Utangulizi wa Sehemu ya 11
Hii sehemu itakusaidia ujue mambo yenye kuzungumuziwa mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Yesu alizaliwa mu familia ya hali ya chini na waliishi katika muji mudogo. Alifanya kazi na baba yake, mwenye alikuwa seremala. Yesu njo angeokoa wanadamu. Yehova alimuchagua ili akuwe Mufalme wa Ufalme wa mbinguni. Kama uko muzazi, usaidie mutoto wako aelewe kama Yehova alichagua kwa uangalifu ni katika familia gani Yesu angekomalia. Umusaidie aelewe kama Yehova alilinda Yesu juu Herode asimuue, na umusaidie aelewe kama hakuna kitu kinaweza kumuzuia Mungu kutimiza kusudi lake. Umuonyeshe kama Yehova alipatiaka Yohana kazi ya kutayarisha njia kwa ajili ya kuja kwa Yesu. Umufasirie muzuri namna Yesu alionyesha kama alikuwa anapenda mashauri yenye hekima ya Yehova tangu wakati alikuwa mutoto.