Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 3 uku. 14-uku. 15 fu. 3
  • Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?
    Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
  • Mungu Anaweza Kuhuzunika​—Namna Tunavyoweza Kumufurahisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tunaenda Wapi Wakati Tunakufa?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Sehemu ya 3
    Umusikilize Mungu
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 3 uku. 14-uku. 15 fu. 3
Adamu na Eva wanatoka mu bustani ya Edeni

3

Adamu na Eva Walikataa Kumutii Mungu

Adamu anakamata tunda lenye Eva alimupatia, tunda lenye Mungu aliwakataza

Siku moja wakati Eva alikuwa peke yake, nyoka alisema naye. Alimuuliza hivi: ‘Kweli kabisa Mungu aliwakataza kula matunda ya miti yote?’ Eva alijibia hivi: ‘Tunaweza kula matunda ya miti yote, alitukataza tu matunda ya muti moja. Tukikula matunda ya ile muti, tutakufa.’ Nyoka akamuambia: ‘Hamutakufa. Kwa kweli, mukikula matunda ya ile muti, mutakuwa sawa Mungu.’ Nyoka alisema kweli? Hapana, alisema uongo. Lakini Eva aliamini ile maneno. Eva alianza kuangalia matunda ya ile muti, mupaka akaitamani. Alikula ile tunda na kisha akapatia Adamu. Adamu alijua kama wakikataa kumutii Mungu watakufa. Lakini, aliikula tu.

Adamu na Eva wanatoka mu bustani ya Edeni, njia ya kuingia mu bustani iko inachungwa na malaika na upanga murefu wenye kuwaka moto

Kisha wakati fulani, ileile siku, Yehova alisema na Adamu na Eva. Aliwauliza juu ya nini walikataa kumutii. Eva alisema ni kosa la nyoka, na Adamu akasema ni kosa la Eva. Juu Adamu na Eva hawakumutii Yehova, aliwafukuza mu bustani. Ili wasirudie tena mu bustani, Mungu alitia malaika na upanga murefu wenye kuwaka moto mu njia ya kuingia mu bustani.

Yehova alisema atapatia malipizi ule mwenye alidanganya Eva. Haiko kabisa nyoka njo alisemaka na Eva. Yehova hakuumba nyoka na uwezo wa kusema. Ni malaika mubaya njo alifanya nyoka aseme. Alifanya vile juu amudanganye Eva. Ule malaika anaitwa Shetani Ibilisi. Wakati wenye kuja, Yehova atamuharibu Shetani ili asiendelee kudanganya watu wafanye mambo ya mubaya.

“Ibilisi . . . alikuwa muuaji tangu mwanzo, na hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haiko ndani yake.”​—Yohana 8:44, maelezo ya chini

Maulizo: Juu ya nini Eva alikula tunda? Nini ilipata Adamu na Eva wakati walikataa kumutii Yehova? Shetani Ibilisi ni nani?

Mwanzo 3:1-24; Yohana 8:44; 1 Yohana 3:8; Ufunuo 12:9

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine