Utangulizi wa Sehemu ya 12
Yesu alifundisha watu juu ya Ufalme wa mbinguni. Tena aliwaambia kama inafaa wakuwe wanasali jina la Mungu litakaswe, Ufalme wake ukuje, na mapenzi yake ifanyike ku dunia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe juu ya nini ile sala ni ya maana kwetu. Yesu hakuruhusu Shetani amufanye avunje ushikamanifu wake. Mitume, wenye Yesu alichaguaka njo washiriki wa kwanza wa Ufalme, na wako na kazi ya maana sana katika ule Ufalme. Onyesha mutoto wako kama Yesu alikuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi. Kwa sababu alitaka kusaidia watu, Yesu aliponyesha wagonjwa, alipatia wenye kuwa na njaa chakula, na hata alifufua wafu. Kwa kufanya vile, alionyesha mambo yenye Ufalme utafanyia wanadamu.