Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 26 uku. 66-uku. 67 fu. 1
  • Wapelelezi 12

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wapelelezi 12
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Umufuate Yehova kwa Moyo Wako Wote
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Yehova Alichagua Yoshua
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 26 uku. 66-uku. 67 fu. 1
Wanaume Waisraeli wanapeleleza inchi ya Kanaani

26

Wapelelezi 12

Waisraeli walitoka ku Mulima Sinai na kusafiri mu jangwa la Parani mupaka wakafika fasi yenye kuitwa Kadeshi. Wakati walifika kule, Yehova akaambia Musa: ‘Chagua watu 12, mutu mumoja mu kila kabila. Uwatume wapeleleze katika inchi ya Kanaani, yenye nitapatia Waisraeli.’ Kwa hiyo, Musa akachagua wanaume 12 na kuwaambia: ‘Muende katika inchi ya Kanaani muchunguze kama udongo wake unakomalishaka chakula. Muangalie kama watu wa ile inchi ni wazaifu ao kama wako na nguvu na kama wanaishi mu mahema ao mu miji.’ Wale wapelelezi 12 wakaenda Kanaani. Kati yao kulikuwa Yoshua na Kalebu.

Waisraeli wanalalamika na kuvunjika moyo

Kisha siku 40, wale wapelelezi wakarudia na matunda ya tini, makomamanga, na zabibu. Wale wapelelezi wakasema: ‘Ni inchi ya muzuri, lakini watu wenye wanakaa ndani wako na nguvu na miji yake iko na kuta za murefu sana.’ Kisha Kalebu akasema: ‘Tunaweza kupata ushindi. Tuende mara moja!’ Unajua ni juu ya nini Kalebu alisema vile? Ni juu yeye na Yoshua walimutegemea Yehova. Lakini wale wapelelezi wengine kumi wakasema: ‘Hapana! Wale watu ni warefu na wanene! Tulikuwa kama panzi mbele yao.’

Waisraeli walivunjika moyo. Wakaanza kulalamika na kuambiana: ‘Tuchague kiongozi mwengine aturudishe Misri. Juu ya nini tujipeleke katika hatari ili tukufe?’ Yoshua na Kalebu wakasema: ‘Mumutii Yehova, na musiogope. Yehova atatulinda.’ Lakini Waisraeli hawakusikiliza. Walianza hata kutafuta kuua Yoshua na Kalebu!

Yehova alifanya nini? Aliambia Musa: ‘Nimefanyia Waisraeli mambo ya mingi, lakini hawanitii. Njo maana watafanya miaka 40 mu hii jangwa na watakufia humu. Watoto wao, na Yoshua, na Kalebu njo tu wataishi katika inchi yenye nilisema nitawapatia.’

“Sababu gani munaogopa sana, ninyi wenye imani kidogo?”​—Matayo 8:26

Maulizo: Ni mambo gani ilifanyika wakati wapelelezi 12 walirudia kutoka Kanaani? Yoshua na Kalebu walifanya nini yenye ilionyesha kama walimutegemea Yehova?

Hesabu 13:1–14:38; Kumbukumbu la Torati 1:22-33; Zaburi 78:22; Waebrania 3:17-19

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine