WIMBO 19
Chakula cha Mangaribi cha Bwana
Maandishi
1. Yehova Baba wa mbinguni,
Leo siku takatifu!
Zamani ulionyeshaka upendo,
hekima, haki, na nguvu.
Na damu ya mwana-kondoo
Ililinda watu wako.
Na kisha wakati Yesu akakufa
Na kutimiza unabii.
2. Leo mukate na divai
Vinatukumbusha Yesu,
Na faida zote zenye tunapata
Kupitia kifo yake.
Leo siku ya Ukumbusho
Tunamukumbuka Yesu,
Mwenye alilipa bei ya ukombozi
Ili tupate uzima.
3. Yehova tunakusanyika;
Ulitualika hapa
Ili tukusifu kwa upendo wako,
Na kuheshimia Kristo.
Ukumbusho unatufanya
Tukuwe wenye shukrani.
Basi tuige Kristo Mufalme wetu,
Kusudi tuishi milele.
(Ona pia Lu. 22:14-20; 1 Ko. 11:23-26.)