Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 75 uku. 178-uku. 179 fu. 4
  • Ibilisi Anamujaribu Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ibilisi Anamujaribu Yesu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Tunaweza Kujifunza Kupitia Namna Yesu Alipambana na Majaribu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 75 uku. 178-uku. 179 fu. 4
Yesu anakataa kujitupa chini kutoka ku sehemu ya juu sana ya hekalu

75

Ibilisi Anamujaribu Yesu

Yesu anakataa kugeuza majiwe ikuwe mukate

Kisha Yesu kubatizwa, roho takatifu ilimuongoza aende mu jangwa. Alifanya kule siku 40, bila kula. Kisha alisikia njaa sana. Halafu Ibilisi akakuja ili amujaribu. Akamuambia: ‘Kama uko Mutoto wa Mungu, ambia hii majiwe ikuwe mikate.’ Lakini Yesu akamujibu kwa kutaja Maandiko. Akamuambia: ‘Imeandikwa kama, ili mutu aishi, hana lazima ya chakula peke yake. Anapaswa pia kusikiliza kila neno lenye Yehova anasema.’

Kisha, Ibilisi akamujaribu mara ya pili. Akamuambia: ‘Kama uko kabisa Mutoto wa Mungu, ujitupe chini kutoka kwenye sehemu ya juu sana ya hekalu. Imeandikwa kama Mungu atatuma malaika zake juu wakubebe katika mikono yao.’ Lakini Yesu akajibu tena kwa kutaja Maandiko. Akasema: ‘Imeandikwa kama haupaswe kumujaribu Yehova.’

Yesu anakataa falme zote za dunia zenye Shetani anataka kumupatia

Kisha, Shetani akamuonyesha Yesu falme zote za dunia, na utajiri na utukufu wa zile falme. Halafu akamuambia Yesu: ‘Nitakupatia hizi falme zote na utukufu wazo kama unaniabudu mara moja tu.’ Lakini Yesu akamujibu: ‘Toka mbele yangu, Shetani! Imeandikwa kama Yehova tu njo unapaswa kuabudu.’

Kisha, Ibilisi akamuacha, na malaika wakakuja na kumupatia Yesu chakula. Kuanzia wakati huo, Yesu akaanza kuhubiri habari njema ya Ufalme. Njo kazi yenye Mungu alimutumaka akuje kufanya ku dunia. Watu walipenda sana mambo yenye Yesu aliwafundisha, na walikuwa wanamufuata fasi yote kwenye alikuwa anaenda.

“Wakati [Ibilisi] anasema uongo, anasema kulingana na muelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni muongo na baba ya uongo.” ​—Yohana 8:44

Maulizo: Ni majaribu gani tatu yenye Yesu alipata? Namna gani Yesu alimujibu Ibilisi?

Matayo 4:1-11; Marko 1:12, 13; Luka 4:1-15; Kumbukumbu la Torati 6:13, 16; 8:3; Yakobo 4:7

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine