Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od uku. 185-192
  • Sehemu ya 1 Mambo Yenye Mukristo Anaamini

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sehemu ya 1 Mambo Yenye Mukristo Anaamini
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Uishi Kulingana na Sala ya Mufano—Sehemu ya 1
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od uku. 185-192

MAULIZO KWA AJILI YA WALE WENYE KUPENDA KUBATIZWA

Sehemu ya 1 Mambo Yenye Mukristo Anaamini

Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kumekusaidia ujue kweli. Bila shaka, mambo yenye umejifunza imekusaidia ukuwe na urafiki wa muzuri pamoya na Mungu, na imekupatia tumaini ya kuishi ku dunia paradiso yenye itatawaliwa na Ufalme wa Mungu. Umeamini kabisa kama Biblia ni Neno ya Mungu, na tayari uko napata baraka mingi juu umeingia mu kutaniko ya Kikristo. Umefurahia kuona namna Yehova iko natendea watumishi wake leo.​—Zek. 8:23.

Juu sasa uko najitayarisha kwa ajili ya ubatizo, itakuwa muzuri wazee wa kutaniko warudilie pamoya na weye mafundisho ya musingi ya Wakristo. (Ebr. 6:1-3) Yehova aendelee basi kubariki bidii yako ya kupenda kumujua, na akupatie zawadi yenye ametuahidi.​—Yoh. 17:3.

1. Juu ya nini unapenda kubatizwa?

2. Yehova ni nani?

• “Yehova ndiye Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani. Hakuna mwingine.”​—Kum. 4:39.

• “Wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”​—Zb. 83:18.

3. Juu ya nini ni muzuri ukuwe natumia jina ya pekee ya Mungu?

• “Basi ninyi munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.’”​—Mt. 6:9.

• “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.”​—Ro. 10:13.

4. Biblia inatumia maneno gani juu ya kuzungumuzia Yehova?

• “Yehova, Muumbaji wa miisho ya dunia, ni Mungu kwa umilele wote.”​—Isa. 40:28.

• “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni.”​—Mt. 6:9.

• “Mungu ni upendo.”​—1 Yo. 4:8.

5. Ni mambo gani yenye unaweza kumupatia Yehova Mungu?

• “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.”​—Mk. 12:30.

• “Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.”​—Lu. 4:8.

6. Juu ya nini unapenda kuwa muaminifu kwa Yehova?

• “Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu, ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.”​—Mez. 27:11.

7. Ni nani njo unaombaka, na unaombaka mu jina ya nani?

• “Kwa kweli kabisa [mimi Yesu] ninawaambia ninyi, kama munamuomba Baba jambo lolote, atawapatia ninyi katika jina langu.”​—Yoh. 16:23.

8. Unaweza kusali juu ya mambo gani?

• “Basi ninyi munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni. Utupatie leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii; na utusamehe madeni yetu, kama vile sisi pia tumesamehe wenye kuwa na madeni yetu. Na usituingize katika jaribu, lakini utukomboe na ule muovu.’”​—Mt. 6:9-13.

• “Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yo. 5:14.

9. Nini inaweza kufanya Yehova asisikilize sala ya mutu?

• “Watamuita Yehova awasaidie, lakini hatawajibu . . . kwa sababu ya matendo yao maovu.”​—Mik. 3:4.

• “Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza sala yao ya kumulilia Mungu, lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya.”​—1 Pe. 3:12.

10. Yesu Kristo ni nani?

• “Simoni Petro akajibu: ‘Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu mwenye kuishi.’”​—Mt. 16:16.

11. Juu ya nini Yesu alikuya ku dunia?

• “Mwana wa binadamu hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine na atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”​—Mt. 20:28.

• “[Mimi Yesu] ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji ingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.”​—Lu. 4:43.

12. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani yako juu ya zabihu ya Yesu?

• “Alikufa kwa ajili ya watu wote ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya ule mwenye alikufa kwa ajili yao na akafufuliwa.”​—2 Ko. 5:15.

13. Yesu iko na mamlaka gani?

• “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”​—Mt. 28:18.

• “Mungu alimuinua kwenye cheo cha juu zaidi na kumupatia kwa fazili jina lenye kuwa juu zaidi ya kila jina lingine.”​—Flp. 2:9.

14. Unaamini kama Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova njo “mutumwa muaminifu na mwenye busara” mwenye Yesu aliweka?

• “Ni nani kwa kweli mutumwa muaminifu na mwenye busara mwenye bwana wake ameweka juu ya watumishi wake wa nyumbani, ili kuwapatia chakula chao kwa wakati wenye kufaa?”​—Mt. 24:45.

15. Roho takatifu ni mutu?

• “Malaika akamujibu: ‘Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu za Mwenye Kuwa Juu Zaidi zitakufunika kwa kivuli. Na kwa hiyo ule mwenye atazaliwa ataitwa mutakatifu, Mwana wa Mungu.’”​—Lu. 1:35.

• “Kwa hiyo, ikiwa ninyi, hata kama muko waovu, munajua kupatia watoto wenu zawadi za muzuri, Baba yenu wa mbinguni atawapatia hata zaidi roho yake takatifu wale wenye kumuomba!”​—Lu. 11:13.

16. Yehova anatumiaka namna gani roho takatifu?

• “Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa, na kwa roho ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.”​—Zb. 33:6.

• “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Mdo. 1:8.

• “Hakuna unabii wa Andiko wenye unatokana na mawazo yoyote ya mutu. Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, lakini wanadamu walisema yenye yalitoka kwa Mungu wakiongozwa na roho takatifu.”​—2 Pe. 1:20, 21.

17. Ufalme wa Mungu ni nini?

• “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moya. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utaponda na kumaliza falme hizi zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.”​—Da. 2:44.

18. Ufalme wa Mungu utakuletea baraka gani?

• “Atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”​—Ufu. 21:4.

19. Nini inafanya ujue kama baraka za Ufalme zitafika hivi karibuni?

• “Wanafunzi wakamukaribia akiwa peke yake, na kusema: ‘Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?’ Yesu akawajibu na kuwaambia: ‘. . . Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine. Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.’”​—Mt. 24:3, 4, 7, 14.

• “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu, wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo.”​—2 Ti. 3:1-5.

20. Unafanyaka nini ili kuonyesha kama Ufalme ni jambo ya maana kwako?

• “Basi, muendelee kutafuta kwanza Ufalme na haki yake.”​—Mt. 6:33.

• “Yesu akaambia wanafunzi wake: ‘Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue muti wake wa mateso na aendelee kunifuata.’”​—Mt. 16:24

21. Shetani na pepo wachafu ni nani?

• “Ninyi mumetoka kwa baba yenu Ibilisi . . . Huyo alikuwa muuaji wakati alianza.”​—Yoh. 8:44.

• “Ule nyoka mukubwa akatupwa chini, ule nyoka wa zamani, mwenye kuitwa Ibilisi na Shetani, mwenye anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu; akatupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.”​—Ufu. 12:9.

22. Shetani alimusingizia Yehova nini na wale wenye wanamuabudu?

• “Mwanamuke akamuambia nyoka: ‘Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu matunda ya muti wenye kuwa katikati ya bustani Mungu amesema: “Hamupaswe kuyakula, hapana, hamupaswe kuyagusa; mukifanya vile mutakufa.”’ Kwa hiyo nyoka akamuambia mwanamuke: ‘Hakika hamutakufa. Kwa sababu Mungu anajua kwamba siku ileile yenye mutakula matunda ya muti huo, macho yenu yatafunguliwa na mutakuwa kama Mungu; mukijua mema na mabaya.’”​—Mwa. 3:2-5.

• “Shetani akamujibu Yehova: ‘Ngozi kwa ngozi. Mutu atatoa kila kitu chenye iko nacho ili aokoe uzima wake.’”​—Yob. 2:4.

23. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama Shetani alidanganya?

• “Umutumikie [Mungu] kwa moyo kamili.”​—1 Ny. 28:9.

• “Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”​—Yob. 27:5.

24. Juu ya nini watu wanakufaka?

• “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”​—Ro. 5:12.

25. Wafu wako mu hali gani?

• “Wazima wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajue kitu chochote.”​—Muh. 9:5.

26. Kuko tumaini gani juu ya wenye washakakufa?

• “Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.”​—Mdo. 24:15.

27. Ni watu ngapi njo wataenda mbinguni ili kutawala na Yesu?

• “Angalia! Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mulima Sayuni, na pamoja naye watu elfu mia moja makumi ine na ine (144 000) wenye kuwa na jina lake na jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye mapaji ya nyuso zao.”​—Ufu. 14:1.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine