Barua ya Baraza Yenye Kuongoza
Muhubiri Mupendwa wa Habari Njema:
Tuko na pendeleo ya ajabu sana ya kumuabudu kwa umoja Mungu wa pekee wa kweli, Yehova! Siye tuko “wafanyakazi” pamoya naye, tuko na kazi ya kuhubiri na kufundisha habari njema ya Ufalme wake wenye uko natawala. Ile ni kazi takatifu na yenye kuokoa uzima. (1 Ko. 3:9; Mt. 28:19, 20) Juu tufanye hii kazi ya kuhubiri mu dunia yote kwa amani na umoja, tunapaswa kufuata utaratibu wa tengenezo ya Mungu.—1 Ko. 14:40.
Hii kitabu itakusaidia uelewe namna kutaniko ya Kikristo iko nafanya kazi leo. Inazungumuzia mapendeleo na madaraka yenye weye Shahidi wa Yehova uko nayo. Kama unafurahia mapendeleo yako na kama uko natimiza muzuri madaraka yako, utaendelea “kuwa nguvu katika imani.”—Matendo 16:4, 5; Gal. 6:5.
Kwa hiyo, tunakutia moyo ujifunze kwa uangalifu hii kitabu. Wakati uko najifunza habari mbalimbali, ujikaze kuona namna gani unaweza kuzitumikisha mu maisha yako. Kwa mufano, kama uko muhubiri mwenye hayabatizwa, ujiulize: Ni mambo gani ingine napaswa kufanya ili nibatizwe na kuwa Shahidi wa Yehova? Kama ulishabatizwa, ujiulize: Ni mambo gani naweza kufanya ili nikomale kiroho na nifanye mambo mingi mu utumishi wangu kwa Yehova? (1 Ti. 4:15) Ninaweza kufanya nini ili kutaniko iendelee kuwa na amani? (2 Ko. 13:11) Utapata majibu ya ile maulizo mu hii kitabu.
Kama uko mwanaume mwenye kubatizwa, ni mambo gani unaweza kufanya ili ustahili kuwa mutumishi wa huduma na kisha ukuwe muzee mu kutaniko? Juu watu wengi wanaendelea kuya mu tengenezo ya Mungu, kuko lazima sana ya wanaume wenye kustahili ili kusimamia makutaniko. Mu hii kitabu utaona mambo yenye kuombwa ili ‘ujikaze’ kufikia ile miradi ya kiroho.—1 Ti. 3:1.
Tunasali kwa moyo wote ili hii kitabu ikusaidie uelewe na kufurahia fasi yako katika mupango wa Yehova. Tunawapenda sana nyie wote na tunasali ili mukuwe kati ya watu wenye watafurahia kumuabudu milele Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Zb. 37:10, 11; Isa. 65:21-25.
Ndugu zenu,
Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova