Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 93 uku. 216-uku. 217 fu. 5
  • Yesu Anarudia Mbinguni

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anarudia Mbinguni
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mamia Wanamuona Mbele ya Pentekoste
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Mutakuwa Mashahidi Wangu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 93 uku. 216-uku. 217 fu. 5
Mitume wanaangalia namna Yesu anapanda mbinguni

93

Yesu Anarudia Mbinguni

Yesu alikutana na wanafunzi wake kule Galilaya. Aliwapatia amri hii ya maana sana: ‘Muende mufanye wanafunzi mu inchi zote. Muwafundishe mambo yenye niliwafundisha, na muwabatize.’ Kisha aliwatolea ahadi hii: ‘Musisahau: Nitakuwa pamoja na ninyi kila siku.’

Kwa siku 40 kisha Yesu kufufuliwa, alitokea wanafunzi wengi katika Galilaya na Yerusalemu. Aliwafundisha mambo ya maana na alifanya miujiza mingi. Kisha, Yesu alikutana na mitume wake mara ya mwisho, ku Mulima wa Mizeituni. Aliwaambia: ‘Musitoke Yerusalemu. Muendelee kungoja ahadi yenye Baba aliwatolea.’

Lakini mitume hawakuelewa. Basi wakamuuliza: ‘Ni wakati huu njo utakuwa Mufalme wa Israeli?’ Yesu akawajibu: ‘Wakati wa Yehova kuniweka nikuwe Mufalme haujafika. Karibuni, mutapokea roho takatifu. Na itawapatia nguvu. Kisha, mutakuwa mashahidi wangu. Muende muhubiri katika Yerusalemu, Yudea, Samaria, na mupaka sehemu za mbali sana za dunia.’

Kisha Yesu akainuliwa juu katika anga na mawingu ikamufunika. Wanafunzi wake wakaendelea kuangalia juu, lakini hawakumuona tena.

Halafu, wanafunzi wakatoka ku Mulima wa Mizeituni na kuenda Yerusalemu. Walikuwa wanakutana pamoja mu chumba cha juu na walikuwa wanasali. Walikuwa wanangoja Yesu awapatie maagizo ingine.

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Matayo 24:1

Maulizo: Yesu alipatia wanafunzi wake amri gani? Ni nini ilitokea ku Mulima wa Mizeituni?

Matayo 28:16-20; Luka 24:49-53; Yohana 20:30, 31; Matendo 1:2-14; 1 Wakorinto 15:3-6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine