumaliza tamaa fulani ya mubaya, bazee batakukumbusha kama ikiwa unajisikia vile ni kusema unaona urafiki wako pamoya na Yehova kuwa wa maana na kama haujitumainie kupita kiasi.—1 Ko. 10:12.

8. Ni lazima tuzungumuze na bazee juu ya kila tatizo yenye tuko nayo? Fasiria

8 Haiko lazima kuenda kuona bazee juu ya kila tatizo yenye tuko nayo. Kwa mufano, unasema kitu fulani yenye inakwaza ndugu ao dada, ao unashindwa kuzuia kasirani yako. Kuliko kuenda kuonana na muzee unaweza tu kutumikisha mashauri ya Yesu kuhusu namna ya kufanya amani pamoya na ndugu ao dada yako. (Mt. 5:​23, 24) Unaweza pia kutafuta habari kuhusu upole, uvumilivu na kujizuia juu zile sifa zinaweza kukusaidia hata siku ingine. Lakini kama unashindwa tu kumaliza tatizo yako unaweza kuomba muzee fulani akusaidie. Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Wafilipi aliomba ndugu fulani mwenye Biblia haitaye jina asaidie Euodia na Sintike baelewane tena. Vilevile muzee fulani mu kutaniko yenu anaweza kusaidia mu ile njia.—Flp. 4:​2, 3.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUITA BAZEE?

9. Juu ya nini hatupaswe kuacha haya ituzuie kuzungumuza na bazee? (Mezali 28:13)

9 Inaomba imani na uhodari juu ya kuomba musaada wakati tunafanya zambi nzito ao wakati tunashindwa kupiganisha uzaifu fulani. Tusiache haya ituzuie kuzungumuza na bazee. Juu ya nini? Juu Yehova njo aliweka ile mupango. Kwa hiyo, wakati tunazungumuza na bazee tunaonyesha kama tunamutumainia na tunamutii. Yehova aliweka ile mupango ili kutusaidia tuendelee kuwa nguvu kiroho na tuendelee kuwa na imani yenye nguvu. Tunajua kama tuko na lazima ya musaada wake juu tuendelee kuwa waaminifu. (Zb. 94:18) Na kama tulifanya zambi, Mungu atatuonyesha rehema kama tunatubu na tunaacha kufanya mambo ya mubaya.—Soma Mezali 28:13.

10. Nini inaweza kutokea kama tunajaribu kuficha zambi?

10 Tumeona kama tutapata faida kama tunatafuta musaada wa bazee. Lakini kama tunajaribu kuficha zambi yetu, hali yetu itakuwa mubaya zaidi. Wakati Mufalme Daudi alificha zambi yake, hali yake ya kiroho iliharibika, alikuwa na huzuni, na hata alisikia maumivu ya kimwili. (Zb. 32:​3-5) Sawa tu vile hali ya mugonjwa mwenye hatunziwe mbio inaharibikaka zaidi, kama mutu mwenye iko na tatizo ya kiroho hatafute musaada, hali yake inaharibikaka zaidi. Yehova anajua ile, njo maana anatuambia “tunyooshe mambo” pamoya naye kwa kuzungumuza na bazee juu tupone kiroho.—Isa. 1:​5, 6, 18.

11. Kuficha zambi nzito inaweza kuwa na matokeo gani juu ya bengine?

11 Kama tunaficha zambi nzito, bengine pia banaweza kuteseka. Ile inaweza kufanya roho takatifu ya Mungu isitumike muzuri mu kutaniko na inaweza pia kuvuruga amani ya ndugu na dada. (Efe. 4:30) Na kama tunajua mutu fulani mu kutaniko mwenye alifanya zambi nzito, tunapaswa kumuomba aende kuongea na bazee. Kama tulishamupatia wakati ya kutosha lakini hafanye vile, tunapaswa kuambia bazee mambo yote yenye tunajua. Kama hatufanye vile na siye tuko na kosa. (Law. 5:1) Juu tunamupenda Yehova na tuko washikamanifu kwake, tutakuwa tayari kuzungumuza na bazee na kusema kweli. Kama tunafanya vile, tunasaidia kutaniko iendelee kuwa safi na tunasaidia mwenye alifanya zambi akuwe tena na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova.

BAZEE BANATUSAIDIA NAMNA GANI?

12. Namna gani bazee banasaidia benye biko zaifu kiroho?

12 Biblia inaomba bazee basaidie bale benye kuwa na uzaifu wa kiroho. (1 Te. 5:14) Kama ulifanya zambi, bazee batakuuliza maulizo fulani yenye itabasaidia kushota byenye biko mu akili yako na mu moyo wako. (Mez. 20:5) Pengine iko nguvu kwako kuzungumuza na bazee juu unakuwaka mutu wa haya ao juu unasikia haya kuzungumuzia mambo yenye ilipitikana, lakini unaweza kusaidia bazee kwa kubaelezea waziwazi tatizo yenye uko nayo. Usiogope kusema juu unawaza kama maneno yako itakuwa sawa “mazungumuzo ya ovyoovyo.” (Yob. 6:3) Bazee habatakuhukumu juu ya mambo yenye unasema, lakini batakusikiliza kwa uangalifu juu baelewe muzuri mambo yote mbele bakupatie mashauri ya Biblia. (Mez. 18:13) Banaelewa kama kuchunga kundi inalomba wakati, kwa hiyo banaweza kuzungumuza na weye zaidi ya mara moya juu bakutolee musaada wenye uko nao lazima.

13. Namna gani bazee banatusaidia kupitia sala na Biblia? (Ona pia picha.)

13 Bazee habiko pale juu ya kuingiza kisu mu kilonda, lakini biko pale juu ya kukusaidia. Batasali kwa ajili yako na utashangala kuona vile sala yabo kwa ajili yako iko na “nguvu nyingi” kuliko vile unaweza kuwazia. Zaidi ya ile, juu ya kukusaidia ‘watakupakaa mafuta katika jina la Yehova.’ (Yak. 5:​14-16) Ile “mafuta” ni kweli yenye kuwa mu Neno ya Mungu. Batatumia Biblia muzuri juu ya kukutuliza, kukufariji, na kukusaidia ukuwe tena na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova. (Isa. 57:18) Mashauri ya Biblia yenye batakupatia itakusaidia uazimie kabisa kuendelea kufanya mambo ya muzuri. Kupitia bazee, itakuwa sawa vile uko nasikia sauti ya Yehova iko nakuambia: ‘Hii ndiyo njia. Tembea ndani yake.’—Isa. 30:21.

Picha: 1. Munganga mwenye tuliona ku picha ya kutangulia iko napima mabega ya ule mwanaume. Balifanya radio ya ule mwanaume na picha ya ile radio iko ku kibambazi. 2. Ule muzee wa ku picha ya kutangulia pamoya na muzee mwingine biko natia moyo ule ndugu mu nyumba yake. Ule ndugu iko nasikiliza bazee kwa furaha.

Bazee banatumia Biblia juu ya kutuliza na kufariji benye kugonjwa kiroho (Ona fungu ya 13-14)


14. Sawa vile Wagalatia 6:1 inaonyesha, namna gani bazee banasaidia mutu mwenye amekamata “hatua fulani ya mubaya”? (Ona pia picha.)

