60
Ufalme Wenye Utaendelea Milele
Usiku moja, Mufalme Nebukadneza alilota ndoto ya kushangaza. Ile ndoto ilimusumbua sana mupaka akakosa usingizi. Kisha, akaita watu wake wenye kufanya uchawi na kuwaambia: ‘Munifasirie maana ya ndoto yenye nililota.’ Wakamuambia: ‘Tuelezee kwanza ile ndoto, Ee mufalme.’ Lakini Nebukadneza akawaambia: ‘Sitawaelezea! Nyiye muniambie mambo yenye nililota. Kama munashindwa, nitawaua.’ Wakamuambia tena: ‘Tuelezee kwanza ndoto yenye ulilota, kisha tutakufasiria maana yake.’ Akasema: ‘Munataka kunidanganya. Munielezee kwanza ndoto yenye nililota!’ Wakamuambia: ‘Haiwezekane. Hakuna mutu mwenye anaweza kufanya vile.’
Nebukadneza alikasirika sana, na akatoa amri yenye kusema kama watu wote wenye hekima wauawe. Kwa hiyo, Danieli, Shadraki, Meshaki, na Abednego, walipaswa pia kuuawa. Lakini Danieli akaambia mufalme amuachie wakati kidogo. Kisha, yeye na marafiki wake wakasali na kumuomba Yehova awasaidie. Yehova alifanya nini?
Kupitia maono, Yehova alionyesha Danieli ndoto yenye Nebukadneza alilota na akamujulisha maana yake. Siku yenye ilifuata, Danieli akaenda kwa mutumishi wa mufalme na kumuambia: ‘Usiue watu wenye hekima. Mimi nitafasiria maana ya ndoto yenye mufalme alilota.’ Ule mutumishi akapeleka Danieli mbele ya Nebukadneza. Danieli akaambia mufalme: ‘Mungu amekujulisha mambo yenye itatokea. Ulilota hivi: Uliona sanamu kubwa. Ilikuwa na kichwa cha zahabu, kifua na mikono ya feza, tumbo na mapaja ya shaba, miguu ya chuma, na vikanyangio vya chuma yenye inachanganywa na udongo. Kisha, jiwe lilitoka ku mulima, na likapiga vikanyangio vya ile sanamu. Ile sanamu ikapondekana na kuwa vumbi, na upepo ukaipeleka mbali. Kisha, lile jiwe likakuwa mulima mukubwa na likaenea mu dunia yote.’
Kisha Danieli akasema: ‘Hii njo maana ya ndoto yako: Ufalme wako njo kichwa cha zahabu. Feza inafananisha ufalme wenye utaanza kutawala kisha ufalme wako. Kisha kutakuwa Ufalme wenye kufananishwa na shaba wenye utatawala dunia yote. Ufalme wenye utafuata utakuwa nguvu sawa chuma. Na ku mwisho, kutakuwa ufalme wenye kugawanyika: utakuwa na sehemu fulani zenye nguvu sawa chuma na zingine zitakuwa zaifu sawa udongo. Jiwe lenye liligeuka mulima ni Ufalme wa Mungu. Utaharibu hizi falme zote, na utaendelea milele.’
Nebukadneza akainamisha uso mupaka chini mbele ya Danieli. Akamuambia: ‘Mungu wako njo alikufunulia ndoto yenye nililota. Kwa kweli, hakuna Mungu mwenye iko sawa yeye.’ Kuliko kuua Danieli, Nebukadneza alimufanya kuwa mukubwa wa watu wote wenye hekima. Tena, alimufanya kuwa mukubwa wa eneo la Babiloni. Unaona namna Yehova alijibu sala ya Danieli?
“Na yakawakusanya pamoja mahali kwenye kunaitwa katika Kiebrania Armagedoni.”—Ufunuo 16:16