Utangulizi wa Sehemu ya 14
Wakristo wa wakati wa mitume walitangaza habari njema ya Ufalme mupaka sehemu ya mbali sana ya dunia. Yesu aliwaambia fasi kwenye walipaswa kuhubiri, na kupitia muujiza, akawapatia uwezo wa kufundisha watu mu luga zao wenyewe. Yehova aliwapatia uhodari na nguvu ya kupambana na mateso makali sana.
Yesu alimuonyesha mutume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono ingine, Yohana aliona namna Ufalme wa mbinguni unapata ushindi juu ya Shetani na kumaliza utawala wa Shetani milele. Yohana aliona Yesu iko anatawala pamoja na wenzake 144000. Tena, aliona dunia yote inakuwa paradiso. Na aliona wanadamu wote wanamuabudu Yehova katika amani na umoja.