Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 2 uku. 10-uku. 11 fu. 1
  • Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Tunazeeka na Kufa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Kifo—Adui wa Mwisho Atakayeangamizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kifo cha Yesu na Ufufuo Wake—Vinaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?
    Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 2 uku. 10-uku. 11 fu. 1
Adamu na Eva mu bustani ya Edeni

2

Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza

Yehova alifanya bustani fasi kwenye kuliitwa Edeni. Mu ile bustani mulikuwa maua, wanyama, na miti ya mingi. Kisha, Mungu aliumba mwanaume wa kwanza Adamu, kwa kutumia mavumbi na alipuliza katika matundu ya pua yake pumuzi. Unajua nini ilitokea? Ule mutu akakuwa muzima! Yehova alipatia Adamu kazi ya kuchunga ile bustani, na kazi ya kupatia wanyama wote majina.

Yehova alimupatia Adamu sheria ya lazima sana. Alimuambia: ‘Unaweza kula matunda ya miti yote, lakini usikule matunda ya muti moja. Ukikula matunda ya ule muti utakufa.’

Kisha, Yehova akasema: ‘Nitafanyia Adamu musaidizi.’ Mungu akamulalisha Adamu usingizi muzito, kisha akakamata mbavu moja ya Adamu na akamuumbia bibi. Jina la ule mwanamuke lilikuwa Eva. Adamu na Eva wakakuwa familia ya kwanza. Adamu alijisikia namna gani wakati aliona bibi yake? Alifurahi sana na kusema: ‘Yehova ameumba mwanamuke kutoka katika mbavu yangu! Huyu ni wa kunifanana kabisa.’

Yehova akaambia Adamu na Eva wazae watoto na wajaze dunia. Alitaka wafurahie kufanya kazi pamoja, na kufanya dunia yote ikuwe paradiso, ao shamba la muzuri, sawa vile bustani ya Edeni. Lakini hawakuweza kufanya dunia ikuwe paradiso. Unajua ni juu ya nini? Tutapata jibu mu sura ya kufuata.

“Ule mwenye aliwaumba tangu mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke.”​—Matayo 19:4

Maulizo: Yehova alipatia Adamu kazi gani? Ni nini ingepata Adamu na Eva kama wangekula matunda ya muti wenye Mungu aliwakataza?

Mwanzo 1:27-31; 2:7-9, 15-23; Zaburi 115:16; Matayo 19:4-6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine