WIMBO 141
Uzima Ni Muujiza
Maandishi
1. Kila mutoto, na mvua yote,
Na jua na chakula: ni zawadi.
Yehova Mungu njo Muumbaji.
Na kila siku tuko tunashangaa.
(REFREE)
Mu maisha yetu, tufanye nini?
Tumupende sana Yehova, Muumbaji.
Tukumbuke kama, uzima wetu ni
Zawadi ya Mungu, na ni muujiza.
2. Watu wengine wako nasema
Kama: “Laani Mungu na ukufe.”
Hatutaiga watu wa vile;
Uzima ni zawadi tutaulinda.
(REFREE)
Mu maisha yetu, tufanye nini?
Tumupende sana Yehova, Muumbaji.
Tukumbuke kama, uzima wetu ni
Zawadi ya Mungu, na ni muujiza.
(Ona pia Yob. 2:9; Zb. 34:12; Muh. 8:15; Mt. 22:37-40; Ro. 6:23.)