Utangulizi wa Sehemu ya 4
Mu hii sehemu tutajifunza juu ya Yosefu, Yobu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo ya mingi ya mubaya yenye Shetani aliwaletea. Wamoja kati yao walitendewa bila haki, walifungwa mu gereza, walikuwa watumwa, na hata waliuawa. Lakini, Yehova aliwalinda mu njia mbalimbali. Kama uko muzazi, umusaidie mutoto wako aelewe namna wale watumishi wa Yehova walivumilia mambo ya mubaya bila kupoteza imani yao.
Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha kama iko na nguvu kupita miungu yote ya Wamisri. Onyesha namna Yehova alilinda watu wake wakati wenye ulipita na namna anawalinda leo.