Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ll sehemu 3 uku. 8-9
  • Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?
  • Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Walimusikiliza Shetani, Walipatwa na Nini?
    Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
  • Sehemu ya 3
    Umusikilize Mungu
  • Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
ll sehemu 3 uku. 8-9

SEHEMU YA 3

Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?

Yehova alipatia Adamu na Eva vitu mingi vya muzuri. Mwanzo 1:28

Kisha Yehova kumufanya Eva, alipatia Adamu ule mwanamuke

Yehova aliumba Eva, mwanamuke wa kwanza, kisha akamupatia Adamu ule mwanamuke ili akuwe bibi yake.​—Mwanzo 2:21, 22.

Wakati Yehova aliwaumba, aliwapatia akili kamilifu na mwili mukamilifu, hawakukuwa hata na uzaifu.

Adamu na Eva wanaangalia Paradiso nafasi kwenye wanaishi

Walikuwa wanaishi mu bustani ao shamba ya Edeni, ilikuwa nafasi ya muzuri sana. Mu ile bustani mulikuwa mutoni, miti ya matunda, na wanyama.

Yehova alikuwa anazungumuza na Adamu na Eva; alikuwa anawafundisha. Kama wangemusikiliza, wangeishi milele mu Paradiso ku dunia.

Mungu aliambia Adamu na Eva wasikule matunda ya muti moja kati ya miti ya mu bustani. Mwanzo 2:16, 17

Ule muti wenye ulikuwa mu bustani wenye Yehova aliambia Adamu na Eva wasikule matunda yake

Mu bustani ya Edeni, Yehova alionyesha Adamu na Eva muti moja wa matunda na akawaambia kama wakikula matunda ya muti huo watakufa.

Malaika mubaya, Shetani Ibilisi, anatumia nyoka ili kuzungumuza na Eva

Malaika mumoja alimupinga Mungu. Ule malaika mubaya anaitwa Shetani Ibilisi.

Shetani hakupenda Adamu na Eva wamutii ao kumusikia Yehova. Basi, alitumia nyoka ili kumuambia Eva kama akikula matunda ya muti huo hatakufa, lakini atakuwa sawa na Mungu. Alimudanganya kabisa.​—Mwanzo 3:1-5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine