Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 9 uku. 28-uku. 29 fu. 1
  • Wanapata Sasa Mutoto!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wanapata Sasa Mutoto!
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sara, Mama ya Wafalme
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • ‘Wewe Ni Mwanamuke Mwenye Sura Nzuri’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Abrahamu Alikuwa Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Abrahamu na Sara Walimutii Mungu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 9 uku. 28-uku. 29 fu. 1
Sara iko mu hema na iko anasikiliza wakati Abrahamu iko anazungumuza na malaika

9

Wanapata Sasa Mutoto!

Abrahamu na Sara walikuwa wamefanya miaka mingi sana tangu waoane. Waliacha nyumba yao ya muzuri kule Uru na walianza kuishi mu mahema. Lakini Sara hakukataa sababu alimutegemea Yehova.

Sara alipenda sana kupata mutoto. Aliambia Abrahamu: ‘Kama mutumishi wangu Hagari anazaa mutoto, ule mutoto atakuwa sawa mutoto wangu.’ Kisha wakati fulani, Hagari alizaa mutoto mwanaume; aliitwa Ishmaeli.

Sara iko na mimba

Kisha miaka mingi kupita, wakati Abrahamu alikuwa na miaka 99 na Sara miaka 89, wageni watatu waliwatembelea. Abrahamu aliwakaribisha ili wapumuzike chini ya muti na wakule chakula. Unajua wale wageni walikuwa nani? Walikuwa malaika! Waliambia Abrahamu: ‘Mwaka wenye kuja, wakati kama huu, wewe na bibi yako mutapata mutoto.’ Sara alikuwa mu hema yake na alikuwa anasikiliza. Alicheka mu moyo na kuwaza: ‘Ninaweza kweli kuzaa mutoto, hata kama niko muzee?’

Mwaka wenye ulifuata, Sara alizaa mutoto mwanaume, sawa vile malaika wa Yehova alimuambiaka. Abrahamu alipatia ule mutoto jina Isaka. Isaka maana yake “Kucheka.”

Wakati Isaka alikuwa na miaka karibu tano, Sara aliona Ishmaeli iko anamucheka Isaka. Kwa sababu alipenda kulinda mutoto wake, aliambia Abrahamu afukuze Hagari na Ishmaeli. Abrahamu alikataa kwanza. Lakini Yehova aliambia Abrahamu: ‘Usikilize Sara. Nitamulinda Ishmaeli. Lakini ni kupitia Isaka njo nitatimiza ahadi zangu.’

Sara na Isaka wanaangalia Hagari na Ishmaeli wakati wanaenda

“Kwa imani Sara pia alipokea nguvu za kupata uzao, . . . kwa kuwa alimuona Ule mwenye alikuwa ameahidi kuwa ni muaminifu.”​—Waebrania 11:11

Maulizo: Sara alisikia malaika wanaambia Abrahamu nini? Namna gani Yehova alilinda Isaka?

Mwanzo 16:1-4, 15, 16; 17:25-27; 18:1-15; 21:1-14; Waebrania 11:11

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine