Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rj sehemu 5 uku. 12-15
  • Umurudilie ‘Muchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zetu’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Umurudilie ‘Muchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zetu’
  • Umurudilie Yehova
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Munirudilie”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Atakupatia Nguvu
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
  • Yehova Anakupenda Sana!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • “Mimi Mwenyewe, Nitatafuta Kondoo Wangu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Umurudilie Yehova
rj sehemu 5 uku. 12-15

5

Umurudilie ‘Muchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zetu’

Katika broshua hii tumezungumuzia mifano ya watu wenye walipatwa na magumu mbalimbali. Umejisikia kuwa kama mumoja wao? Ikiwa ndiyo, usiwaze kama ni wewe peke. Watumishi wengi waaminifu wa Mungu​—wa zamani na wa siku zetu, walipatwa na magumu kama hayo katika maisha yao. Yehova aliwasaidia na walishinda magumu hayo, wewe pia anaweza kukusaidia.

Yehova atakupokea wakati utamurudilia

UWE hakika kwamba Yehova atakupokea wakati utamurudilia. Atakusaidia upiganishe mahangaiko yako, mambo yenye kuumiza moyo wako. Utakuwa na zamiri safi, na hiyo itakusaidia ukuwe na amani ya akili na ya moyo. Kisha utakuwa na furaha ya kumutumikia tena Yehova pamoja na Mashahidi wenzako. Hali yako itafanana na ile ya Wakristo fulani wa wakati wa mitume. Mutume Petro aliwaandikia Wakristo hao hivi: ‘Mulikuwa kama kondoo, wanaopotea njia; lakini sasa mumerudilia muchungaji na mwangalizi wa nafsi zenu.’​—1 Petro 2:25.

Kumurudilia Yehova ndio jambo muzuri kabisa lenye unaweza kufanya. Juu ya nini? Ukifanya hivyo, utafurahisha moyo wa Yehova. (Methali 27:11) Kama vile unajua, matendo yetu yanaweza kumufurahisha Yehova ao kumusikitisha. Bila shaka, Yehova hatulazimishe tumupende na kumutumikia. (Kumbukumbu 30:19, 20) Mutu mumoja mwenye aliandika sana juu ya Biblia alisema hivi: “Moyo wa mwanadamu ni kama mulango wenye kufungiwa kwa ndani. Ni ule iko ndani tu ndiye anaweza kuufungua.” Tunaweza kufungua mulango huo wa mufano wakati sisi wenyewe tunaamua kumuabudu Yehova kwa moyo wenye kujaa upendo. Moyo kama huo, unatusukuma tumutolee Yehova zawadi za muzuri sana. Kumuabudu Yehova hivyo kunafurahisha moyo wake sana. Kumutolea Yehova ibada yenye anastahili kunaleta furaha sana. Hakuna jambo lingine linaweza kutupatia furaha kama hiyo.​—Matendo 20:35; Ufunuo 4:11.

Dada huyu aliacha kukusanyika na kuhubiri, anakaribishwa kwa furaha katika kutaniko

Tena, wakati unarudilia utumishi wako kwa Yehova, mahitaji yako ya kiroho yatatimizwa. (Mathayo 5:3) Namna gani? Watu wengi wanajiuliza, ‘sababu gani tuko duniani?’ Wako na hamu ao njaa ya kupata majibu ya maulizo kama hayo. Wanadamu wanapenda kujua mambo hayo kwa sababu Yehova aliwaumba na tamaa hiyo. Alituumba tukuwe na furaha wakati tunamutumikia. Wakati tunamuabudu Yehova kwa sababu tunasukumwa na upendo, tutakuwa na furaha ya kweli katika maisha.​—Zaburi 63:1-5.

Tafazali, jua kwamba Yehova anapenda umurudilie. Namna gani unaweza kuwa hakika kwamba anapenda ufanye hivyo? Wazia jambo hili: Tulitayarisha broshua hii kwa uangalifu sana na kisha kusali sana. Pengine ni muzee ndiye alipatia broshua hii ao Shahidi mwengine. Kisha uliisoma na ukafuata mashauri yenye kuwa ndani. Yote hiyo inaonyesha kwamba Yehova hajakusahau. Lakini, anakuvuta kwa upole ili umurudilie.​—Yohana 6:44.

Tunatiwa moyo kujua kwamba Yehova hasahau hata kidogo watumishi wake wenye kupotea. Dada Donna alijionea jambo hilo. Anasema hivi: “Niliacha kweli polepole, lakini mara nyingi nilikuwa ninafikiri sana juu ya Zaburi 139:23, 24, yenye kusema: ‘Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofazaisha [zenye kuhangaika]. Ona kama ndani yangu muko njia yoyote yenye kuumiza [mawazo yoyote mubaya], na uniongoze katika njia ya wakati usio na kipimo [ya milele].’ Nilijua kama sikupaswa kuwa sehemu ya ulimwengu, sikujisikia vizuri humo, na nilijuwa kwamba ni katika tengenezo la Yehova ndimo ninapaswa kuwa. Nilianza kuona kwamba Yehova hajanitupa; iliomba tu nimurudilie. Na ninafurahi sana kwa kuwa nilifanya hivyo!”

“Nilianza kuona kwamba Yehova hajanitupa; iliomba tu nimurudilie”

Tunasali kabisa ili wewe pia upate tena “shangwe ya Yehova.” (Nehemia 8:10) Utaona kwamba haukukosea kwa sababu umemurudilia Yehova.

Pengine Unapenda Kumurudilia Yehova, na Sasa Unajiuliza

NIANZIE WAPI?

Dada huyu aliacha kukusanyika na kuhubiri, anakaribishwa kwa furaha katika kutaniko

Ili mutu mwenye alikuwa mugonjwa arudilie mambo alikuwa anafanya zamani kwa ukawaida, inaweza kuwa lazima afanye hivyo polepole. Vilevile, unaweza kurudilia nguvu yako ya kiroho kwa kujaribu kula chakula cha kiroho kidogo tu kila siku. Usiwaze kama utafanya mambo yote siku moja. Unaweza kutumia dakika kidogo kwa kusoma ao kusikiliza usomaji fulani wa Biblia wenye ulirekodiwa, kujifunza moja ya vichapo ao vitabu vyetu, ao kutafuta habari kwenye adrese yetu ya jw.org. Pia, jaribu bila kukawia kuhuzuria mikutano ya kutaniko. Zaidi ya yote, umuombe Yehova akusaidie. ‘Umutupie mahangaiko yako yote, kwa sababu anakujali [anakuhangaikia] wewe.’​—1 Petro 5:7.

“Wakati niliacha kuhubiri na kukusanyika, nilisikia hata haya ya kusali. Wakati nilipata nguvu ya kusali, muzee mumoja wa kutaniko letu alinitembelea. Alinisaidia nielewe kwamba Yehova hakunitupa. Muzee huyo alinishauri nianze kwanza kusoma Biblia kila siku. Wakati nilifanya hivyo, nilipata nguvu ya kuanza tena kukusanyika. Kisha wakati fulani, nilianza tena kuhubiri. Nafurahi sana kwa sababu Yehova hakunitupa hata kidogo.”​—Dada Eeva.

KUTANIKO LITANIPOKEA NAMNA GANI?

Ukuwe hakika kwamba ndugu na dada katika kutaniko watakupokea kwa furaha sana. Kuliko kukuchekea ao kukuhukumu, watakuonyesha upendo wao na kufanya yote yenye wanaweza ili kukutia moyo.​—Waebrania 10:24, 25.

“Nilisikia haya sana kurudi ku Jumba la Ufalme. Nilijiuliza namna ndugu na dada wataniona. Dada mumoja mwenye kuzeeka, mwenye alikuwa katika kutaniko hilo kwa miaka 30 aliniambia hivi: ‘Karibu nyumbani, Kijana!’ Hilo lilinigusa moyo sana. Nilijisikia kuwa nyumbani kabisa.”​—Ndugu Javier.

“Nilienda ku Jumba la Ufalme na nikaikala ku kiti cha mwisho ili nisionekane. Lakini, wengi walinitambua, kwa sababu walinijua tangu utoto, wakati nilikuwa nakusanyika. Walinikaribisha na kunikumbatia ao kunipokea kwa upendo. Hilo lilifanya nijisikie vizuri kuwa kati yao. Ilikuwa kama vile nilirudi nyumbani.”​—Ndugu Marco.

WAZEE WATANISAIDIA NAMNA GANI?

Wazee watakutendea kwa upole. Watakushukuru kwa sababu unaonyesha nia ya kurudisha tena “upendo uliokuwa nao mwanzoni.” (Ufunuo 2:4) Watakusaidia kwa upole utengeneze kila jambo lenye uliharibisha, watafanya hivyo “katika roho ya upole.” (Wagalatia 6:1; Methali 28:13) Wazee watatafuta ndugu ao dada fulani mwenye mutajifunza naye Biblia, pengine katika kitabu kama vile Furahia Maisha Milele! ao Mubaki Mkaribie Yehova. Uwe hakika kwamba wazee watakufariji na kukusaidia katika kila hatua yenye utafanya.—Isaya 32:1, 2.

“Niliacha kuhubiri na kukusanyika kwa miaka munane, lakini wazee waliendelea kunitafuta. Siku fulani muzee mumoja alinionyesha picha zenye alitukamataka. Zilinikumbusha mambo mengi mazuri na furaha yenye nilikuwa nayo wakati nilikuwa ninamutumikia Yehova. Wazee walinisaidia kwa upendo nirudilie programu yangu ya kiroho.”​—Ndugu Victor.

“Atakupa tia Nguvu”

Dada huyu aliacha kukusanyika na kuhubiri, anakaribishwa kwa furaha katika kutaniko

Kitabu chetu cha wimbo, Tuimbe kwa Furaha, kiko na nyimbo nyingi zenye kuchochea na zenye zinaweza kukutia moyo wakati unaamua kumurudilia Yehova. Kwa mufano, fikiria maneno ya wimbo namba 38. Yanategemea andiko la 1 Petro 5:10, kichwa cha wimbo huo ni “Atakupatia Nguvu.”

  1. Nini ilifanya Mungu akuite

    Na kukufundisha kweli yake?

    Aliona moyo wako unapenda

    Kumujua na kufanya mema

    Mu sala ulijitoa kwake;

    Hataacha kukusaidia.

  2. Mungu alitoa Yesu, Mwana wake;

    Kusudi ukuwe na furaha.

    Kama Mungu alikutolea Yesu,

    Basi atakupatia nguvu.

    Hatasahau upendo wako.

    Atakuhangaikia sana.

    (KORASI)

    Kwa damu ya Yesu uko mali ya Mungu.

    Hautaanguka, atakupa nguvu.

    Tena atakulinda na kukuongoza.

    Hautaanguka, atakupa nguvu.

Mwimbieni Yehova—Muziki wa Kuimbwa

Ili kusikiliza sauti ya wimbo huu na nyimbo zingine za Ufalme, tumia chombo cha kusoma alama hii Tafuta neno MACHAPISHO > MUZIKI.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine