UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 12
Maana ya Pasaka kwa Wakristo
Ili Waisraeli wasipatwe na pigo la kumi, walipaswa kutii maagizo. (Kut 12:28) Usiku wa Nisani 14, kila familia ilipaswa kukutana mu nyumba yao. Walipaswa kuua mwana-kondoo dume ao mbuzi; wale wanyama walipaswa kuwa na mwaka moja na walipaswa pia kuwa na afya ya muzuri. Na walipaswa kupakaa damu yake kwenye miimo ya milango na muingilio wa milango. Kisha walipaswa kuchoma ule munyama na kumukula haraka. Hakuna mutu mwenye alipaswa kutoka inje ya nyumba mupaka asubui.—Kut 12:9-11, 22.
Utii unatulinda leo mu njia gani mbalimbali?