Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 29 uku. 74-uku. 75 fu. 2
  • Yehova Alichagua Yoshua

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Alichagua Yoshua
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wapelelezi 12
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 29 uku. 74-uku. 75 fu. 2
Makuhani wanabeba sanduku la agano na kuvuka Muto Yordani

29

Yehova Alichagua Yoshua

Yoshua anasoma Sheria

Kisha kuongoza taifa la Israeli kwa miaka mingi, Musa alikuwa karibu kufa. Yehova akamuambia: ‘Haiko wewe njo utaingiza Waisraeli katika Inchi ya Ahadi. Lakini nitakuonyesha ile inchi.’ Kisha Musa akamuomba Yehova achague kiongozi mupya juu aongoze watu. Yehova akamuambia: ‘Uende kwa Yoshua umuambie yeye njo atakuwa kiongozi.’

Musa akaambia taifa lote kama iko karibu kufa na kama Yehova amechagua Yoshua ili akuwe kiongozi mwenye atawaingiza mu Inchi ya Ahadi. Kisha Musa akaambia Yoshua: ‘Usiogope. Yehova atakusaidia.’ Wakati kidogo kisha pale, Musa akapanda juu ya Mulima Nebo, na kule Yehova akamuonyesha inchi yenye alikuwa ametoa ahadi kama ataipatia Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Musa alikuwa na miaka 120 wakati alikufa.

Musa anapatia Yoshua mugao mbele ya kuhani na wanaume wengine

Yehova akaambia Yoshua: ‘Vuka Muto Yordani, na uingie Kanaani. Nitakusaidia sawa vile nilisaidia Musa. Usome Sheria yangu kila siku. Usiogope. Ukuwe hodari. Uende, na ufanye mambo yote yenye nimekuambia.’

Yoshua akatuma wapelelezi wawili waende katika muji wa Yeriko. Mu hadisi ya kufuata, tutaona jambo lenye lilitokea kule. Wakati walirudia, walisema kama ilikuwa wakati wa muzuri wa kuingia Kanaani. Siku yenye ilifuata, Yoshua akaambia taifa lote lijitayarishe kuenda. Kisha akaambia makuhani wenye walikuwa wanabeba sanduku la agano wapite mbele ya taifa na waingie katika Muto Yordani. Muto ulikuwa umejaa maji. Lakini wakati tu miguu ya makuhani ilikanyanga mu maji, muto ikaacha kuteremuka, na maji ikaanza kukauka! Wakati makuhani walifika katikati ya muto wakasimama wakati taifa lote la Israeli lilikuwa linavuka ngambo ingine. Unawaza kama ule muujiza uliwakumbusha jambo lenye Yehova aliwafanyiaka ku Bahari Nyekundu?

Kisha ile miaka yote, Waisraeli waliingia sasa mu Inchi ya Ahadi. Sasa wangeweza kujenga nyumba na miji, kulima mashamba ya chakula, ya mizabibu, na ya matunda. Ile inchi ilikuwa na maziwa na asali mingi.

“Yehova atakuongoza sikuzote na kukushibisha hata katika inchi yenye kukauka.”​—Isaya 58:11

Maulizo: Ni nani aliongoza Waisraeli kisha Musa kufa? Ni nini ilifanyika ku Muto Yordani?

Hesabu 27:12-23; Kumbukumbu la Torati 31:1-8; 34:1-12; Yoshua 1:1–3:17

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine