Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 102 uku. 236-uku. 237 fu. 2
  • Yohana Anapokea Ufunuo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yohana Anapokea Ufunuo
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maono Kuhusu Wale Wenye Kuishi Mbinguni
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • “Angalia! Kundi Kubwa la Watu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 102 uku. 236-uku. 237 fu. 2
Mutume Yohana anaandika kitabu cha Ufunuo

102

Yohana Anapokea Ufunuo

Wakati mutume Yohana alikuwa mufungwa mu kisiwa cha Patmo, Yesu alimuonyesha maono 16, ao picha ya mambo ya wakati wenye kuja. Ile maono ilionyesha vile jina la Yehova litatakaswa, vile Ufalme wake utakuja, na vile mapenzi yake itafanyika hapa ku dunia sawa vile mbinguni.

Katika maono fulani, Yohana alimuona Yehova amekaa kwenye kiti chake cha ufalme mbinguni. Wazee 24 walikuwa wamemuzunguka. Walikuwa wamevaa nguo za mweupe na mataji ya zahabu ilikuwa juu ya vichwa vyao. Mwangaza wa radi na sauti za mingurumo zilikuwa zinatoka mu kile kiti cha ufalme. Wale wazee 24 waliinama mbele ya Yehova na kumuabudu. Katika maono ingine, Yohana aliona kundi kubwa la watu wenye walikuwa wanamuabudu Yehova: walitoka mu mataifa yote na vikundi vyote vya watu, na luga zote. Mwana-Kondoo, ni kusema Yesu, alikuwa anawachunga na kuwapeleka kwenye maji ya uzima. Kisha, katika maono ingine, Yohana aliona Yesu anaanza kutawala mbinguni pamoja na wale wazee 24. Katika maono ingine, Yohana aliona Yesu iko anapigana na ule nyoka mukubwa, ni kusema Shetani, pamoja na pepo wake wachafu. Yesu aliwafukuza mbinguni na kuwatupa ku dunia.

Yesu na wale 144000 ku Mulima Sayuni

Kisha Yohana aliona maono ya muzuri sana, mu ile maono aliona Mwana-Kondoo amesimama ku Mulima Sayuni na wale 144000. Tena, aliona malaika mwenye alikuwa anaruka mu dunia yote na iko anaambia watu wamuogope Mungu na kumupatia utukufu.

Katika maono ingine, Yohana aliona vita ya Armagedoni. Katika ile vita, Yesu na majeshi yake walipata ushindi juu ya ulimwengu mubaya wa Shetani. Mu maono ya mwisho, Yohana aliona umoja wa muzuri sana kati ya mbingu na dunia. Shetani na wote wenye kuwa upande wake waliharibiwa kabisa. Kisha, watu wote mbinguni na duniani walitukuza jina la Yehova na kumuabudu yeye peke yake.

“Na nitatia uadui kati yako na ule mwanamuke na kati ya uzao wako na uzao wake. Ataponda kichwa chako, na wewe utamupiga kwenye kisigino.”​—Mwanzo 3:15

Maulizo: Yohana aliona maono ngapi? Yesu atafanya nini wakati wa vita ya Armagedoni?

Ufunuo 1:1-3; 4:1-11; 7:4, 9-17; 11:15-18; 12:5-12; 14:6, 7; 16:14, 16; 21:5

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine