Utangulizi wa Sehemu ya 8
Yehova alibariki Sulemani kwa kumupatia hekima ya mingi na alimupatia pendeleo la kujenga hekalu. Lakini, polepole Sulemani alimuacha Yehova. Kama uko muzazi, ufasirie mutoto wako namna watu wenye walikuwa wanaabudu miungu ya uongo walifanya Sulemani aache kumuabudu Yehova. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakafanya watu wakuwe waasi-imani na waabudu-sanamu. Mu ile wakati, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli alifanya watu wa ufalme wa kaskazini wakuwe waasi-imani sana. ule ulikuwa wakati wa mubaya sana mu historia ya Israeli. Lakini kulikuwa kungali watumishi wengi waaminifu wa Yehova, sawa vile Mufalme Yehoshafati na nabii Eliya.