14 Soma Wagalatia 6:1. Kukamata “hatua fulani ya mubaya” ni kufanya jambo yenye haimupendeze Yehova. Kwa mufano, Mukristo anakamata hatua ya mubaya wakati anachukua uamuzi wa mubaya ao wakati anafanya zambi nzito. Juu bazee Bakristo biko na upendo, ‘banajaribu kumurekebisha upya mutu huyo kwa roho ya upole.’ Neno ya kigiriki yenye inatafsiriwa “kumurekebisha” ilikuwa natumiwa juu ya kuzungumuzia namna munganga alikuwa narudisha fasi yake mufupa yenye ilivunjika juu mutu aweze kupona muzuri. Sawa vile munganga anajikazaka kurudisha mufupa yenye ilivunjika bila kuongezea mutu maumivu, bazee banajikaza kuponyesha mutu mwenye anagonjwa kiroho bila kumuongezea maumivu. Biblia inaambia pia bazee ‘baendelee kujiangalia.’ Wakati bazee biko nasaidia mutu kutumikisha mashauri ya Biblia, banakumbuka pia kama nabo habakamilike, banaweza kukamata hatua ya mubaya. Bazee habawaze kama abo njo bazuri zaidi kupita mutu mwenye biko nasaidia, na habamuhukumu-hukumu. Lakini, banajikaza kuwa banyenyekevu na benye huruma.—1 Pe. 3:8.

15. Tunaweza kufanya nini kama tuko na tatizo?

15 Tunaweza kutumainia bazee ba kutaniko. Bamezoezwa juu bajue kuchunga siri, batoe mashauri yenye inategemea Biblia hapana mawazo yabo, na baendelee kutusaidia juu tuweze kupiganisha magumu yenye tuko nayo. (Mez. 11:13; Gal. 6:2) Kila muzee iko na utu wake, na bazee bote habana uzoefu uleule. Lakini tunapaswa kujisikia huru kuzungumuza na muzee yeyote juu ya tatizo yetu. Ile haimaanishe kama tutaenda kuona muzee mumoya, kisha mwingine, na kisha mwingine tena juu ya kutafuta mwenye atatuambia mambo yenye tunapenda kusikia. Tukifanya vile tutakuwa sawa batu benye banapendaka ‘masikio yao ifurahishwe,’ kuliko kusikia mambo yenye Yehova anafundisha mu Neno yake. (2 Ti. 4:3) Wakati mutu anaenda kuona muzee fulani juu ya tatizo fulani, ule muzee anaweza kumuuliza kama alishakuongea na bazee bengine na kuuliza kama bale bazee balimupatia shauri gani. Na juu ule muzee ni munyenyekevu anaweza kulomba mashauri kwa bazee bengine.—Mez. 13:10.

JAMBO YENYE KILA MUMOYA WETU ANAPASWA KUFANYA

16. Tunapaswa kufanya nini?

16 Ni kweli kama bazee biko pale juu ya kuchunga kondoo wa Mungu, lakini habatukamatiake maamuzi. Kila mutu anapaswa kuonyesha kupitia maneno na matendo yake kama anapenda Yehova na anapenda kumufurahisha. Na Yehova atatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri na kuendelea kuwa waaminifu. (Ro. 14:12) Njo maana bazee habatukamatiake maamuzi, lakini banatumia Biblia juu ya kutuonyesha mawazo ya Yehova kuhusu jambo fulani na kisha banatuacha tujiamulie. Wakati tunafuata mashauri yabo yenye inategemea Biblia, ile inatusaidia kuzoeza ‘nguvu zetu za utambuzi’ juu tuweze kukamata mashauri ya hekima.—Ebr. 5:14.

17. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

17 Ni pendeleo kubwa sana kuwa kondoo wa Yehova! Yehova alituma Yesu “muchungaji mwema,” juu atoe bei ya ukombozi kwa ajili yetu ili tukuwe na tumaini ya kuishi milele. (Yoh. 10:11) Na kupitia bazee ba kutaniko Yehova anatimiza hii ahadi: “Nitawapatia ninyi wachungaji kulingana na moyo wangu mwenyewe, na watawakulisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu.” (Yer. 3:15) Wakati tunagonjwa kiroho ao tuko bazaifu kiroho, tusisite kuita bazee. Yehova amebaweka juu ya kutusaidia. Tuazimie basi kutafuta musaada wao.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Tunapaswa ‘kuita bazee’ wakati gani?

  • Juu ya nini tunapaswa kuita bazee?

  • Bazee banatusaidia namna gani?

WIMBO 31 Utembee Pamoja na Mungu!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine