WIMBO 8
Yehova Ni Kimbilio Yangu
Maandishi
1. Yehova Mungu wetu,
Uko kimbilio.
Tunakutegemea;
Hautatuacha.
Utalinda watu wako,
Hata nini itokee.
Mungu tusaidie,
Weye tu njo nguvu yetu.
2. Makumi ya maelfu
Wataanguka tu,
Lakini wenye haki
Wataendelea.
Hatupaswe kuogopa
Musiba ao mateso.
Mungu atatulinda
Chini ya mabawa yake.
3. Sitaogopa simba,
Nyoka na mutego.
Hata kukuwe giza,
Utaniokoa.
Baba, sitatetemeka,
Wala sitahangaika.
Yehova Mungu wangu,
Uko kimbilio yangu.
(Ona pia Zb. 97:10; 121:3, 5; Isa. 52:12.)