77
Mwanamuke Kwenye Kisima
Kisha Pasaka, Yesu na wanafunzi wake walipitia Samaria wakati walikuwa wanarudia Galilaya. Wakati walifika karibu na muji wa Sikari, Yesu alisimama fasi yenye iliitwa kisima cha Yakobo. Wakati alikuwa anapumuzika pale, wanafunzi wake walienda kuuza chakula katika muji.
Mwanamuke mumoja alikuja kwenye kisima hicho ili kushota maji. Yesu akamuambia: “Nipatie maji nikunywe.” Ule mwanamuke akasema: ‘Juu ya nini unazungumuza na mimi? Mimi niko Musamaria. Wayahudi hawazungumuzake na Wasamaria.’ Yesu akamuambia: ‘Kama ungejua niko nani, ungeniomba maji na ningekupatia maji ya uzima.’ Halafu ule mwanamuke akamuuliza, ‘Unataka kusema nini? Hauna hata chombo cha kushotea maji.’ Yesu akasema: ‘Mwenye anakunywa maji yenye ninamupatia hatasikiaka kiu tena.’ Kisha, ule mwanamuke akasema: ‘Bwana, nipatie ile maji.’
Yesu akamuambia: ‘Uende uambie bwana yako akuje hapa.’ Ule mwanamuke akasema: ‘Sina bwana.’ Yesu akamuambia: ‘Unasema kweli. Uliolewaka mara tano. Na kwa sasa, uko unaishi na mwanaume mwenye haiko bwana yako.’ Ule mwanamuke akasema: ‘Ninaona kuwa uko nabii.’ Kisha akasema: ‘Sisi tunaamini kama tunaweza kumuabudu Mungu kwenye mulima huu, lakini Wayahudi wanasema kama tunapaswa kumuabudu Mungu kule Yerusalemu tu. Mimi, ninaamini kama wakati Masiya atakuja, atatufundisha namna ya kuabudu.’ Halafu Yesu akamuambia: ‘Mimi njo Masiya.’ Alikuwa hajaambiaka mutu mwingine kama yeye njo Masiya.
Palepale ule mwanamuke akarudia mu muji wao na kuambia watu hivi: ‘Ninawaza nimeonana na Masiya. Anajua mambo yangu yote. Mukuje muone!’ Wasamaria wakamufuata mupaka kwenye kisima na wakasikiliza mafundisho ya Yesu.
Kisha Wasamaria wakamuomba Yesu abakie katika muji wao. Yesu aliwafundisha kwa siku mbili, na watu mingi wakamuamini. Na waliambia ule mwanamuke Musamaria: ‘Kisha kusikiliza ule mwanaume, sasa tunajua kama yeye njo mwokozi wa ulimwengu.’
“‘Kuja!’ Na kila mutu mwenye kuwa na kiu akuje; kila mutu mwenye anataka achukue maji ya uzima bure.”—Ufunuo 22:17