Utangulizi wa Sehemu ya 1
Biblia inaanza na habari ya uumbaji. Inatusaidia tuone vitu mingi vya muzuri vyenye Yehova ameumba, ikuwe mbinguni ao ku dunia. Kama uko muzazi, umusaidie mutoto wako aone vitu mbalimbali vya kushangaza vyenye Yehova aliumba. Umuelezee kama Mungu aliumba wanadamu ili wakuwe wa hali ya juu sana kupita wanyama. Alitupatia uwezo wa kuzungumuza, kufikiri, kufanya vitu, kuimba, na kusali. Umusaidie afurahie uwezo na hekima ya Yehova na zaidi sana upendo wake kwa kila mumoja wetu, na kwa viumbe wote.