Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 21 uku. 54-uku. 55 fu. 2
  • Pigo ya Kumi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Pigo ya Kumi
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mapigo Tatu ya Kwanza
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Musa Alichagua Kumuabudu Yehova
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Mapigo Ingine Sita
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Maana ya Pasaka kwa Wakristo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 21 uku. 54-uku. 55 fu. 2
Mwanaume Mwisraeli anapakaa damu ku miimo ya mulango yake

21

Pigo la Kumi

Musa aliambia Farao kama hangeonana naye tena. Lakini mbele atoke kwa Farao alimuambia: ‘Katikati ya usiku, kila mutoto wa kwanza katika inchi ya Misri, kuanzia mutoto wa kwanza wa Farao mupaka mutoto wa kwanza wa watumwa, atakufa.’

Yehova aliambia Waisraeli watayarishe chakula cha pekee. Alisema: ‘Muchinje kondoo dume ao mbuzi wa mwaka moja, kisha mupakae damu yake ku miimo (encadrement) ya milango ya nyumba zenu. Muchome ile nyama na kuikula na mukate yenye haina chachu. Muvae nguo na viatu na mukuwe tayari kuenda. Usiku wa leo nitawakomboa.’ Hauone kama Waisraeli walipaswa kufurahi kabisa?

Katikati ya usiku, malaika wa Yehova alipita ku kila nyumba mu inchi ya Misri. Mutoto wa kwanza wa kila nyumba yenye haikupakaliwa damu ku miimo ya mulango, alikufa. Lakini ule malaika aliacha nyumba zenye zilikuwa zimepakaliwa damu. Kila mutoto wa kwanza alikufa mu kila familia ya Wamisri, za matajiri na maskini. Lakini hakuna mutoto Mwisraeli mwenye alikufa.

Hata mutoto wa Farao alikufa. Farao hakuweza kuvumilia tena. Palepale akaambia Musa na Haruni: ‘Musimame. Mutoke hapa. Muende muabudu Mungu wenu. Mukamate wanyama wenu na muende!’

Ule usiku wenye Waisraeli walitoka Misri, mwezi ilikuwa yote muviringo. Walikuwa wamepangwa kulingana na familia na makabila yao. Kulikuwa wanaume Waisraeli 600000, na wanamuke na watoto wengi. Na watu wengine wengi walienda pamoja nao ili wamuabudu Yehova. Sasa Waisraeli walikuwa huru kabisa!

Ili kukumbuka vile Yehova aliwakomboa, kila mwaka walikuwa wanatayarisha ile chakula ya pekee, yenye inaitwa Pasaka.

Waisraeli wanatoka Misri

“Kwa sababu hii nimekuacha ubakie: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”​—Waroma 9:17

Maulizo: Pigo ya kumi ilikuwa nini? Waisraeli walipaswa kufanya nini ili kujilinda wakati wa ile pigo?

Kutoka 11:1–12:42; 13:3-10

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine