UTAJIRI WA NENO LA MUNGU
Umufuate Yehova kwa Moyo Wako Wote
Kalebu alimufuata Yehova kwa moyo wake wote wakati alikuwa kijana (Yos 14:7, 8)
Hata wakati alizeeka, aliendelea kumutegemea Yehova juu amusaidie kutimiza mugawo yake ya nguvu (Yos 14:10-12; w04-SW 1/12 uku. 12 fu. 2)
Kalebu alibarikiwa juu alimutumikia Yehova kwa moyo wake wote (Yos 14:13, 14; w06-SW 1/10 uku. 18 fu. 11)
Yehova alibariki Kalebu juu alifuata muongozo wake. Ile ilifanya imani ya Kalebu ikuwe nguvu. Wakati tunajionea namna Yehova iko najibia sala zetu na kutuongoza mu njia mbalimbali, ile inatupatia nguvu ya kuendelea kumutumikia.—1Yo 5:14, 15.